JINSI YA KUANZISHA BIASHARA YA UWEKEZAJI KWENYE ARDHI NA MAJENGO HATA KAMA HUNA MIA MFUKONI | JIFUNZE UJASIRIAMALI

JINSI YA KUANZISHA BIASHARA YA UWEKEZAJI KWENYE ARDHI NA MAJENGO HATA KAMA HUNA MIA MFUKONI

Uwekezaji majengo

Biashara ya ardhi na majengo ni moja kati ya vyanzo vya utajiri vya uhakika zaidi duniani lakini watu wengi wameishiwa kabisa hamu ya kufikiria kuanzisha biashara ya kuwekeza kwenye ardhi na majengo kutokana na kukosa pesa za kutosha kufanya hivyo na dhana potofu iliyojengeka kwamba biashara hii walio na uwezo nayo ni matajiri tu wenye pesa zao. Watu hao hujiuliza hivi; 

“Ikiwa kama mimi sina hata shilingi mia mfukoni ya kuanzisha biashara ya kawaida, sembuse niweze kuingia kwenye uwekezaji wa ardhi na majengo unaohitaji mamilioni ya pesa?”

Ukweli ni kwamba ni rahisi sana mtu kutengeneza pesa ikiwa tayari unazo pesa na hii ndiyo sababu kubwa ya matajiri wengi kuendelea kuwa matajiri wakati masikini wakiendelea kudidimia katika umasikini mkubwa.

SOMO: Unajua biashara yenye faida kubwa na ya haraka mara mbili ya mtaji unaowekeza?

Hata hivyo habari njema kwa watu wa namna hii ni kwamba zipo njia chache ambazo mtu asiyekuwa na hata mia mfukoni anaweza kuzitumia mwishowe akaweza kutimiza ndoto yake ya kumiliki biashara ya uwekezaji katika ardhi na majengo kwa muda mfupi sana.

Siri za kufanikiwa katika kuwekeza kwenye ardhi na majengo (Real Estate Investing) haziegemei tu kwa wale waliokuwa na pesa nyingi mfano kina Dangote, Donald Trump, Warren Buffet, Mo na Bakhresa hapana, lakini pia ikumbukwe kuwa uwekezaji kwenye Real estate siyo miradi ya kuleta utajiri wa haraka ndani ya usiku moja umeamka ukajikuta bilionea, inahitajika subira na uvumilivu wa kutosha

SOMA: Tajiri namba moja Afrika Aliko Dangote amekopa, wewe unangoja nini? 

Katika kufafanua jinsi ya kuwekeza kwenye biashara ya ardhi na majengo bila pesa nitazungumzia njia kubwa 2 watu wengi huzitumia, lakini kabla sijaanza, tambua kuwa uwekezaji katika ardhi na majengo ni miradi inayohitaji uwekezaji wa kiwango kikubwa cha fedha kuliko biashara za kawaida na pia haijalishi una umri gani kuwa mwekezaji, unaweza kuwa na umri wa miaka 15, 45 au hata 70 na kuendelea.

Ardhi na majengo ni biashara nzuri ya kuwekeza mtu wa rika lolote lile ingawa inaonekana walio na umri mkubwa ndio zaidi wanaojihusisha nayo pengine ktokana na sbabu kubwa kwamba tayari wanakuwa wameshajilimbikizia mitaji ya kutosha ujanani. Hata hivyo vijana na walio na umri mdogo wanaweza wakatumia mbinu na mikakati itakayoainishwa katika somo hili kuweza kukivuka kihunzi hiki cha kukosa mtaji.

SOMA: Biashara yenye mtaji mdogo isiyojulikana na watu wengi bado

Badilisha pia msimamo wako ambao pengine umekuwa nao kwa muda mrefu kwamba huwezi kabisa kuwekeza kwenye biashara ya ardhi na majengo bila ya kuwa hata na mia mfukoni. Na badala yake jiulize, ni rasilimali zipi nyingine unazoweza ukazitumia kutimiza ndoto yako hiyo ya kuwa mwekezaji wa ardhi na majengo.

Serikali kupitia Wizara ya uwekezaji, viwanda na biashara katika dira ya biashara tayari imekwishaweka mazingira mazuri kwa kila mtu kwenye sekta binafsi anayefikiria kuanzisha biashara yeyote ile Tanzania, hivyo ni uamuzi wa mtu mwenyewe kunyoa au kusuka. Utajiri maana yake ni kumiliki vitegauchumi na biashara na wala siyo kumiliki pesa kama wengi wanavyodhani kimakosa.

SOMA: Kanuni za kugundua uwekezaji unaolipa pesa nyingi zaidi ukitumia vigezo vya faida, hatari & uoevu wa mradi

Kitu cha kwanza kabisa na muhimu kuliko vyote ni kuweka malengo, mwisho ni lazima utambue kwamba pesa taslimu peke yake ni sawa na chombo tu ambacho mtu anaweza kukitumia kupata mali anazohitaji haraka, hata hivyo pesa siyo chombo pekee duniani kinachoweza kufanya kazi ya uwekezaji kwenye ardhi na majengo, kuna vyombo vingine mbadala.

Sasa hapo ndipo ninapotaka ufahamu hivyo vyombo vingine zaidi ya pesa ni vipi katika kujibu swali letu, “Nitawekezaje kwenye ardhi na majengo wakati sina hata mia mfukoni?”

Kwani uwekezaji maana yake ni nini? Kuna uwekezaji wa aina nyini, wapo wanaoamua kufanya uwekezaji mtandaoni, kuwekeza kwenye hisa, kuwekeza kwenye ardhi na majengo, kuwekeza kwenye biashara za kawaida za uchuuzi nk. mifano ipo mingi lakini kwa ujumla uwekezaji ni kitendo cha kuweka pesa zako kwenye miradi ya kiuchumi kwa lengo la kuja kupata faida hapo baadae. Kuwekeza ndiyo njia bora zaidi ya kufanikiwa kuwa tajiri iliyokuwa halali na uwekezaji kwenye ardhi na majengo ni njia salama na ya uhakika zaidio kuwekeza muda na rasilimali zako.

SOMA: Wazo la biashara ipi yenye hatari kidogo naweza kufanya kwa mtaji wa milioni 5?: Mwajiriwa serikalini

Tambua pia kuwa hakuna uwekezaji mdogo ikiwa maono yako ni makubwa, mfano kuna walioamua kuwekeza kwenye kilimo na kupata mikopo ya kilimo kwa urahisi sana lakini kumbe maono yao makubwa kichwani yalikuwa ni kuja kuwekeza kwenye biashara kubwakubwa za majengo na ardhi.

Huu ni mfano mdogo tu nimekumegea, kuna mbinu nyingi watu kote duniani huzitumia ukiwaona unawadharau lakini mwishowe unakuja kuwakuta ni mabilionea wa kutupa kama walivyo kina Trump na Warren Buffet, fuatilia somo hili hadi mwisho kuzifahamu mbinu hizo zote.

Ikiwa basi kama huna hata mia mfukoni,..................................... ...............................................................................................................................................................................................................................................................................................................
.....................................................somo litaendelea usiku leo tarehe 18/07/2023 saa 3 kwenye mastermindgroup la Michanganuo.

Mtu yeyote anaweza akajiunga na group hili kwa kulipa ada ya mwaka mzima sh. Elfu 10 tu, kupitia namba zetu, 0712202244  au 0765553030 jina ni Peter Augustino Tarimo, na kisha kutuma ujumbe kwa sms au watsap usemao;

“NIUNGE GROUP LA MASOMO NA OFFA INAYOKARIBIA KUISHA MUDA WAKE”

Muda huohuo nitakutumia vitu vifuatavyo;

1.   OFFA yetu ya vitu 12 inayokaribia kumalizika

2.   Masomo yote ya fedha tuliyojifunza kwenye group tangu limeanza (compilation)

3.   Kukuunganisha na Group la masomo na semia ikiwa unataka (wengine huwa hawapendi magroup)

 

OFFA yetu ya vitu 12 inajumuisha vitabu na michanganuo ifuatayo;

                 1.      COURSE/SEMINA: (compiled complete course) ya Jinsi ya kuandika Mchanganuo wa biashara –(Ukishindwa kuandika mchanganuo wako mwenyewe utarudishiwa pesa zako) - kwa kiswahili

                 2.       KITABU: Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali chenye course zote muhimu za BIASHARA, jinsi ya kuandaa michanganuo ya biashara na sample za michanganuo mbalimbali 10 iliyokamilika kila kitu.kwa kiswahili

                 3.      KITABU: Mifereji 7 ya Pesa na Siri Matajiri wasiyopenda kuitoa -kiswahili

                 4.      KITABU: Siri za upishi wa chapati laini-UPENDO CAFE pamoja na Mchanganuo wake kamili.-kwa kiswahili

                 5.       KITABU: Njia rahisi ya kuandika mpango wa biashara-dakika 30 - kwa kiswahili

                 6.       KITABU: HOW TO WRITE A BUSINESS PLAN  ni maarufu sana duniani na ndio hutumika vyuo vikuu vingi.-kwa kiingereza

                 7.       MCHANGANUO: Kuku wa nyama -Tumaini Broilers - kwa kiswahili

                 8.      MCHANGANUO: Kuku wa nyama –kwa kiingereza

                 9.      MCHANGANUO: Ufyatuaji tofali za saruji- kwa kiswahili

              10.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa Kiswahili

              11.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa kiingereza

              12.    MCHANGANUO: Kiwanda cha usagishaji Dona (Usado milling) - kwa Kiswahili

              13.    Kuunganishwa Group la masomo ya kila siku ya fedha na michanganuo mwaka mzima ukitaka. (Mentorship group) (Ni hiyari yako lakini, usipotaka hatukuunganishi)

 

Imeandaliwa na:

Peter A. Tarimo

0712202244

0765553030

 


Kujipatia vitabu vyetu au Michanganuo mbalimbali ya biashara tembelea duka letu la mtandaoni hapa la SMART BOOKS TZ


Kupata toleo jipya 2023 la kitabu cha MAFANIKIO YA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA bofya hayo maandishi.

 

Kuona kwa kifupi baadhi ya kazi tulizowafanyia wadau wetu bovya hapa>>OUR PORTFOLIO

0 Response to "JINSI YA KUANZISHA BIASHARA YA UWEKEZAJI KWENYE ARDHI NA MAJENGO HATA KAMA HUNA MIA MFUKONI"

Post a Comment