SABABU 4 KWANINI MATANGAZO YA BIASHARA YAKO HAYALETI WATEJA KAMA UNAVYOTAKA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

SABABU 4 KWANINI MATANGAZO YA BIASHARA YAKO HAYALETI WATEJA KAMA UNAVYOTAKA

kileleni

Una kampuni nzuri, unazalisha bidhaa bora kabisa kupita washindani wako, unao mtaji mkubwa wa kutosha lakini unashangaa hupati wateja wengi kama vile ambavyo ungependa iwe. Na hata unapojaribu kufanya matangazo ya biashara katika vyombo vya habari mbalimbali bado huoni matokeo mazuri, hamna wateja wanamiminika kuja kununua.


Matangazo ya biashara au kwa jina jingine promosheni ni moja ya silaha 5 au tuseme nguzo za masoko ambapo soko ndiyo kiini kikubwa cha uhai wa biashara. Silaha nyingine 4 za masoko ni Bidhaa, Bei, Eneo na Watu, kwa kimombo, Product, Price, Place & Peple. Bila soko hamna mtiririko chanya wa pesa kwenye biashara yeyote ile na soko ni lazima litafutwe kwa njia ya matangazo.


Kabla hatujakwenda kuziona sababu zenyewe nne zinazosababisha matangazo ya biashara nyingi kutokuzaa matunda yaliyokusudiwa yaani kuleta wateja wa kutosha, hebu kwanza kwa kifupi tuone matangazo ya biashara ni kitu gani, yanafanya kazi gani na dondoo mbili tatu kuhusiana na matangazo ya biashara.


Kutangaza biashara maana yake ni kile kitendo cha kuvutia hisia za watu kwenye bidhaa ama huduma unayouza katika jamii au umma wa watu kwa lengo la kuifanya bidhaa yenyewe iuzike kwa haraka na kwa wingi zaidi.

Tangazo ni ule ujumbe, unaweza ukawa aidha katika mfumo wa maandishi, sauti, picha au hata video.


KAZI MUHIMU ZA MATANGAZO YA BIASHARA
·       Hutengeneza uhitaji wa kile kitu unachouza.

·       Huwapa wateja taarifa kuwa kuna mahitaji katika maisha yao yanayotakiwa kutimizwa.

·       Hukusudiwa kutoa taarifa na kushawishi tabia na mitizamo ya watu.

Ili ujumbe wa tangazo uweze kufanya kazi vizuri, watu tofauti wanahitaji kusikia au kuona  tangazo hilohilo kila mara na mara nyingi kadiri iwezekanavyo kupitia njia tofauti.

Ni bora tangazo liwafikie idadi ndogo kabisa ya watu lakini ujumbe mzito wa maana ufike, kuliko tangazo kuwafikia mamilioni ya watu pasipo kufikisha ujumbe mzito wa maana.


DONDOO: UKWELI KUHUSU MATANGAZO YA BIASHARA
·       Hakuna tangazo linaloweza kupendwa na kila mtu

·       Tangazo moja pekee kamwe halitaweza kuleta mafanikio kwa asilimia 100%

·       Tangazo hubeba taarifa na ni njia inayoweza kuwashawishi watu kubadili mitazamo yao na tabia.

·       Tangazo la biashara litapoteza umuhimu uliokusudiwa ikiwa litatazamwa au kusikilizwa na watu wasiokuwa walengwa au wenye chuki na bidhaa/huduma inayotangazwa

SASA BASI SABABU HASA NNE (4) KWANINI MATANGAZO YA BIASHARA YAKO HAYALETI WATEJA NI ZIPI?.....

………………………………………….

Mpendwa msomaji wa makala hizi, ungana na mimi leo kwenye kundi la masomo ya kila siku la WHATSAPP la MICHANGANUO-ONLINE. Huko tunakuwa na masomo yahusuyo fedha kila siku pamoja na Semina za mara kwa mara juu ya namna ya kuandika Mpango wa biashara(Michanganuo ya biashara zile zilizo na uwezo mkubwa wa kuzalisha faida)

Ili kujiunga na Group hili kuna kiingilio/ada ya shilimgi elfu 10(10,000) na mara tu mtu anapomaliza kulipa huwa tunamuunganisha papo hapo na Group ikiwa ni pamoja na kumtumia masomo na semina zote zilizopita tangu January, Vitabu na michanganuo kamili mbalimbali. Namba za kulipia ni 0712202244  au  0765553030 jina hutokea Peter Augustino Tarimo. Ukishalipa tuma ujumbe wa “NIUNGANISHE NA GROUP LA MICHANGANUO”

0 Response to "SABABU 4 KWANINI MATANGAZO YA BIASHARA YAKO HAYALETI WATEJA KAMA UNAVYOTAKA"

Post a Comment