Kila
mtu alifikiri kuwa Uholanzi ingelifungwa mabao mengi zaidi katika kipindi cha
pili lakini matokeo yake yaligeuka kuwa kinyume kabisa kwani hata kabla ya
kipindi hicho cha kwanza kumalizika Waholanzi walisawazisha mnamo dk. Ya 44,
bao lililowekwa kimiani kwa kichwa safi kabisa na Nahodha wa timu hiyo, ‘Robin
Van Persie’ huku golikipa wa ‘spain’ akibaki akitazama tu.
Ni
kama vile Waholanzi walikuwa wakiwasoma miamba hao wa kombe lililopita la Dunia
Bondeni A.Kusini kwani ilipofika kipindi cha pili tu, dakika za mwazoni, ‘Arjen
Robben’ akaifungia timu yake goli la pili. Hii ni moja kati ya mechi nzuri
kabisa mashabiki wameishuhudia katika kombe hili la Dunia la mwaka 2014 na
pengine itabakia kuwa historia kutokana na jinsi watu wengi walivyokuwa
wakitabiri bingwa mtetezi Uhispania kufanya vizuri.
Kadiri
muda ulivyokuwa ukienda Wahispania walizidi kuchanganyikiwa hasa kipa wao,
jambo lililosababisha walambwe tena bao jingine dakika ya 64, bao hilo
lilifungwa na ‘Stefan de Virji.’ Bao la nne lilipachikwa wavuni na ‘Robin Van
Persie’ kwa mara ya pili sasa na kufanya matokeo yasomeke 4-1. Kama vile Robin
Van Persie na mwenzake Arjen Robben
walikuwa wamepanga kupachika mabao mawilimawili katika mechi hii, ‘Arjen’ naye
katika dakika ya 80 karibu na mchezo kumalizika aliifungia timu yake ya
Uholanzi bao la tano na ambalo ndilo lililokuwa la mwisho katika mechi hii.
Bao
la pekee walilopata Uhispania lilikuwa ni lile lililofungwa kwa mkwaju wa penalty
iliyopigwa na ‘Xabi Alonso’ mnamo dakika ya 27 katika kipindi cha kwanza, baada
ya mchezaji wao Diego Costa kuangushwa chini.
0 Response to "MECHI KALI YA KIHISTORIA: UHOLANZI VS SPAIN, MASHABIKI WASHANGAA"
Post a Comment