“Vijana wanaosubiri mifumo iliyowekwa iwasaidie kujikwamua kiuchumi wataendelea kubaki kuwa watumwa wa maamuzi ya watu wengine.” -Dr. Mengi. | JIFUNZE UJASIRIAMALI

“Vijana wanaosubiri mifumo iliyowekwa iwasaidie kujikwamua kiuchumi wataendelea kubaki kuwa watumwa wa maamuzi ya watu wengine.” -Dr. Mengi.

DAR ES SALAAM, Tanzania

Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk. Reginald Mengi (kulia), ambaye ni muasisi wa shindano la ku-Tweet kuhusu njia mbalimbali za kupambana na umaskini kupitia akaunti yake ya @regmengi, akiwa katika picha ya pamoja jana na washindi wa Julai wa shindano hilo, Tony Alfred (wa pili kulia) aliyeshika nafasi ya kwanza na kujipatia Shilingi milioni moja, John Mkungu (wa tatu kulia), aliyeshika nafasi ya pili na kujipatia Sh. 500,000 na Maduhu Jumanne, aliyeshika nafasi ya tatu na kujinyakulia Sh. 300,000, muda mfupi baada ya kuwakabidhi zawadi zao. Wa kwanza kushoto ni Dk. Donath Ulomi, ambaye ndiye mchambuzi wa shindano hilo.

MWENYEKITI wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi,amesema  vijana wanaosubiri mifumo iliyowekwa iwasaidie kujikwamua kiuchumi wataendelea kubaki kuwa watumwa wa maamuzi ya watu wengine.

Mengi alitoa kauli hiyo jijini Dar esSalaam, leo wakati akikabidhi zawadi kwa washindi watatu walioshinda shindano la wazo bora la 'kutweets na Mengi'.

Amesema kwa sasa vijana wengi wanamaliza elimu ya msingi Sekondari na vyuo vikuu ambao hawana ajira wala mitaji na wengi wao wanajisikia kama hawana pa kutokea.

Aliongeza kuwa  licha ya serikali, jamii na wazazi kuwa na wajibu katika jambo hili kijana anapaswa kuwa mtu wa kwanza kutafuta njia inayowezekana kwake.

Swali la mwezi julai lililowatoa washindi hao liliuliza “Kijana asiyekuwa na ajira wala fedha anawezaje kuanza kujijenga kiuchumi”ambapo Tony Alfred muuza kahawa katika kituo cha mabsi Ubungo aliibuka mshindi  wa kwanza.

Alfred ambaye ni msomi wa shahada ya masoko kutoka chuo kikuu cha Da resSalaam, aliwashinda John Mkungu na Maduhu Jumanne kwa jibu lake lililoeleza kuwa “kama kijana fikiria katika hali uliyopo ni nini unachoweza kufanyia jamii yako, ukipata jibu huo ndio mtaji na ajira yako.”

Kutokana na ushindi huo Alfred amejipatia Sh Mil 1 ambapo John Mkungu alishika nafasi ya pili na kujipatia kiasi cha Sh laki 5 na  maduhu jumanne alijipatia sh. laki 3

Mengi aliongeza kuwa kutokana na watu wengi kuchangia katika mtandao wake wa kijamii wa Tweeter, ataanda mpango wa kuyakusanya mawazo yaliyokuwa mazuri na kuyaweka katika mfumo sahihi kisha kuyafikisha kwa vijana wengine kupitia mashuleni na vyuoni.


Akizungumzia ushindi wake Alfred alisema Alfred alimshukuru Mengi kuanzisha mfumo huo na kuwataka vijana wenzake wasikate tamaa pale wanapokosa ajira za serikali.

Kumbuka hapo May 13 mwaka huu Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Dr. Reginald Mengi alianzisha shindano la ku 'Tweet' ambalo litakuwa likifanyika kilamwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja na mshindi wa kwanza atakayeandika tweet bora juu ya kupigana vita dhidi ya umasikini atajipatia sh. millioni moja. Kwa habari zaidi juu ya shindano lililopita tembelea

VYANZO : Blogu ya Hakingowi na mtandao wa IPP Media.

0 Response to "“Vijana wanaosubiri mifumo iliyowekwa iwasaidie kujikwamua kiuchumi wataendelea kubaki kuwa watumwa wa maamuzi ya watu wengine.” -Dr. Mengi."

Post a Comment