HIVI UNAJUA UNAWEZA KUFANYA MIUJIZA HAPA DUNIANI UKIAMUA? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

HIVI UNAJUA UNAWEZA KUFANYA MIUJIZA HAPA DUNIANI UKIAMUA?

MAAJABU
Kufanya muujiza katika jambo lolote lile maishani hakuhitaji mtu kuwa na kitu cha pekee sana zaidi ya kuwa na mabadilio ya kifikra. Unapoamua kubadilisha mtazamo wako kuelekea jambo fulani basi hapo ndiyo umeanza kutenda muujiza na jambo ambalo hapo kabla ulikuwa ukiliona ni gumu haliwezekani kabisa sasa linawezekana.

Watu wote waliowahi kufanya miujiza wakiwemo hata Mitume na Manabii mbalimbali, miujiza hiyo ilianzia kwenye mawazo. Nitatoa mifano ingawa kwa leo sitatumia mifano ya mitume na manabii katika vitabu vitakatifu, mifano hiyo tutaitafutia siku nyingine kutokana na sababu kwamba ni mingi  na inabidi niweze kupitia karibu vitabu vyote vitakatifu vya dini na madhehebu yote makubwa duniani.


Hapa tutaangalia mifano ya miujiza iliyowahi kufanywa na wagunduzi wakubwa 3 duniani ambao vitu walivyogundua kwa hakika mpaka karne nyingi zijazo vitabakia kuwa ndiyo vitu vilivyoibadilisha Dunia yetu hii kwa kiasi kikubwa sana na kuonekana kama vile ilivyo sasa. Maendeleo makubwa yote ya Kisayansi na Kiteknolojia msingi wake mkuu unatokana kwa kiasi kikubwa na uvumbuzi wao. Sisemi mchango wa wagunduzi wengine ni mdogo hapana bali hawa waligundua vitu vya msingi zaidi.

Thomas Edison, Alexander Graham Bell na ndugu wawili Wright Brothers ndio nitakaozungumzia ‘miujiza’ yao leo. Thomas Edson aligundua  mamia ya vitu lakini vilivyompa umaarufu mkubwa zaidi ni taa/balbu ya umeme tunayoitumia hadi leo, spika za redio. Sementi ya kujengea na betri za magari za alkaline.

SOMA: Maajabu ya kufikiri mambo makubwa na kwanini uweke malengo makubwa maishani.


Alexander Bell aligundua Simu zile za waya ambazo kanuni yake ndiyo hiyohiyo imeendelezwa mpaka kufikia hizi simu za mkononi za kisasa tunazotumia leo, aligundua pia gramophone, kifaa kilichotumika kurekodi na kucheza sauti/muziki, muendelezo wake umefanikisha kuwepo kwa player za santuri, cassettes na hata teknolojia nyinginezo za kisasa za kurekodi na kucheza sauti katika makompyuta, simu nk.

Kwa upande wa ndugu wawili Wright Brothers, Orville na Willbur Wright au ‘watoto wa mchungaji’ kama watu walivyopenda kuwaita, wao walifanya ugunduzi wa ndege hizi tunazosafiria kwa mara ya kwanza kabisa.

Ingawa wagunduzi hawa wote 3 walikwishafariki dunia kitambo zaidi ya karne moja iliyopita na waliishi pia katika nyakati tofauti lakini kuna vitu fulani wanavyoshea vinavyowafanya kufanana kikubwa kikiwa, kwanza wote ni wagunduzi wakubwa na pili ni kwamba vitu vyote walivyogundua kuna wakati kabla ya ugunduzi wao vilikuwa ni mawazo matupu(ndoto) katika akili zao.


Vitu vilivyokuwa mawazo matupu akilini mwao hatimaye vikaja kubadilika na kuwa vitu halisi, mashine zilizo na uwezo wa kumrahisishia binadamu kazi zake kwa kiwango cha hali ya juu kabisa.

Mwanzoni katika akili zao walianza tu na mawazo madogo wakifikiria uwezekano wa kuwepo kwa vitu hivyo, kisha mawazo hayo yaliongezeka kidogokidogo na kugeuka kuwa imani yenye nguvu. Na hatimaye basi Imani hizo ndizo zilizosababisha wachukue hatua mbalimbali zilizowaletea uzoefu, hali, watu na kila kitu kilichosaida wao kukamilisha ugunduzi wao.

Njiani walikutana na vikwazo vingi, mfano Edison alipokuwa akigundua balbu ya umeme alifeli mara 9,999 kabla hajaja kufaulu mara ya elfu 10, lakini mara zote alizoanguka katu hakukata tamaa mpaka muujiza ulipotimia. Vivyo hivyo na ndugu wawili waliogundua ndege mwazoni walikumbana na vikwazo vingi kikiwemo cha kukataliwa hatimiliki na serikali ya Marekani ikawabidi wakauze ugunduzi wao Ufaransa. Pia walipata ajali kadhaa wakati wa majaribio ya kuruka kiasi cha kuhatarisha maisha yako kwa kiasi kikubwa.


Kwahiyo mawazo au fikra ndiyo hatua ya mwanzo kabisa ya kufanikiwa katika kila kitu ikiwa mtu ataamini katika kile anachokifanya huku akikifanyia kazi kwa juhudi zote bila kukata tamaa. Mwisho wazo hilo litageuka kuwa kweli. Zawadi kubwa kulio zote Mwenyezi Mungu aliyotupatia wanadamu ni nguvu ya ajabu ya mawazo yetu kwani mawazo ndiyo hutuwezesha kubadilisha maisha kutoka kushindwa mpaka ushindi, kutoka huzuni mpaka kuwa na furaha, kutoka umasikini hadi utajiri kupitia tendo dogo tu la kubadilisha mtazamo wa mawazo yetu.

Tatizo tu ni kwamba watu wengi hawafahamu wala kuamini kwamba nguvu hiyo kubwa wanayo na wanaweza kuidhibiti.

Mwisho.

………………………………………..

Ndugu msomaji wangu mwezi huu tunahitimisha mwaka wa 2018 na kuukaribisha 2019. Ingependeza kama tungelizitumia siku hizi 30 zilizobakia kufanya tathmini ya yale yote tuliyofanya kwa mwaka mzima lakini kwa upande wangu nimefikiri niendelee kutuma makala hizi pamoja na kuweka masomo katika group la wasap nikilenga hasa wale ambao hawakupata fursa ya kujiunga na programu yetu inayoisha ya “MZUNGUKO WA FEDHA NDIYO NJIA BORA ZAIDI YA KUTIMIZA MALENGO YAKO 2018”.

Kwa siku hizo 30 na nimeanza jana tayari kwenye group, tutakuwa tukitoa somo moja lenye maudhui ya pesa kila siku huku nikikukumbusha umuhimu wa kujiunga na programu hiyo kabla ya mwisho wake itakapofika Novemba 30. Nafanya hivyo kuepuka lawama zozote mtu anazoweza kuja kunipa hasa kwa wewe ambaye huwa unafuatilia blogu hii. Kama unapenda makala hizi basi naamini zile ninazotuma wasap zitakuwa nzuri zaidi kwako ndio maana nachukua hatua ya kukuhamasisha kujiunga.

Ni sababu hiyohiyo pia iliyonifanya masomo na semina zote za tangu mwezi Januari mpaka sasa nitengeneze vitabu maalumu 3(PDF) kwa ajili yako. Vilevile kuna michanganuo ya biashara bunifu tuliyoandika hatua kwa hatua na wadau wa group, vitabu na sasa masomo haya makubwa 30 kuhusiana na fedha tutakayokwenda kujifunza kwa muda wa siku 30.

Kwenye Group somo tuliloanza nalo jana katika utaratibu huu wa masomo 30 ya siku 30 lilikuwa linasema hivi; “NJIA 5 ZA KUONDOA WOGA NA STRESS ZA FEDHA KATIKA MAISHA YAKO

Na leo hii tarehe 2 Desemba 2018 tutakuwa na somo jingine linalosema;  AINA ZA BIASHARA UTAKAZOFANYA ILI KUPATA UHURU KAMILI WA KIFEDHA

Ukitaka kujiunga na masomo haya lipia kiingilio ambacho ni sh. Elfu 10 kisha tuma ujumbe wa kawaida au wa wasap usemao; NIUNGANISHE NA GROUP LA MICHANGANUO-ONLINE”. Namba zetu za simu ni 0765553030  au  0712202244 WHATSAP tumia 0765553030 na jina ni Peter Augustino Tarimo.

Kumbuka baada ya Desemba 30, offa ya programu hii itamalizika rasmi na tutaanza nyingine ya mwaka 2019. Masomo yote ya mwaka 2018 pamoja na semina zake hazitakuwepo tena, Pia nafasi katika group zilizobakia ni chache kufikia watu 250 hivyo nakusihi sana msomaji wangu, usikose fursa hii adimu kama wewe ni mpenzi wa masomo haya.

0 Response to "HIVI UNAJUA UNAWEZA KUFANYA MIUJIZA HAPA DUNIANI UKIAMUA?"

Post a Comment