Mexico
wanajipatia bao dakika ya 61 Oribe alipiga mpira kipa wa Cameroon alipourudisha
ukapigwa tena na bao likajaa wavuni. Sasa Cameroon wanakuwa na kibarua kikubwa
kuona ni jinsi gani watakavyorudisha goli hili. Eso Okoto anaangushwa chini na
mpira unapigwa kuelekea lango la Mexico, anagaagaa chini lakini refarii wala
hajali kitu, mpira unaendelea. Cameroon kama ilivyokuwa kwa timu nyingi za kiafrika wamekuja kwenye haya mashindano wakiwa na "mzigo mzito mgongoni" mizigo ya migogoro ndani ya timu na club zao nyumbani. Pengine hata ndiyo sababu ya kutokufanya vizuri kila mara.
Mpaka kipenga cha mwisho kinapulizwa, mechi hii ya pili kundi A timu ya Cameroon inatoka kichwa chini huku Mexico ikitoka kifua mbele kwa bao 3 kwa 0.
Mpaka kipenga cha mwisho kinapulizwa, mechi hii ya pili kundi A timu ya Cameroon inatoka kichwa chini huku Mexico ikitoka kifua mbele kwa bao 3 kwa 0.
0 Response to "SOKA LAIVU BRAZILI LEO: MPAKA HALF TIME BRAZILI NA MEXICO BADO NGOMA DROO"
Post a Comment