HUDUMA BORA KWA WATEJA KWELI HII, CUSTOMER CARE AU CUSTOMER KERO? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

HUDUMA BORA KWA WATEJA KWELI HII, CUSTOMER CARE AU CUSTOMER KERO?

CUSTOMER CARE AU CUSTOMRE KERO?
Biashara ndogondogo nyingi huku mitaani huendeshwa kwa mazoea kiasi kwamba kuna wakati mteja unalazimika kujiuliza ikiwa mjasiriamali huyu mdogo anafahamu kweli jinsi ya kutoa huduma bora kwa mteja(good customer care) au anachotoa yeye ni customer kero kwa mteja.


Kama kawaida yangu ninapopita mitaani nikiwa kwenye shughuli zangu za kawaida siachi pia kuchunguza mienendo ya biashara nyingi ndogondogo kwa faida ya wasomaji wangu katika blogu hii ya JIFUNZEUJASIRIAMALI, na safari hii nilikuwa maeneo fulani ya Mbezi mwisho baada ya kushuka kwenye mwendokasi nikawa nawaza nikanunue kapaja ka kuku mahali fulani walipoweka kibanda cha kukaangia nyama za kuku, mapaja, vidari, firigisi, shingo za kuku, na hata miguu na vichwa vya kuku.


Nilikuta hamna paja nikaamua kumwambia mchoma kuku yule anipe tu kidari cha kuku lakini anikaushie vizuri, atie chumvi, pilipili na mazagazaga yote yaliyokuwepo pale nibebe nikalie nyumbani. Lakini kwa mshangao yule muuzaji nyama za kuku alinijibu “Aisee nyama zimeshakaushwa tayari, unachukua tu hamna haja tena ya kutia kwenye mafuta ya moto” Nilipozitazama zile nyama, naona kabisa zimepoa na pengine huenda hata hazikuwa zimewiva sawasawa.

Tulibishana kidogo huku akionekana mtu mwenye haraka sana manake ilikuwa jioni na alikuwa akikazani kuandaa nyama mbichi ambazo hazikuwa zimetiwa kwenye mafuta ya moto bado. Baada ya kumlazimisha, akaiweka ile nyama kwenye mafuta kwa shingo upande huku akinung’unikanung’unika. Ile kufumba na kufumbua tu alikitoa kile kidari kwenye mafuta na kudai tayari kimewiva akaanza kukifungia harakaharaka, na mimi sikuona tena sababu ya kuendelea kubishana naye, akaweka kila kitu nikaondoka zangu.


Kufika nyumbani, nyama ikawekwa mezani, nyama kwa juu ina moto kidogo lakini ndani nyama ilikuwa baridi utadhani imetoka kwenye friji muda uleule. Nikagundua pia kwamba nyama zile wala hazikuwa za siku ileile bali zilikuwa za jana yake na yule muuzaji alichofanya ni kuzitoa kwenye friji na kuziweka pale mezani. Sasa nikajiuliza alivyokuwa akiniambia zimeshakuwa tayari alikuwa akimaanisha nikifika nyumbani nikaitie tena kwenye mafuta ya moto? au  basi yeye lengo lake ni kuuza tu nyama, mteja utajijua mwenyewe mbele ya safari?

Lakini niliendelea kujiuliza maswali ikiwa muuzaji yule kweli yupo ‘serious’ na biashara anayofanya kwani kwa mfano mimi binafsi sidhani kama itatokea tena siku nyingine nikanyage pale kwake kununua nyama ya kuku. Alinifanya hata nianze kutilia mashaka wauzaji wengine wote wa nyama za kuku wanaoweka vibanda na meza zao maeneo ya stendi au kandokando ya barabara. Kwa kweli ni kama aliniharibia jioni yangu ile yote niliyopanga kwenda kutafuna kidari cha kuku kilichotiwa pilipili na limao.

MUUZA KUKU WA KUCHOMA
Kijana akichoma kuku barabarani tayari kwa kuuza kwa wateja.
Mfanyabiashara katika kutoa huduma nzuri kwa wateja wako hakikisha kwanza unafahamu kwa uhakika mteja ni nani na maana ya huduma bora kwa mteja ni nini. Mteja unatakiwa umchukulie kama mtoto mdogo anayejifunza, hupaswi kujifanya wewe unajua zaidi yake hata ikiwa unaona kabisa yeye anachosema ni pumba, wewe jifanye mjinga huku ukifahamu unachohitaji kutoka kwake ni kitu gani. Kwa mteja wewe hauhitaji kingine zaidi ya pesa yake na yeye hahitaji kitu kingine zaidi ya huduma nzuri itakayotatua shida yake iliyomleta pale kwako, kwa hiyo jitahidi sana kuhakikisha unafahamu kikamilifu ni kitu gani au shida gani iliyomleta mteja kwako na uhakikishe pia unampa huduma kupita matarajio yake.


Kama yeye alijua atapata paja la kuku kwako likiwa la moto basi na wewe muongezee hapo vikorombwezo vingine kibao, mfungie kwa foil safi, mwekee kalimao kidogo, kachumbari kama anapenda, pilipili, viungo vya kunukia na hata mayonnaise kama ipo, vitu ambavyo wala hakufikiria kabisa kuvipata kutoka kwako.

Na vikorombwezo vingine hivyo wala hata havina gharama kubwa sana, lakini hapo unakuwa umeshajihakikishia mteja wa kudumu, maana yake mteja huyo atakuwa akijisemea, “kesho itafika lini nikikitoka kazini nipite tena pale kwa yule Mpemba nikajichukulie hapo firigisi na kidari”  ‘Umeshamloga’ tayari badala ya wewe kwenda kuhangaika kwa Masangoma matapeli watakaofilisi mpaka na kamtaji kenyewe ulikokapata kwa shida.

………………………………………………………………………..
Mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa makala hizi juu ya biashara ndogondogo zinazolipa, usikose kila siku kujifunza kitu kipya ndani ya blogu yako hii na pia ikiwa utataka kujifunza mambo mengine makubwa na mengi zaidi, basi usiache kujipatia vitabu vyako bora kutoka SELF HELP BOOKS TANZANIA chini ya SMART BOOKS TZ. 

Vitabu hivi kuna vya bure na vya malipo pia unaweza kuvipata katika mifumo yote ya SOFTCOPY kwa njia ya email au HARDCOPY ofisini kwetu au kuletewa ulipo. 

Namba zetu za simu ni;
0712202244  au  0765553030

Jina linalotokea ni;

Peter Augustino Tarimo

Tupo Mbezi Kwa Msuguri jirani na Stendi au Bochi Hospital
SOFTCOPY SH. 10,000/=
HARDCOPY SH. 20,000/=


SOFTCOPY SH.     5,000/=
HARDCOPY SH.   10,000/=


SOFTCOPY SH. 3,000/=
HARDCOPY SH. 5,000/=


0 Response to "HUDUMA BORA KWA WATEJA KWELI HII, CUSTOMER CARE AU CUSTOMER KERO?"

Post a Comment