SIRI ZA PESA: NI MBINU YA KIZAMANI SANA YA KUTUNZA PESA LAKINI WATAALAMU WANASEMA NI NZURI KUSHINDA ZILE ZA KISASA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

SIRI ZA PESA: NI MBINU YA KIZAMANI SANA YA KUTUNZA PESA LAKINI WATAALAMU WANASEMA NI NZURI KUSHINDA ZILE ZA KISASA

Old school-zamani

Siri ya kufanikiwa kimaisha ni vitu vidogovidogo sana kama ulikuwa hujui, mathalani utunzaji mzuri wa pesa zako, jinsi ya kuwekeza vizuri pesa zako zizae, jinsi ya kuweka na kutunza akiba yako nk. 

Na wala usije ukafikiri eti suala kama la la utunzaji mzuri wa fedha ama kuwa na nidhamu ya pesa limeanza juzijuzi tu hapana, tokea enzi na enzi mababu na mabibi zetu walikuwa na njia zao bora kabisa za wakati huo walizokuwa wakizitumia na walijifunza jinsi ya kuishi kwa bajeti maishani katika kuhakikisha mambo yao kiuchumi yanakwenda barabara na hawaingii katika mikwamo ya kuishiwa fedha ovyo ovyo. Walikuwa pia na mbinu zao za kujifunza jinsi ya kuwa tajiri.

SOMA: Elimu ya fedha na umuhimu wake, njoo tuunganishe nguvu tuhamishe milima!

Licha ya siku hizi teknolojia kwenye nyanja ya fedha kuwa imekua sana, tukishuhudia  kwa mfano mpaka ujio wa ma ‘apps’ yenye uwezo wa kumfundisha mtu jinsi ya kuishi kwa bajeti kulingana na kipato cha biashara au hata jinsi ya kupangilia mshahara utokanao na kazi/ajira yako. 
Kuna apps nyingine pia zinazomwezesha mtu kufanya manunuzi mtandaoni (online) kwa urahisi, lakini bado njia hii ya kizamani sana (OLD SCHOOL…Technick) imethibitishwa na wataalamu wengi wa uchumi kote duniani kuwa inao uwezo wa kumfanya mtu atengeneze nidhamu ya hali ya juu ya pesa na ni bora zaidi kushinda hata zile za kisasa, na isitoshe ni ya kutegemewa.

Usidhani kwamba siri ya kufanikiwa kibiashara ni lazima tu mtu utumie teknolojia za kisasa kama applications za kwenye simu janja au mifumo ya kiuhasibu iliyobobea hapana, kwani unafikiri waliokuwa mabilionea miaka hiyo ya arobaini na saba walitumia compyuta na simu janja kutunza fedha zao?

SOMA: The sky is very wide, every star can shine( Mbingu ni kubwa mno, kila nyota inaweza kung'ara)

Njia hii ya kitambo unayoweza pia ukaiita mfumo ama siri ya kutunza pesa siyo ngumu kutumia hata kidogo mpenzi msomaji wangu na hata wewe mwenyewe unaweza leo ukaamua kwenda kuijaribu, ni rahisi sana na itakayokwenda kuufanya mzunguko wako wa fedha kuwa chanya muda wote na hivyo pia kukufanya wewe mwenyewe kutabasamu muda wote kwani ni sheria ya asili kwamba,

MZUNGUKO CHANYA WA FEDHA = FURAHA (POSITIVE CASH FLOW = HAPPINESS)

Njia hii ni nzuri sana hasa kwa watu wa vipato vya kawaida na wasioweza kuilinda vyema mizunguko yao ya fedha au kwa wale wanaosumbuliwa na madeni ya mara kwa mara. Huweza kukomesha kabisa matumizi ya hovyo kwenye vitu kama chakula na starehe kwa kifupi hufundisha jinsi ya kutunza akiba ama hata ukipenda jinsi ya kuwa tajiri haraka

SOMA:  Niweke akiba kiasi gani cha mapato yasiku katika faida ya duka la mahitaji ya nyumbani?

Watu wengi huwa hawaoni kabisa umuhimu wa kupanga kabla matumizi ya vitu kama umeme na maji lakini kwa kweli kufahamu utatumia kiasi gani cha umeme au maji kabla hata ya mwezi wenyewe haujaanza ni jambo la msingi sana na litakalokujengea nidhamu nzuri ya matumizi yako ya pesa kwa vitu hivyo.

Kwa njia hii utaweza kufahamu kwa uhakika zaidi ni wapi fedha zako zinakokwenda lakini pia ni wapi zinakotokea. Siri kubwa ya kufanikiwa kwenye suala la pesa iwe ni biashara au matuumizi yako binafsi ni kuwa na mfumo thabiti unaohakikisha unafahamu bayana kile unachoingiza na kile unachotoa.

SOMA: Kwanini mikopo ya riba mitaani, michezo ya upatu na baadhi ya vocoba si salama kujiunga?

Si mganga, si mchawi wala wataalamu wa mambo ya pesa watakaokufundisha wewe jinsi ya kutajirika kwa haraka ikiwa utashindwa zoezi hili muhimu la kuzitunza pesa zako vizuri. Mfumo huu wa kizamani uliovuma sana miaka ya 50, 60, 70, na 80 ni kama vile ilivyokuwa dhahabu, hauchuji wala haupitwi na wakati na unatumiwa bado na watu mpaka huko Marekani, Uchina na hata Bara la Ulaya.

......................................................

Mpenzi msomji wangu, somo hili au mbinu hii ya utunzaji pesa tutakwenda kujifunza kikamilifu leo tarehe 14/07/2023 katika Group la Masomo ya kila siku WHATSAPP la MICHANGANUO ONLINE. Ili kujiunga katika group hili mwanachama anapaswa kulipa kiingilio cha shilingi elfu 10 tu kwa mwaka mzima

Unapata papo hapo vitu mbalimbali vikiwemo vitabu, masomo yaliyopita na michanganuo mbalimbali ya biashara zinazolipa. Jumla ni items 12. Package ama kifurushi hiki kitakuwezesha kujifunza ujasiriamali na biashara kwa kina na ikiwa kama ulikua hujui ni nini maana ya Business plan (Mpango wa biashara) basi hapa ndiyo mahala pake.

Si hivyo tu unapata pia fursa ya kujiunga na group letu la masomo ya fedha kila siku, kumbuka hili ndiyo group pekee Tanzania unaloweza kupata somo jipya lenye maudhui ya fedha kila siku. Siyo dondoo, narudia tena, ni masomo kamili ya fedha usiyoweza kuyapata mahali pengine popote nje na ndani ya mtandao.

Malipo ni kupitia namba; 0712202244 au 0765553030 jina Peter Augustino Tarimo. Ukishatuma, tuma pia ujumbe usemao,  "NIUNGE NA GROUP LA MICHANGANUO NA OFFA YA VITU 12" au wasiliana na sisi moja kwa moja kupitia hizo namba.

0 Response to "SIRI ZA PESA: NI MBINU YA KIZAMANI SANA YA KUTUNZA PESA LAKINI WATAALAMU WANASEMA NI NZURI KUSHINDA ZILE ZA KISASA"

Post a Comment