HATIMAE ILE NYAMA YA KUTENGENEZA MAABARA YAANZA KULIWA. | JIFUNZE UJASIRIAMALI

HATIMAE ILE NYAMA YA KUTENGENEZA MAABARA YAANZA KULIWA.

Angalao ina ladha ya nyama!

 Professor Mark Post pichani wa Maastricht University  Netherlands.
Hatimae ile nyama ya kutengenezwa maabara (artificial meat) sasa imeanza rasmi kutumika kama kitoweo. Mwaka 2004 niliwahi kuripoti katika Jarida moja lililokuwa likitoka kila mwezi hapa nchini  liitwalo SAYARIMPYA juu ya utafiti uliokuwa ukiendelea wa kutengeneza nyama maabara. Habari hizo nilizitoa katika mtandao wa Associate Press.

Jarida lenyewe lilikuwa ni hili hapa chini na habari yenyewe ilisomeka hivi;




Nyama kutengenezwa maabara.
Timu ya kimataifa ya watafiti imependekeza teknolojia mpya ambayo itaweza kufanikisha utengenezaji wa nyama kwa kiasi kikubwa. Ukuzaji huo wa nyama  siyo kama ule uliozoeleka wa kufuga mifugo kama ngombe bali ni kwa njia ya kimaabara.

Wataalamu hao wanasema  kulingana na maendeleo katika uhandisi wa tishu (Tissue engineering) chembechembe hai (cells) za mnyama huchukuliwa  na “kuoteshwa” maabara, seli hizo hatimae hukua na kuwa nyama.

Teknolojia hiyo itakuwa na faida kwa binadamu na vilevile kwa mazingira. “Kinadharia, seli moja tu inaweza kutengeneza nyama inayoweza kuliwa na watu dunia nzima na jambo hilo linaweza kufanyika pasipo kuharibu mazingira, hili ni wazo zuri sana” alisema Jason Mathey wa chuo kikuu cha Marryland na mmoja wa mainjinia waliochapisha utafiti huo kwenye jarida moja liitwalo “Engineering ajaournal”

Kuotesha nyama maabara kunaweza kuondoa ule umuhimu wa kufuga mamilioni ya mifugo katika mazingira duni na itasaidia kupunguza uharibifu wa mazingira. Nyama hiyo pia inaweza kuwa bora na safi zaidi ya ile ya kawaida. Teknolojia hiyo hapo kabla ilikuwa ikitumika kwa ajili ya utafiti wa kitabibu pekee, ni nyama kidogo tu kwa ajili ya kula iliyowahi kutengenezwa na watafiti wa shirika la mambo ya anga la Marekani NASA;

Lakini pia teknolojia hiyo inaweza kuzusha upinzani na ubishani mkubwa kimaadili kwa makundi mbalimbali ya kidini na kijamii. Inaweza pia ikawa ni suluhisho kwa wale wasiopenda kula nyama iliyotokana na mnyama aliyechinjwa.

Habari  na shirika la (AP)


Sasa miaka zaidi ya 8 imepita utafiti huo umezaa matunda baada ya nyama hiyo kuanza kuliwa rasmi siku ya tarehe 5, mwezi huu. Kati ya watu  wa mwanzo kuionja alikuwa ni mtafiti wa chakula Hanni Rutzier aliyetamka hivi, “Nilitegemea mnofu wake kuwa laini zadi ……..inakaribiana sana na nyama ya kawaida lakini siyo laini hivyo”

 Nyama hiyo ilikaangwa kwenye kikaango na vipande viwili vikapewa watu waliojitolea kula.

Mwingine ni John Schonwald , mwandishi wa maswala ya chakula aliyesema, “Kilichopungua ni mafuta lakini ni sawa na hambaga ya kawaida, kilichoonekana tofauti ilikuwa ni ladha yake”

Nyama hii huchukua miezi mitatu kuota ikiwa  maabara kwa kutumia seli chache zinazotokana na ng’ombe wa ukweli. Mtengenezaji wake, mwanasayansi wa kidachi, Mark Post anadai kwamba  hii inaweza ikaleta mapinduzi makubwa katika sekta ya chakula duniani. Anaamini bidhaa za nyama ya kutengenezwa maabara zinaweza zikajaa madukani na kwenye masupermarket  ndani ya muongo mmoja tu ujao.

Wakati akiionja, alipoulizwa ikiwa atawalisha wanawe nyama hiyo, mtaalamu huyo alijibu kwamba amewawekea wanawe hao nyama kidogo na baadaye angekwenda kuwapa nao waonje.

Hatua nyama inazopitia.



Pia imebainika kwamba mmoja wa wafadhili wakubwa wa mradi huu ni mwanasayansi wa kompyuta wa Kimarekani, Sergey Brin na ambaye pia ndiyo mwanzilishi mwenza wa kampuni la Google. Mwenzake ni Larry Page.

Sergey Brin anamiliki asilimia 16 katika kampuni hili kubwa kabisa la mtandao (Internate search giant). Utajiri wake unakaribia kufikia Pauni billion 13.6 mwaka 2012. Inakadiriwa kwamba katika mradi huu wa barger za nyama zinazotengenezwa maabara, aliwekeza kiasi cha pauni  215 elfu.

Amewahi kuwekeza pia katika mradi wa safari binafsi za anga  za juu hususani mwezini. Mradi mwingine  ni utafiti wa nishati na madini katika sayari na maumbo mengine kama vimondo nje ya sayari hii ya dunia katika juhudi za kutatua tatizo la uchafuzi wa mazingira na upungufu wa nishati katika sayari ya Dunia.

CHNZO : MAIL ONLINE.

0 Response to "HATIMAE ILE NYAMA YA KUTENGENEZA MAABARA YAANZA KULIWA."

Post a Comment