CHANJO YA UKIMWI YAMALIZA KABISA VIRUSI NDANI YA SOKWE | JIFUNZE UJASIRIAMALI

CHANJO YA UKIMWI YAMALIZA KABISA VIRUSI NDANI YA SOKWE

Kufanyiwa majaribio kwa binadamu hivi karibuni

Virus wa Ukimwi
Chanjo kwa Nyani inayofanana naya Ukimwi kwa binadamu imeonyesha kutokomeza kabisa virusi, utafiti umeonyesha. Utafiti uliochapishwa katika Jarida la ‘Journal Nature’  umeonyesha kwamba Nyani waliochanjwa wanaweza wakamaliza kabisa virusi wanaodhoofisha kinga ya mwili wajulikanao kama SIV Mac 239 kutoka miili yao.


Ilifanya kazi vizuri kwa Manyani 9 kati ya 16 waliochanjwa . Wanasayansi wa Kimarekani wamesema kwamba wanataka kutumia njia kama hiyo kufanya majaribio ya chanjo ya HIV kwa Binadamu. Profesa Lous Picker kutoka Chuo kikuu cha Tiba cha Oregon amesema; “Ni vigumu kudai virusi vimetokomea kabisa , inawezekana kuna seli ambazo labda hazikuchunguzwa vizuri zilizobaki na virusi, lakini kwa sehemu kubwa kulikuwa hamna kirusi kilichosalia katika miili ya nyani hao”
 
Nyani

Virusi hao aina ya SIV Mac 239 ni hatari mara 100 kuliko vile vya HIV. Nyani aliyeathirika hufa ndani ya miaka 2.

0 Response to "CHANJO YA UKIMWI YAMALIZA KABISA VIRUSI NDANI YA SOKWE"

Post a Comment