Zamani ndiyo ulikuwa ukimsikia mtu akihangaika kulinda
kwa udi na uvumba wazo lake la biashara kusudi mtu mwingine mjanja asije
akaliiba na kwenda kulifanyia kazi na hivyo kumpiku kibiashara, lakini katika
dunia ya leo ambapo utandawazi umebadilisha karibu kila kitu kuanzia biashara
mpaka jinsi tunavyowasiliana, wazo la biashara la kipekee tena siyo ishu kubwa
kivile.
Zilikuwa ni zile enzi za ugunduzi, sasa hivi ni nani tena
anayegundua kitu kipya kabisa kirahisi ambacho hakifanani hata kidogo na vile
vilivyokwisha kugunduliwa kabla? Bila shaka hakuna na hata kama vipo vitakuwa
ni vichache kwa nadra sana.
Wazo la biashara hata hivyo ni muhimu sana na linapaswa
tu kuwa ni wazo la biashara ambayo utakuwa na uwezo wa kuifanyia ubunifu mkubwa
kusudi uweze kuhimili ushindani katika
soko na siyo lazima liwe la kipekee hapana. Katika uchumi wa leo uliojaa
ushindani usiokuwa na hata chembe ya huruma, ikiwa kama hautaweza kufikiria nje
ya boksi na kuja na ubunifu mkubwa
wakati uleule unapokuwa ukilitekeleza wazo lako, ukategemea upekee wa wazo hilo
peke yake, utakuwa umepitwa na wakati.
Hapa siri kubwa inabakia kuwa katika utekelezaji ambao
mara nyingi nimekuwa nikiusisitiza. Unaweza ukakaa na wazo lako bora la
biashara hata miaka 10 lakini kama hakuna utekelezaji(execution), unabakia kuwa
sawa tu na mtu yule asiyekuwa na wazo la biashara lolote lile la maana
kichwani.
Dunia imejaa mifano ya biashara na makampuni mbalimbali
yanayong’ara duniani kote sasa hivi kutokana na kutumia ubunifu katika mawazo
yaliyoasisiwa na watu au makampuni mengine tofauti kabisa huku waanzilishi
wenyewe wa mawazo hayo wengine wakiwa hata hawajulikani kama ni wao
walioanzisha.
Kampuni ya Microsoft kwa mfano imepata umaarufu mkubwa
kote duniani kwa mifumo yake ya uendeshaji kompyuta(Operating Systems) lakini
Bill Gates hakuwa ni mtu wa kwanza kuigundua mifumo hiyo, naye aliiga kutoka
watu/makampuni mengine na kuiboresha huku waanzilishi wake kwa kukosa ubunifu
wakatoweka kwenye ushindani na kumwacha Gates ‘akipeta’
Hapa kwetu Tanzania pia tuna mifano mingi na mmoja wapo
ni Kampuni ya uchapishaji ya Global Publishers chini ya mwasisi wake Bwana Eric
James Shigongo, Shigongo hakuwa mtu wa kwanza kuanzisha biashara ya magazeti ya
udaku hapa Tanzania. Hapo kabla tokea miaka ya 70 palikuwepo na magazeti ya
udaku kama vile SANI, HEKO, KASHESHE, SANIFU, KOMESHA nk. lakini Eric Shigongo alikuja na ubunifu wake
wa kipekee wa kutunga hadithi tamu akafanya mapinduzi makubwa katika tasnia
nzima ya magazeti hayo pendwa nchini na kupata mafanikio makubwa.
Halikadhalika kampuni kubwa la Google, Google haikuwa
Search Engine ya kwanza mtandaoni, hapo kabla kulikuwepo na akina, Webcrawler,
Yahoo, Excite nk. lakini leo hii kutokana na ubunifu, Google kwa kutumia mawazo
yaleyale ya kwao anakaribia kuwapoteza kabisa kwenye ulimwengu wa search
engines.
Orodha ni ndefu, tukitaja makampuni yote hapatatosha hapa
lakini yote kwa yote ni kwamba kama unahangaika kupata wazo zuri la biashara
itakayokutoa, kitu kikubwa cha kufanya wewe wala usiwaze sana fanya hivi;…………
……………………………………................
Ndugu
msomaji wangu, somo hili hapa ni kipande tu, somo zima tutasoma leo katika
Group la Whatsap la MICHANGANUO ONLINE. Masomo kama haya na yale yahusuyo jinsi
ya kuandika mchanganuo wa biashara huwa tunajifunza kila siku.
Na
hata ikiwa hutapata nafasi ya kushiriki leo, hujachelewa sana kwani masomo ya
tangu January mpaka mwisho wa mwaka wetu unaoishia mwezi February mwakani
tunayatunza kwa ajili ya mwanachama yeyote anayejiunga kabla ya muda huo
kumalizika. Baada ya muda huo ukijiunga huwezi tena kupewa mfululizo wa masomo
hayo.
Kiingilio
ni sh. Elfu 10 tu na unalipa kupitia namba 0712202244 au 0765553030 jina
hutokea Peter Augustino Tarimo. Ukishalipia tuma anuani yako ya email kwa
meseji pamoja na ujumbe huu; NIUNGANISHE NA GROUP LA MICHANGANUO au unaweza
kuwasiliana nasi kwa wasap 0765553030 kwa maelezo zaidi. Ikiwa hutumii wasap
email inatosha tutakutumia masomo na
semina kama kawaida. Unapewa pia na kitabu cha Michanganuo ya biashara
na ujasiriamali bure.
KARIBU!
KARIBU!
0 Response to "KWANINI WAZO LA BIASHARA INAYOWEZA KUKULETEA FAIDA KUBWA SIYO TATIZO?"
Post a Comment