Yamkini kwa muda
mrefu sasa umekuwa na wazo lako iwe ni biashara au jambo jingine lolote lile
ambalo umetamani sana kulitimiza bila mafanikio na hujui uanzie wapi. Inaweza
kuwa ni ndoto yako ya kupunguza uzito, azma yako ya kuanzisha kiwanda kidogo
cha juisi ya matunda asilia, nia ya kuandika kitabu fulani juu ya mada unayoipenda,
lengo lako na wewe kuwa na kwako/kumiliki kiwanja/nyumba au hata nia yako ya
kumiliki biashara halisi yenye mafanikio.
Katika makala yangu
ya leo hii pamoja na dondoo nyingine muhimu 4 nimekuandalia filosofia
yangu ambayo huwa naitumia wakati
ninapotaka kukamilisha malengo yangu mbalimbali yakiwemo yale ya uandishi wa
vitabu au projekti nyinginezo mbalimbali, na nafikiri phylosophy hiyo hutumiwa hata na watu wengine mbalimbali pia
wanapotaka kuwa na kitu fulani au kutimiza
malengo yao, nayo ni hii namba 1 hapa chini;
1.
KUJIWEKEA MALENGO
Kabla haujaanza mwaka
wa 2020 unatakiwa kwanza uwe na picha halisi akilini ya kile kitu unachokitaka
kwa mwaka huu(najua unataka vitu vingi
lakini kuna kile muhimu zaidi kwako unachowaza kuwa nacho au kukifanya) Ukishakuwa
na lengo sasa jiulize maswali yafuatayo;
· Kwanini unakitaka kitu hicho?
· Ungetaka ukipate
mpaka kufikia muda gani?
Kwa mujibu wa kitabu changu
cha MIFEREJI 7 YA PESA itakuwa ni
jambo gumu sana kufanikisha lengo lolote lile ikiwa kama hautaweza kabla
kuliweka bayana lengo hilo liweze kupimika, kutekelezeka na kuwa na muda
maalumu wa kulitekeleza. Kwa kimombo wanaita vitu hivi, Specific, Measurable,
Attainable, Realistic and Time based(S.M.A.R.T)
Hebu tuchukulie kwa
mfano unadaiwa deni la shilingi million 5 na umeweka lengo mwaka huu wa 2020
kulipunguza deni hilo au ikiwezekana kulifuta kabisa. Badala tu ya kusema
utapunguza deni au ikiwezekana kulimaliza, sema utapunguza kiasi fulani
mathalani, “nitapunguza milioni 2, 3 au zote 5”
Ikiwa labda umelenga
mwaka wa 2020 ujiwekee pesa kwa ajili ya kujenga nyumba yako na wewe uwe na
kwako kama wengine, panga kabisa kiasi kamili kinachotosha kujenge nyumba hiyo,
ni lini utahitaji kiasi hicho na vilevile kitu cha muhimu sana ni lazima pia
upange ni kiasi gani utakacholazimika kuweka akiba kidogokidogo kila siku/mwezi
au mwaka ili kuweza kulifikia lengo lako hilo la kujenga kwa muda ulioupanga.
Fikiria ni mabadiliko gani utakayoyafanya kwenye maisha yako ya kila siku ili kuweza kutimiza lengo lako.
Hapa nitakupa mfano
wangu mimi binafsi wakati ninapokuwa naandika vitabu vyangu . Nikishaweka lengo
la kuandika kitabu fulani, huwa napanga kabisa kitabu hicho nikimalize kwa
gani. Kisha kila siku najiwekea malengo madogomadogo kwa mfano ya kuandika
kurasa mbili mbili au aya kadhaa.
Kwahiyo hata ikiwa
kitabu ni kikubwa kama kilivyo kile cha MICHANGANUO
YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI zaidi ya kurasa 410, najikuta kwa kuandika kidogokidogo kila siku hatimaye
namaliza kitabu kizima kwa urahisi kabisa. Kwahiyo Lengo na hata liwe kubwa
kiasi gani au dogo ukifuatilia kanuni hii ni lazima tu ulitimize. Filosofia hii
imenisaidia sana mimi binafsi na ni
matumaini yangu hata na wewe pia itakusaidia.
2.
FANYA UFUATILIAJI
Ikiwa utapenda
kufaulu kwenye jambo lolote lile maishani hususani malengo uliyojiwekea ni
lazima ufanye ufuatiliaji wa kile ulicholenga. Hauwezi kujua unakoelekea ni
wapi ikiwa hujui ulipo ni wapi. Ukishaweka malengo yako katika hatua ya kwanza,
sasa fanya ufuatiliaji na upime ikiwa kama kweli yanaoana na vile vipengele vya
S.M.A.R.T
Kama mfano lengo lako
ni la kupunguza deni kama tulivyotangulia kusema pale mwanzoni, basi ni wakati wa
kuhakikisha kama kweli unapunguza matumizi yako kwa kiasi ulichopanga, deni
linapungua na mapato yako yanaongezeka kusudi uweze kupata pesa za ziada za
kupunguza deni lenyewe. Hapa ni lazima utafute njia itakayokuwezesha kufanya
huo ufuatiliaji mfano unaweza kutumia ‘app’ za kwenye simu, programu za
kompyuta, credit card nk. Credit card husaidia ufuatiliaji kwani mwisho unaweza
kucheki taarifa nzima ya mwezi mzima kiasi cha miamala uliyofanya bila
kuandika-andika.
Lakini njia rahisi
kabisa kuliko zote unayoweza kufanya ufuatiliaji ni ile ya jadi ya kuandika
katika daftari la kawaida kwa kalamu, chora jedwali(spreadsheet) na ujaze
taarifa zako kila siku, umetumia kiasi kadha wa kadha, umelipa hiki na kile nk.
Ikiwa utazembea kuandika na kufanya ufuatiliaji hesabu zako zinaweza
kukushangaza, hutajua umetumia kiasi gani wala upunguze wapi na kuongeza wapi.
Kuandika vitu katika karatasi kuna maajabu mengi sana katika kutimiza malengo.
3.
KUWEKA FEDHA AKIBA IWE NDIO KIPAUMBELE CHAKO CHA KWANZA
Kuweka pesa(Savings)
ndiyo njia nyepesi zaidi ya kweli iliyojaribiwa na kuthibitika kote Ulimwenguni
kwamba inaweza kutengeneza Utajiri. Wataalamu mbalimbali wanaweza kukushauri
viwango tofautitofauti unavyopaswa mtu kujiwekea kama akiba, wengine
watakuambia, “weka asilimia 10%” wengine asilimia 5%, asilimia 20% nk. Lakini
ukweli ni kwamba kama unataka kweli kuwa huru kifedha haraka au kutimiza lengo
lako la muda mrefu ‘faster’ basi huna budi kujiwekea akiba ya pesa kiasi kingi
kwa kadiri utakavyoweza wewe, hata kama utaweka asilimia 80% ya mapato yako na
mambo yakaenda vizuri bila kuathiri maisha yako, wewe weka.
4. LIPA
MADENI YAKO
Unapokuwa na deni
hauna tofauti na mvuvi aliyetia nanga baharini wakati huohuo akitaka ashindane
mbio za mashua majini. Nanga haitamuachia asogee mbele hata sentimita moja. Ni
kama inakuvuta nyuma wakati wenzako wanakata maji. Tumia akiba yako kupunguza
madeni hasa yale yaliyokuwa na riba kubwa zaidi kwanza.
5.
WEKEZA PESA ZAKO
Sasa baada ya kulipa
madeni yako yote, kile kiasi cha pesa ulichokuwa ukilipa madeni kiongezee
kwenye biashara au vitegauchumi vyako vingine vyenye uwezo wa kuzalisha pesa
zaidi ikiwa kama kweli upo ‘serious’
kuufikia uhuru wa kifedha. Vitegauchumi vizuri visivyokuwa na hatari kubwa ni ardhi
na majengo
kwani thamani yake huwa inaongezeka kadiri muda nao unavyozidi kusogea. Pia
unaweza ukavitumia kama dhamana ukitaka kwenda kukopa kwenye taasisi za fedha au
benki.
Mwisho
wa makala hii, Asante sana
................................................................................................
Taarifa
muhimu !
OFFA YA MWISHO KABISA KWA MWAKA 2019
(Haitakaa
itokee tena offa kama hii!)
Katika vipindi
tofauti mwaka 2019 tulikuwa tukitoa offa hii kubwa ya kujiunga na GROUP LA MICHANGANUO-ONLINE na watu wengi sana waliweza kuichangamkia.
Group la mwaka 2019 ndio tayari limefikia tamati mwezi huu wa Desemba na sasa
tunaanza tena rasmi kusajili wanachama kwa ajili ya Group la mwaka 2020.
Asilimia 95% ya
wanachama wa group linaloisha muda wake wote wameamua kujiunga tena na group la
2020, hii inamaanisha kwamba nafasi kwa wanachama wapya safari hii zitakuwa
chache na pengine hata isifike Machi 2020 kabla hazijamalizika kabisa kwani
kama kawaida sisi hatunaga utaratibu wa kuendesha magroup mawili kwa wakati
mmoja. MICHANGANUO-ONLINE ni moja tu na litaendelea kuwa moja siku zote.
Kujiunga na group la
2020 kiingilio ni Sh. 10,000/=(Elfu 10 tu) na ada hii ni ya MWAKA MZIMA wa 2020, hakuna malipo ya ziada wala yaliyojificha nyuma ya pazia na
utashiriki programu zetu zote za masomo, mijadala pamoja na semina mbalimbali
za kuandaa Michanganuo bunifu ya viwanda, kumbuka kaulimbiu yetu kuu 2020 ni “THE
TANZANIA INDUSTIAL REVOLUTION 2020”
OFFA YENYEWE NI HII
HAPA
Unapojiunga kabla ya
tarehe 15 January 2020 utapata Offa yetu kubwa ya Vitabu na Michanganuo
mbalimbali ifuatayo. Offa hii ilitakiwa iwe imeshafungwa rasmi Desemba na Group
la 2019 lakini kutokana na rai za wadau wengi hasa walio kwenye utaratibu wangu
wa kutumiwa masomo kwa njia ya email, basi nimeona ni busara kuisogeza mbele
kidogo ili wale kwa sababu mbalimbali hawakuweza kupata kiingilio basi wawe wamepata.
Baada ya hapo mtu
atakayehitaji vitu vilivyoko ndani ya offa hii itabidi avinunue kimoja kimoja
kwenye DUKA LETU HILI HAPA LA VITABU NA MICHANGANUO ambapo, badala ya
sh. elfu kumi atalipa sh. elfu 10 kwa kila kimoja sawa na sh. elfu 95 ikiwa
atapenda kupata vitu(items) zote 15.
OFFA ina vitu
vifuatavyo;
1. Kitabu cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA
UJASIRIAMALI kwa lugha ya Kiswahili.
2. Kitabu kipya (Saikolojia na Utambuzi wa
hali ya juu Kifedha(Advanced Money Literacy & Psychology)
3. Kitabu cha masomo ya Mzunguko chanya wa
fedha 2018 part 1
4. Kitabu cha Masomo yam ZUNGUKO chanya wa
fedha 2018 part 2
5. Kitabu cha jinsi ya kuandika michanganuo
ya biashara hatua kwa hatua.
6. Kitabu mashuhuri zaidi duniani, HOW TO
WRITTE A BUSINESS PLAN kwa lugha ya kiingereza, ndio kinachotumika vyuo vikuu
vingi duniani.
7. SEMINA: Masomo 11 ya jinsi ya kuandika
mpango wa biashara.
8. Kifurushi maarufu cha michanganuo 3 ya
ufugaji wa kuku(MKOMBOZI CHICKS PLAN 3PACKS)
9. Mchanganuo wa biashara ya mgahawa(JANE
RESTAURANT) kwa Kiswahili na kiigereza
10.
Mchanganuo
wa biashara ya kilimo cha matikiti maji.
11.
Semina
na Mchaganuo mzima wa Kiwanda cha tofali(KILUVYA QUALITY BRICKS)
12.
Vielezo(Templates)
za michanganuo ya biashara inayokuwezesha kuandika michanganuo kwa muda mfupi.
13.
Mfumo
mpya wa usimamizi wa duka la rejareja(2 IN ONE STORE MANAGEMENT SYSTEM)
unaomwezesha mmiliki wa duka dogo la rejareja au la kati kuthibiti mapato yake
pasipo msaidizi kudokoa hata senti 5
14.
Somo
muhimu sana la mzunguko wa fedha.
15.
Ukurasa
mmoja wa mchanganuo.
Ukijumlisha gharama
ya vitu vyote katika offa jumla yake ni sh. 95,000/=. Kwa hiyo ukiwahi offa ni sawa na kusema umeokoa sh. elfu 85, (85,000/=) Mjasiriamali Unasubiri
nini ? Tembelea hapa Duka letu la Vitabu & Michanganuo Mtandaoni
la Self Help Books Tanzania liitwalo; Smart Books Tz kujionea bei halisi ya vitu vilivyoko kwenye
offa hii ya kutupa!
0 Response to "JINSI 2020 UNAVYOWEZA KUGEUZA WAZO LAKO LA MUDA MREFU KUWA BIASHARA HALISI YENYE MAFANIKIO"
Post a Comment