BIASHARA
YA SUPU NA CHAPATI SEHEMU YA 2: SUPU
Katika somo hili tutakwenda kujifunza vitu vifuatavyo;
ü Aina
kuu 4 za supu
ü Jinsi
ya kupika supu nzuri kwa ajili ya biashara
ü Jinsi
ya kupika supu ya kongoro
ü Changamoto
za biashara ya supu
ü Siri
5 ili supu ikulipe vizuri
AINA
KUU 4 ZA SUPU
Kuna aina nyingi za supu kulingana pia na aina ya nyama zinazotumika
kupika supu hizo. Ifuatayo ni orodha ya nyama zinazotumika zaidi kwa supu;
1. Nyama ya Ng’ombe
· Nyama
yenyewe
· Utumbo
· Kichwa
· Makongoro(miguu)
· Ulimi
· Mkia
2. Nyama ya Mbuzi
· Nyama
yenyewe
· Utumbo
· Vichwa
· Makongoro(miguu)
3. Nyama ya Kuku
4. Samaki na viumbe wengine wa baharini kama vile Pweza
nk.
Watu wanapenda sana supu na supu iliyozoeleka zaidi
katika maeneo mengi ni ile ya ng’ombe na mbuzi. Supu hunywewa kama kifungua
kinywa muda wa asubuhi lakini pia wapo wanaokunywa supu hata nyakati za jioni mfano katika vituo
mbalimbali vya mabasi(stendi) utakutana na watu wakifurahia kunywa supu na
vitafunwa kama chapati, ndizi na maandazi asubuhi hata na jioni.
Bishara ya supu pamoja na kwamba ina uwezo wa kumpatia
mtu faida nzuri lakini ina changamoto ambazo mtu asipokuwa makini nazo anaweza akaona haimlipi kabisa.
Tutaziona changamoto hizo baada ya kuona kwanza jinsi ya kupika supu
JINSI
YA KUPIKA SUPU NZURI NA TAMU KWA AJILI YA BIASHARA
Mahitaji:
· Nyama
kiasi unachohitaji
· Maji
· Chumvi
· Kitunguu
swaumu kilichosagwa
· Tangawizi
iliyosagwa
· Pilipili
manga
· Kitunguu
maji kilichosagwa
· Unaweza
pia kuweka ladha ya supu inayouzwa madukani
· Viungo
vingine ukipenda
Maandalizi:
1. Osha
nyama yako vizuri na kama ni utumbo basi hakikisha unachukua muda wa kutosha kuuosha
kwani utumbo huwa na kawaida ya kuwa na mchanga.
2. Katakata
vipande nyama yako na uitie kwenye sufuria
3. Tia
chumvi kiasi kulingana na wingi wa nyama yako
4. Ongeza
viungo vyako vingine kama nilivyotaja pale juu
5. Bandika
jikoni sufuria lako bila ya kuweka kwanza maji hadi pale nyama itakapobadilika
rangi na maji yake ya asili kuonyesha yanaanza kukauka
6. Ongeza
maji kiasi unachoona kitatosha nyama iive na kubaki kama supu kuepuka kuja
kuongeza maji supu ikiwa imeshaiva tayari kwani itapoteza ladha
7. Punguza
moto uwe wa kiasi wakati supu ikikaribia kuiva kusudi supu ijichuje vizuri na
kuifanya iwe na ladha ya kupendeza.
NB:
Unaweza wakati wa kuweka viungo ukaongeza mbogamboga na vitu kama njegere,
karoti na viazi ulaya kulingana na mapenzi ya wateja wako kwani wengine huwa
hawapendi supu iliyotiwa viungo sana.
Vilevile viungo kama pilipili na ndimu au limao wateja
wana uhuru wa kuchagua wenyewe kama waweke ama la, hivyo viungo hivi viwekwe
pembeni kwenye sahani ya supu.
JINSI
YA KUPIKA SUPU YA KONGORO
Tofauti na supu ya nyama au ile ya utumbo,supu ya
makongoro(miguu ya ng’ombe) ina wateja wake maalumu na ukiweza kuizoesha eneo fulani
unaweza kupata wateja wengi wa kudumu kila siku na hasahasa huwa ni wanaume
kwani inaaminika kwamba supu hii huongeza nguvu za mwili.
Upishi wake hauna tofauti sana na ule wa supu ya nyama au
utumbo isipokuwa tu hii huchukua muda
mrefu zaidi jikoni na maandalizi yake kama ilivyokuwa utumbo unatakiwa uyaoshe
vizuri na kurudia kuyaparua kwa kutumia kisu au kiwembe ili kuondoa manyoya
yote yaliyobaki kwani wauzaji mara nyingi hawayasafishi vizuri
CHANGAMOTO
ZA BIASHARA YA SUPU
1.
Supu kuwa kidogo kuliko nyama yenyewe
Kama hujawa makini utajikuta kila siku ukimaliza supu/mchuzi
wote huku nyama ikiwa bado haijaisha, hii ina maana kwamba unakuwa umezidisha
kipimo chako cha supu, umewatilia wateja supu nyingi zaidi kuliko ilivyotakiwa.
Wauzaji supu wengi hukimbilia kuongeza maji kwenye sufuria la supu jambo
linalosababisha supu hii ya awamu ya pili kuwa nyepesi na isiyokuwa na ladha
nzuri kama ile ya awali na mteja anayekutana nayo si ajabu kesho asije tena na
atamwambia na mwingine kuwa kwako supu siyo nzuri.
Suluhisho la changamoto hii ni mtu kujitahidi kujenga
uzoefu wa kujua kiasi fulani cha nyama
kinatakiwa kitoe supu ujazo gani na hivyo tokea mwanzoni unapoongeza
maji kwa ajili ya supu ufahamu kabisa ni maji kiasi gani utatakiwa kuongeza ili
mpaka supu inapoiva basi kiasi kinachohitajika tu ndicho kibakie kwenye sufuria
lako.
Na pia kiasi hicho cha supu uhakikishe kitatoa idadi ya
bakuli ulizokadiria kwamba zitarudisha ghara zako zote na faida juu. Wakati wa
kuwapimia wateja supu ni lazima uhakikishe unazingatia sana kipimo kile
ulichopanga, usizidishe wala kupunguza na kataa kwa hekima pale wateja
wanapokushawishi uwaongezee supu watakavyo pasipo kuongeza pesa.
Wateja wengi wamejijengea imani kwamba supu au mchuzi
hauna gharama na kwamba muuzaji anaweza tu kuongeza maji atakavyo kupata supu
nyingi, kumbe hawajui kufanya hivyo ndiyo kuwapatia tiketi ya kukuhama kwani
supu yako itakuwa na maji mengi tena isiyo na ladha ya kuvutia kabisa. Wafahamishe
kwa hekima wanunue bakuli nyingine ya supu kwani nyongeza-nyongeza itakusababishia
hasara na mwishowe ushindwe kuwapatia huduma waipendayo.
2. Kutokuendana
na muda wateja wanaotaka supu
Supu ya asubuhi inatakiwa iwe tayari mapema kwa kadiri
inavyowezekana ili kuwavutia wateja wa aina mbalimbali. Kwa mfano wapo wateja
ambao hupenda kuwahi kazini mapema sana na utakuta wanapenda wapate supu hata
saa 12 asubuhi, kuna wengine watataka wanywe supu saa 1, saa 2 nk. Kwa hiyo ni
juu yako kuhakikisha wote unawaridhisha kwa kuwahi mapema kuivisha supu yako.
Ili supu iweze kuiva mapema ni lazima pia maandalizi yake
yafanyike mapema hata ikiwezekana siku moja kabla na usiku wa kuamkia siku
yenyewe. Maandalizi siku moja kabla ni pamoja na jiko-kununua mkaa au gesi,
ununuzi wa mahitaji mengine yote vikiwamo viungo pamoja na usafi wa vyombo na
mazingira.
Nyama kwa ajili ya supu inafaa zaidi inunuliwe usiku ama
alfajiri ikiwa freshi na watu wengi hununua moja kwa moja kutoka machinjioni
ambapo kwenye miji mingi kama Dar es salaam uchinjaji wa ng’ombe na mbuzi
huanza saa 4 usiku mpaka saa 11 alfajiri, ni juu yako kuamua utanunua saa ngapi
ili supu yako isichelewe.
Ikiwa unatumia nyama iliyolala kwenye friji basi
utainunua buchani siku moja kabla ili uanze kuichemsha kuanzia saa 10 au saa 11
alfajiri. Hata hivyo nyama nzuri itakayotoa supu yenye ladha ya kupendeza zaidi
ni ile ya siku hiyohiyo ambayo haijalala.
Vitafunwa navyo viandaliwe mapema ikiwezekana kuwe na mtu
maalumu kabisa kwa ajili ya kazi hiyo na siyo yuleyule anayeandaa supu ukute
ndiye huyohuyo anayeandaa na vitafunwa. Kufanya majukumu yote mawili mtu mmoja
mara nyingi husababisha ucheleweshaji usiokuwa wa lazima na hii siyo sifa njema
kwa wateja wako.
3.
Supu kutokwisha kwa wakati
Unategemea supu iliyopikwa kumalizika kwa siku moja
lakini kutokana na sababu mbalimbali unaweza kukuta haiishi na hata wakati mwingine inabaki mpaka siku inayofuata
jambo ambalo si zuri kwani supu ni chakula kinachoharibika upesi na ikilala ni
rahisi wateja kutambua hata kama utaihifadhi vizuri namna gani.
Sababu kubwa kwanini supu hubaki ni wateja kuwa wachache
mno au kukisia kwa makosa kiasi cha supu unayopika kulingana na idadi ya wateja
uliokuwa nao. Ili kuhakikisha kila siku supu yako inaisha, jitahidi kupika
kiasi cha supu inayolingana na idadi ya wateja uliokuwa nao tu huku ukiendelea kuvutia
wateja wapya mpaka pale watakapoongezeka basi ndipo na wewe uongeze kiasi cha
supu unayopika.Hili litawezekana kwa kudumisha huduma kila siku bila ya kukosa wateja
wakuzoee.
Kuna njia mbili kubwa unazoweza kutumia kuhifadhi supu
iliyobaki isiharibike, ya kwanza ni kuitia katika friji na ya pili kuipasha
moto vya kutosha kila baada ya masaa 6 kuisha.
4.
Kuchagua saizi mbaya ya bakuli za supu
Bakuli za kunywea supu wateja zinapaswa kulingana na
kipimo ulichoamua kutumia. Ikiwa umeamua kuuza supu ya shilingi 1,500 basi
bakuli zisijekuwa ni za supu ya sh. 2,000/= nikimaanisha zisiwe oversize kwani wateja wana tabia ya
kuhisi wanapunjwa bakuli isipojaa vizuri mpaka juu, hivyo basi nunua bakuli
ambazo ukipima kipimo chako inajaa hadi juu kuepusha ushawishi wa kuongeza
kiasi cha supu. Halikadhalika pia zisije kuwa ndogo mno ukawapunja wateja
watakimbilia kule wanakouziwa kwa haki. Pima supu inayokulipa na siyo
itakayokusababishia hasara.
5. Ukataji
wa vipande vya nyama
Idadi ya vipande vya nyama ni kitu cha muhimu sana, ni
lazima idadi iendane na idadi ya bakuli za supu unazohitaji ili kurudisha
gharama zote na faida juu. Kuna wengine hukatakata kabisa idadi ya vipande
kabla ya kuanza kuchemsha supu na wengine huamua kuchemsha kwanza nyama mapande
makubwa makubwa na kisha kuja kukatakata vipande vidogo wakati wa kumhudumia
mteja supu.
Mimi huwa napendelea zaidi aina ya kwanza ya ukataji
kwani huepusha kuchafua mazingira ya sehemu unayouzia supu kila mara kuchafua
kibao cha kukatia nyama hukaribisha inzi. Kama hesabu zako zinasema kila mteja
atapata vipande 3 basi usizidishe wala kupunguza labda tu mteja mwenyewe alipie
vipande vya ziada.
6.
Wateja wanaopenda wauziwe mchuzi (supu tupu) isiyokuwa na nyama.
Wauzaji wengi hii huifanya kwa kuwauzia wateja supu tupu
kwa nusu bei au hata chini ya hapo lakini hii mara nyingi inavuruga mahesabu ya
supu na hazitatoka idadi ya bakuli ulizopanga zitoke matokeo yake supu inaleta
hasara. Unaweza kufanya hivyo ukijua tu kwamba kuna kiasi cha supu ya ziada
itakayobaki baada ya idadi ya bakuli ulizopanga kuisha.
7. Nyama
kuiva kupita kiasi
Wakati ukisubiri wateja waje unaweza ili wasikute supu
ikiwa imepoa, unaamua kuacha sufuria la supu kwenye moto jikoni ikiendelea
kuchemka muda mrefu. Hali kama hii husababisha nyama kuiva sana na kuwa
teketeke huku supu ikikakamia na kupungua ujazo wa awali uliopima kwamba utatoa
idadi ya bakuli zitakazokupa faida. Suluhisho la tatizo hili ni kuwa na vifaa
bora hasa jiko la gesi ama jiko unaloweza kulitumia kupasha supu yako haraka
mteja anapokuja.
Supu inapokuwa tayari imeiva, ipua sufuria na uiweke
pembeni ukisubiri wateja. Mteja akija na kukuta imepoa basi washa jiko haraka
na upashe kiasi kile unachompimia tu kwa kutumia sufuria nyingine ndogo. Funika
sufuria kubwa la supu vizuri kwa mfuniko usioruhusu wadudu kama nzi wala vumbi
kuingia ndani yake .
SIRI 5 ILI SUPU IKULIPE VIZURI.....................
·
Je, ungependa kuzijua siri
hizo 5 ni zipi?
·
Na je, ungependa pia
kushiriki katika kuandika mchanganuo wa biashara hii ya mgahawa mdogo wa supu na chapati
hatua kwa hatua katika group letu la masomo ya kila siku la Michanganuo-online?
Basi jiunge na group hilo leo uweze kujifunza na masomo mengine yaliyopita zaidi ya 100 tuliyoyaweka katika channel yetu ya Telegram
Ndani ya group pia unapata mfululizo mzima wa somo hili la chapati laini na supu, siri za kupika chapati laini na tamu.
Ada
ya mwaka mzima ni Tsh. 10,000/=
Unatumiwa pia na zawadi ya vitabu na michanganuo ya biashara mbalimbali
Namba za malipo ni 0712202244 au 0765553030 Peter Augustino Tarimo, kisha tuma neno,"Niunge na Mastermind group 2023"
Michanganuo inaanza leo tarehe 16/12/2022 usiku saa 3-4
Kumbuka masomo na michanganuo ndani ya group ni kila siku, na unaweza kuamua kufuatilia baadhi ya masomo na michanganuo ile unayotaka tu, somo kama hulihitaji hulazimishwi kujifunza.
Masomo na michanganuo itabakia kwenye channel ya group kwa muda kabla ya kuondolewa ili kutoa nafasi kwa wanachama wapya kuyapata kiurahisi.
0 Response to "JINSI YA KUPIKA SUPU NZURI NA TAMU YA BIASHARA (SUPU NA CHAPATI SEHEMU-2)"
Post a Comment