UTOKE VIPI KIMAISHA? RUGE ANAKUPA FURSA MUHIMU 10 HIZI HAPA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

UTOKE VIPI KIMAISHA? RUGE ANAKUPA FURSA MUHIMU 10 HIZI HAPA

Wiki iliyopita, Mkurugenzi wa vipindi wa kampuni ya Clouds Media inayomiliki vituo cha redio na Televisheni vya Clouds fm na Clouds Tv, Bwana Ruge Mutahaba alitangaza kuzitaja fursa kumi (10) za kibiashara na kiuchumi zinazopatikana hapa Tanzania. Alizitaja fursa hizo 10 ndani ya kipindi maarufu cha Power Breakfast na pia kupitia TV, Kwenye kipindi cha Clouds360.

Akizitaja fursa hizo muhimu za kibiashara alisema kwamba, mtu anachopaswa kufanya kwanza ni kuzisikiliza fursa kumi, na pili ni sharti ajitambue yeye binafsi. Akitolea mfano, alimtaja Nyota Ndogo, msanii wa muziki wa kizazi kipya kwamba kama asingelitambua kipaji chake kwanza kuwa yeye ni mwanamuziki, kamwe asingeliweza kufikia hatua aliyofikia sasa.

Aliongeza kuwa wengi tunashindwa kujitambua, kushindwa kufahamu nguvu tulizokuwa nazo, “Ninaamini kila mtu anacho kipaji(talanta) ambayo amezaliwa nayo”. Alisema Ruge Mutahaba, “Mwingine anaweza kuwa mchoraji mzuri lakini hajawahi kufikiria kuwa ni ‘designer’ mzuri kwani hakuna mtu aliyemsaidia kumuonyesha anafanyaje vitu, hivi vitu ni kujaribu, kujifunza, kujitathmini na kujifahamu” aliongeza Ruge Mutahaba.

Akitolea mfano mwingine wa madalali, Ruge aliuliza kuwa ni madalali wangapi wanaotumia mtandao wa ‘Instagram’ katika biashara zao, zaidi tu ya kuwa na ‘contact’ za kawaida za simu?.

Mwisho alianza sasa kuzitaja fursa zenyewe 10 nazo ni kama ifuatavyo:-

1. FURSA KATIKA SEKTA YA KILIMO.
Alisema kuwa kilimo ndio msingi wa shughuli nyingine zote lakini Watanzania hulima si kwa lengo la kufanya kilimo cha kibiashara, bali kujikimu na njaa. Hivyo alisema hali hiyo inatoa mwanya kwa mtu yeyote anayependa kufanya kilimo cha kibiashara kuwa na fursa kubwa ya kutoka kiuchumi. Aidha alisema kilimohuchochea viwanda na mwishowe ongezeko la ajira katika nchi.

2. BIASHARA YA CHAKULA (FOOD PROCESSING)
Ruge Mutahaba fursa hii katika tasnia ya chakula anaitazama kwa jicho la kuongeza thamani “value added”, matangazo na ubunifu. Alihimiza watu wasiishie tu kupika kwa mazoea bali pia waongeze ubunifu kwa kwa kuibuka na vitu(njia) mpya tofauti tofauti kusudi waweze kuongeza tija zaidi.

3. BIASHARAYA REJAREJA MITANDAONI “RETAIL E-COMMERCE”
Alisema biashara hii mtu anaweza kuifanya, aidha anaponunua ama kuuza bidhaa/huduma kupitia mtandao wa intaneti, “Huna haja ya kuonana na wateja ana kwa ana, na unaweza ukauza bidhaa za kila aina kuanzia, nguo, viatu nk.

4.  SEKTA YA HABARI NA BURUDANI.
“Tukiweza kutengeneza filamu nzuri   tunaweza kufika mbali” Alitolea mfano wa Wanaigeria ambao alisema waliweza kutengeneza filamu moja nchini Marekani na ikaweza kufikisha mauzo ya nakala laki tano(500,000) katika kipindi cha mwezi mmoja pekee.

5.  BIASHARA KATIKA TASNIA YA HUDUMA ZA KIJAMII.
Alitoa mifano ya Mahospitali na mashule mengi ya watu binafsi, jinsi zinavyofanya vyema na kusema, hiyo ni fursa nzuri ya watu wengi zaidi kuanza kuwekeza huko.
 
6. SEKTA ZA MITINDO NA UREMBO.
Alisema hapo zamani ili mtu aonekane kuwa ni mrembo na mwenye mvuto alihitaji kuzaliwa nao lakini kwa sasa hivi, urembo wa mtu ni “featuring” ya mambo mbalimbalikuanzia, nywele, kucha mek up nk. Kuna fursa nyingi, mfano mmoja tu, kufanya ‘Pedicure na Manicure’ ni shilingi elfu arobaini (40,000) na hicho ni kitu kimoja tu katika urembo” alisisitiza Ruge Mutahaba.

SEKTA YA VIWANJA, MASHAMBA NA MAJENGO “REAL ESTATE”
Alitaja pia ongezeko la mashule na vyuo kama fursa ya Watanzania kuwekeza katika ujenzi wa hosteli na majengo yatakayotoa huduma  kwa wanafunzi, biashara ambayo ni ya kudumu.

8. TASNIA YA USAFIRISHAJI NA USAMBAZAJI.
Fursa nyingine aliyotaja kuwa ni miongoni mwa fursa za kibiashara na uchumi zinazokuwa kwa kasi na ambazo Watanzania wanaweza kunufaika nazo ni hii ya usafirishaji wa abiria, mizigo na usambazaji wa bidhaa na huduma za aina mbalimbali.

Akitoa mfano wa ununuzi na uuzaji wa Hisa, alisema kwa sasa masuala ya hisa, uelewa umekuwa ni mkubwa miongoni mwa Watanzania na ni fursa nzuri sasa kwa vijana kuwekeza katika hilo.

Alisema karibia kila jambo siku hizi huhusisha matumizi ya mtandao wa intaneti kama kufanya biashara  na hivyo alisema ni fursa nzuri kwetu kuanza kuwekeza na kujiajiri.

0 Response to "UTOKE VIPI KIMAISHA? RUGE ANAKUPA FURSA MUHIMU 10 HIZI HAPA"

Post a Comment