VITABU VYA MAFANIKIO 300 VILIVYOSOMWA ZAIDI DUNIANI NAKALA MAELFU KWA MAELFU | JIFUNZE UJASIRIAMALI

VITABU VYA MAFANIKIO 300 VILIVYOSOMWA ZAIDI DUNIANI NAKALA MAELFU KWA MAELFU

Vitabu 300 vya mafanikio vilivyosomwa zaidi duniani
Hivi ni vitabu vya pesa na mafanikio vya wakati wote(SELF DEVELOPMENT BOOKS OF ALL TIMES), Hii ni safu mpya ambayo inaanza hapa katika blogu yako ya jifunzeujasiriamali, na safu hii itakuwa kila siku tukiangazia kwa ufupi vitabu mashuhuri zaidi duniani vinavyohusiana na maendeleo binafsi ya mtu, vitabu ambavyo vilitamba, bado vinatamba na vitaendelea kutamba kwa miaka mingi ijayo. Tutazungumzia pia waandishi wake, wasifu wao na nakala walizowahi kuuza mpaka sasa.

Kumbuka ndugu msomaji, duniani kumejaa vitabu mamilioni kwa mamilioni lakini vile vinavyofanikiwa kuwa maarufu au kuuza nakala nyingi ni vichache, hata hivyo uchache wake hatuwezi tukasema labda ni vitabu mia au elfu kadhaa tu hapana, navyo ni maelfu kwa maelfu.

Hata useme leo unaamua kila kitabu utakisoma basi itabidi labda uishi miaka elfu moja. Lakini kama kitabu cha KANUNI YA KUJIFUNZA ELIMUYA PESA NA MAFANIKIO kinavyopendekeza, unaweza ukachagua baadhi ya vitabu utakavyovisoma na ukapata maarifa makubwa kwa kile unachokihitaji katika muda fulani tu huku masuala mengine ya kimaisha nayo yakipata muda wa kuyafanya.

“Countdown” hii nitakayokwenda kukuletea hapa, siyo kama ni sheria kwamba mtu ni lazima avisome hapana, ni pendekezo linalotokana na utafiti uliofanyika juu ya umashuhuri wa vitabu hivyo

Bila ya kupoteza muda mwingi leo hii tutaanza moja kwa moja na kitabu namba moja cha elimu ya pesa na mafanikio kutoka katika listi yangu ambacho siyo kingine bali ni kitabu cha Mwandishi Napoleon Hill, Think and Grow Rich(Fikiri Utajirike) au kwa jina jingine MSAHAFU WA MAFANIKIO kama kilivyopewa jina hilo kwa mara ya kwanza kabisa na Blogu hii.

Napoleon Hill anajulikana kuwa ndiye mwandishi rasmi wa kwanza kabisa kuandika vitabu vya maendeleo binafsi ya watu. Vitabu vyake kama vilivyopata kuwa muhimu miaka takribani 80 iliyopita, ndivyo hivyohivyo na leo vilivyokuwa muhimu. Kamwe havijapitwa na wakati.

Fikiri Utajirike(Think and Grow Rich)
Fikiri utajirike
Kitabu chake, THINK AND GROW RICH ni mkusanyiko au ufupisho wa kitabu kingine kiitwacho, Sheria za Mafanikio(Laws of Success) Mkusanyiko huo ukazaa kanuni 13 za mafanikio binafsi ya mtu na maudhui yake makubwa ni kwamba, mtu yeyote mwenye Shauku ya jambo/kitu, akiwa na Imani na Uvumilivu vikiambatana na kuondoa aina zote za mawazo hasi akilini, huku akiwa na Malengo makubwa, mtu huyo hakuna kitu chochote kile kitakachoweza kumzuia kufikia MAFANIKIO MAKUBWA KABISA MAISHANI MWAKE.

Kitabu hiki kwakweli nasema katika Blogu hii ndipo mahali pake kwani tangu imeanza, tumekuwa tukikitafsiri kitabu hicho katika lugha ya kiswahili, kitabu kizima kama kilivyo pamoja na Ufupisho wake au uchambuzi  kwa kifupi. Kusoma tafsiri hiyo na ufupisho wake fungua maandishi yafuatayo, FIKIRI UTAJIRIKE(Think & Grow Rich)

Usikose mfululizo wa orodha ya vitabu hivi 300 nilivyokuandalia kila siku. Asante.

..............................................................................................

Ile SEMINA ya Michanganuo ya Biashara bado inaendelea, soma Masomo yatakayofundishwa hapa, RATIBA YA MASOMO YA SEMINA YA MPANGO WA BIASHARA

Kwa vitabu vyako bora kabisa vya biashara na ujasiriamali katika lugha ya kiswahili, ingia kwenye ukurasa wa SMARTBOOKSTZ






1 Response to "VITABU VYA MAFANIKIO 300 VILIVYOSOMWA ZAIDI DUNIANI NAKALA MAELFU KWA MAELFU"