UZINDUZI WA SEMINA YA MIPANGO YA BIASHARA BUNIFU 2017 ULIVYOFANA MTANDAONI | JIFUNZE UJASIRIAMALI

UZINDUZI WA SEMINA YA MIPANGO YA BIASHARA BUNIFU 2017 ULIVYOFANA MTANDAONI

KUANDIKA MCHANGANUO WA BIASHARA
Hatimaye jana ijumaa tarehe 19/1/2017 ndiyo ilianza rasmi ile semina au mafunzo ya Michanganuo ya biashara 12 zilizo na fursa kubwa ya kuleta faida na kusababisha mtiririko wa fedha kuwa chanya katika mwaka wote wa 2018.

Mafunzo haya yametokana na utafiti tulioufanya mwaka jana 2017 katika kampeni yetu iliyoitwa Make your self great again” au “Jirudishie ukuu wako tena ambapo tulibaini kwamba watu wengi huwa tunashindwa kutimiza malengo yetu tunayojiwekea kila mwaka kutokana na sababu mbali mbali lakini kubwa ikiwa ni mzunguko mdogo wa fedha katika biashara zetu. Kwa hiyo tukaona itapendeza zaidi ikiwa tutajaribu kutafuta biashara bunifu 12 tutakazochanganua pamoja na washiriki watakaoamua kujiunga na mafuzo hayo katika mwaka mzima wa 2018.

UFUNGUZI JANA ULIVYOKUWA
Kwanza Admin alianza kama saa 11 jioni hivi kuunganisha katika kundi majina ya washiriki ambao tayari walishatuma namba zao za wasap pamoja na kulipia kiingilio cha shilingi elfu 10, Kuna makundi mawili, la MAPOKEZI na kisha lile lenyewe la MICHANGANUO ONLINE ambalo sasa wanaingia tu wale waliokamilisha malipo yao na kuanza kujifunza.


Washiriki wengi walikuwa na shauku ya kuanza kujadili mada lakini kutokana na admin kuwa na shughuli nyingi muda huo za kuadd majina ya washiriki, ilibidi achelewe kidogo mpaka ilipofika kama saa 1 na nusu hivi jioni ndipo sasa mjadala ukaanza rasmi. Tuliweka kwanza baadhi ya sera za group na tukakubaliana kuwa muda wa kuanza uwe ni saa 3 mpaka saa 4 usiku kwani watu unakuta pilikapilika nyingi zimepungua.

Darasa litaendelea tena leo, ila samahani kama wewe unayesoma hapa siyo mshiriki, utanisamehe kwani siwezi kutaja chochote kuhusiana na mada, mchanganuo wa mwezi tuliowasilisha au hata yaliyomo kwenye masomo hayo kwa undani, maswala hayo yote ukipenda kuyapata bila chenga njia rahisi ni kujiunga na darasa.

Kama umechelewa kuanza huna sababu ya kuwa na wasiwasi kwani, vitu vyote muhimu utavikuta katika blogu yetu ya ‘private’, utakuta downloads zote hapo na nyingine unatumiwa moja kwa moja katika email au wassap.


Unapojiunga unapata vitu vingi kwa gharama kidogo ukilinganisha na mafunzo yeyote ya ujasiriamali yanayotolewa hapa Tanzania kupitia hii mitandao ya kijamii. Kwa shilingi elfu 10 tu unapata vitu vifuatavyo;

1.  Masomo ya semina, jinsi ya kuandaa michanganuo, michaganuo bunifu yenye uwezo mkubwa wa kuboresha mzunguko wa fedha pamoja na chochote kile kuhusiana na ujasiriamali/biashara mshiriki atakachowasilisha.

2.  Michanganuo  bunifu 12  ya kila mwezi katika mwaka wote wa 2018

3.  Kitabu cha jinsi ya kuandika mpango wa biashara cha Kiswahili(softcopy)

4.  Kitabu mashuhuri zaidi cha jinsi ya kuandaa mpango wa biashara cha kiingereza kinachoaminiwa katika vyuo vingi duniani(softcopy)

5.  Templates(vielezo) unavyoweza kutumia katika uandaaji mpango wako kwa urahisi na haraka zaidi, unajaza tu maneno yako.

6.  Michanganuo(Samples) ya Kiswahili na kiingereza unayoweza kuitumia kama mifano wakati ukijifunza kuandika wakwako.

7.  Masomo au semina zopte zilizopita kwenye blogu yetu ya private pamoja na material mbalimbali unazoweza kudownload hapo free.

8.  Fursa ya kushiriki mafunzo mengine yote kwa mwaka wote huu wa 2018 bila kulipa gharama yeyote ile ya ziada.

Zana hizi 8 unakabidhiwa pindi tu umalizapo kutimiza taratibu za kujiunga, Ikiwa wewe ulishawahi kujiunga na semina zetu siku zilizopita, tafadhali tujulishe tukuunganishe kwani wewe tayari una sifa zote za kuingia katika mafunzo haya na hautalipa tena kiingilio kingine.


Mwisho nikukaribishe sana leo, njoo tujifunze pamoja saa 3 usiku pale ‘MICHANGANUONI ONLINE’, WHATSAPP: 0765553030

SIMU: 0712202244

Peter Augustino Tarimo.

0 Response to "UZINDUZI WA SEMINA YA MIPANGO YA BIASHARA BUNIFU 2017 ULIVYOFANA MTANDAONI"

Post a Comment