Wakati akifunga mashindano ya kuimba na kucheza muziki yanayoendeshwa na Redio ya Taifa TBC jana tarehe 11 April 2015, Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo Dr. Fenella Mukangara alisema kwamba inafaa shindano hilo linaloendeshwa kwa muda wa kipindi cha miezi mitatu, likahusisha pia na mafunzo ya Ujasiriamali wa masuala ya sanaa kwa washiriki kusudi wanapotoka pale, washindi waweze kupata ajira katika mahoteli mbalimbali pamoja na kuanzisha vikundi vitakavyokuwa rahisi kupata misaada mbalimbali kwa wale ambao hawatakuwa wakipata ushindi.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo Dr. Fenella Mukangara |
Aidha Waziri
Mukangara aliaasa vijana tunapoelekea kipindi cha uchaguzi mkuu, kutaibuka
migomo na migogoro ya kila aina, hivyo wajiepushe kabisa nayo kwani
maendeleo hayawezi kuja pakiwa na migogoro na migomo isiyokuwa ya lazima.
Aliwaasa pia kujiandikisha muda utakapowadia ili kupiga kura kwa wagombea
wanaowataka na pia kuhakikisha wanaichagua katiba iliyopendekezwa kwani ni
halisi.
Shindano hilo linalosimamiwa na Manju wa muziki,
mtangazaji maarufu Masoud Masoud, lilimalizika huku washindi wa kwanza katika
vipengele vya Uimbaji na uchezaji wakijipatia vitita vya shilingi milioni tano
kila mmoja na washindi wa pili shilingi milioni mojamoja. Kwenye kipengele cha
uimbaji washindi walikuwa ni; Hassana
Chibwana kwa upande wa Taarabu, Mshana Mohamed-Dansi, na Mohamed Kupela katika
upande wa Bongo fleva, hawa kwa kuwa fani zao zilikuwa tofauti walishea zawadi
kwa kupata shilingi milioni mbilimbili kila mmoja.
Katika upande wa uchezaji, Elizabeth Matapa mshiriki
pekee wa kike aliyeonyesha maajabu, alijinyakulia kitita hicho cha sh. Millioni
5, baada ya kutangazwa mshindi wa miondoko ya Salsa, iliyokuwa maarufu sana
huko visiwa vya Carrebean, (Cuba na Colombia). Twist alijinyakulia Mzee Joseph
Chengula huku Pop ikimuangukia kijana Exavery Anton aliyengara jukwaani
utafikiri ni Michael Jackson alikuwa amerudi. Kwa upande wa Rhumba aliyeonyesha
umahiri na hatimaye kujinyakulia zawadi ya kwanza ni kijana machachari, Ayubu
Hans.
Baada ya jaji mkuu ( Chief Justice) wa mashindano hayo mwimbaji mkongwe wa Reggae
nchini Innocent Nganyagwa kumaliza kazi ya kuwatangaza washindi, ndipo, Mc wa
shughuli Masoud Masoud alipowakaribisha tena jukwaani Bendi ya Le Grand Utalii kutumbuza na ukawa ndiyo
mwisho wa Shindano hilo lililokuwa na msisimko wa aina yake.
0 Response to "DR. FENELLA MUKANGARA: CLUB RAHA LEO SHOW IJUMUISHE MASOMO YA UJASIRIAMALI WA SANAA"
Post a Comment