Ikiwa sababu na chanzo
cha kifo cha Reginald Mengi, mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, tajiri na
mfanyabiashara mashuhuri bado kujulikana rasmi kila mtu nchini Tanzania na nje
ya nchi ana tashwishi ya kutaka kujua ugonjwa uliomuua mzee Mengi, ni nini hasa kilichomsibu Mzee huyu
aliyekuwa mmiliki na mwenye mchango mkubwa katika tasnia nzima ya vyombo vya
habari na viwanda kwa ujumla.
Ni takriban miezi miwili
tu imepita tangu Mzee Mengi ahutubie katika shughuli ya kumuaga Ruge Mutahaba ‘kijana
wake’, na mtu mwingine aliyekuwa na umuhimu mkubwa katika tasnia ya habari na
biashara kwa ujumla nchini Tanzania. Katika hotuba yake Mzee Reginald Mengi
alisema kuwa Ruge Mutahaba hakuwa amekufa bali anaendelea kuishi na sisi
Kiroho.
Kwa hiyo kama
ilivyokuwa kwa kauli yake hiyo, Watanzania hatuna budi kukubali ukweli huo
kwamba Mzee Reginald Mengi hajafa, tunaishi naye kupitia maono yake mbalimbali
aliyotuachia katika kazi zake zote kikiwemo kitabu chake cha I CAN I WILL IMUST. Kilichokufa ni mwili wake tu au “Kasha”
kama alivyosema yeye mwenyewe kwenye hotuba hiyo iliyonukuliwa yote hapa chini;
Bwana
asifiwe, Assalaam Alaykum,
Ndugu
zangu mimi sina mengi ya kuzungumza, nimekuja hapa kumuaga kijana wangu
aliyeitwa na Bwana Mungu. Lakini nina habari njema kwenu, habari yenyewe ni
kwamba Ruge hajafa kwasababu roho haifi, na mtu ni roho. Mwili ni kasha tu la
roho. Tutazika mwili wake lakini hatutazika roho yake. Mkumbuke kwamba
tuliumbwa kwa sura na mfano wa Mungu na Mungu anatupenda sana.
Kwa
hiyo nimesema kwamba kilichokufa ni kasha tu la Ruge siyo roho yake. Kwahiyo
Ruge bado anaishi na siku moja atakuja kwenu kufahamu kwa kweli anaishi.
Kwahiyo unakufa tu wakati roho imekufa,
lakini roho haifi. Na Ruge ataendelea kuishi mahali pawili(makao mawili) Ataendelea
kuishi kwa Baba Mungu na katika roho zetu kwasababu alitupenda na tulimpenda.
Kwa hiyo makao ya kwanza yatakuwa ni Mbinguni na ya pili katika roho zetu Wanadamu.
Mimi
Ruge alikuwa kijana wangu, muungwana sana, He
was a true Human Being ambaye alikuwa na upendo, na vijana wengi Tanzania wamefaidika
sana kuishi kwa Ruge. Amewapa matumaini, na katika tasnia ya habari ameleta
mabadiliko makubwa sana na mengine leo hamtafahamu lakini aliyaleta.
Naweza
nikasema kwamba sisi badala ya kulia kama alivyosema Ruge, tusherekee, tufurahi
naye. Badala ya kulia tumuombee ili roho yake ilale mahali pema Mbinguni. Ningependa
kuwapa pole wote sana, wazazi, ee.. Kusaga na vijana wengine na Mungu naomba tu
awape Moyo wa kuzidi kumuombea. Mkae kwa Amani ya Bwana. ASANTENI.
Chanzo
cha habari hii ni Video kutoka AZAM TV,
ukitaka kuangalia video hiyo bonyeza hapo.
0 Response to "MZEE REGINALD MENGI HAJAFA, ATAENDELEA KUISHI KATIKA ROHO ZETU SIKU ZOTE"
Post a Comment