UAMUZI HATARI WA KUSHANGAZA ULIO CHANZO CHA UHURU WA TAIFA LA MAREKANI | JIFUNZE UJASIRIAMALI

UAMUZI HATARI WA KUSHANGAZA ULIO CHANZO CHA UHURU WA TAIFA LA MAREKANI

Wakoloni walichukia watu wenye silaha kuandamana mbele yao. Watu walianza kuonyesha chuki yao wazi, wakivurumisha mawe pamoja na maneno kwa wanajeshi waliokuwa wakitembea, mpaka ofisa mwenye amri alipoamrisha, “Kaza singe…..Chomeka!

Mapambano yalianza. Yalizaa vifo na majeruhi wengi. Tukio liliamsha chuki kiasi kwamba Baraza la jimbo(lililoundwa na wakoloni mashuhuri) liliitisha mkutano kwa lengo la kuchukua hatua madhubuti zinazostahili. Wawili kati ya wanachama wa Baraza hilo walikuwa ni John Hancock na Samuel Adams. Walizungumza kwa ujasiri na kutangaza kwamba hatua ni lazima ichukuliwe kuondoa wanajeshi wote wa Uingereza kutoka Boston.

Kumbuka huu- uamuzi, katika akili ya watu wawili, ungeweza vizuri kuitwa mwanzo wa uhuru ambao Wamarekani sasa wanaufurahia. Kumbuka pia kwamba uamuzi wa watu hawa wawili ulihitaji imani na ujasiri, kwasababu ulikuwa hatari.

Kabla ya Baraza kuahirishwa, Samuel Adams alichaguliwa kumuona Gavana wa jimbo, Huchinson, na kutaka kuondolewa kwa vikosi vya majeshi ya Uingereza. Ombi lilikubaliwa na vikosi viliondolewa kutoka Boston, lakini tukio halikufikia tamati. Lilikuwa linasababisha hali iliyotaka kubadilisha mwenendo mzima wa ustaarabu.

Ajabu, siyo kwamba ni ukubwa kiasi gani wa mabadiliko kama yale ya Mapinduzi ya Marekani na vita vingine vingi mara kwa mara vilivyo na mianzo yao katika mazingira yanayoonekana kuwa siyo muhimu?. Inavutia pia kuona kwamba mabadiliko haya muhimu mara nyingi huanza katika hali ya uamuzi dhahiri katika akili za idadi ndogo sana ya watu.

Wachache wetu tunafahamu historia ya Marekani vizuri vyakutosha kutambua kwamba John Hancock, Samuel Adams na Richard Henry Lee(wa jimbo la Virginia) walikuwa mababa wa kweli wan chi.

Richard Henry Lee alikuwa kigezo muhimu katika simulizi hii kutokana na sababu kwamba yeye na Samuel Adams waliwasiliana mara kwa mara(kwa maandishi), walibadilishana kwa uhuru, wasiwasi na matumaini yao kuhusiana na masilahi ya watu wa jimbo lao. Kutokana na kitendo hiki, Adams alipata wazo kuwa mabadilishano ya pamoja ya barua kati ya makoloni 13 yanaweza kusaidia kuleta uratibu wa nguvu iliyohitajika sana kuhusiana na suluhisho la matatizo yao.

Mnamo Machi 1772, miaka miwili baada ya makabiliano na wanajeshi Boston, Adams aliliwasilisha wazo hili  kwenye baraza katika mfumo wa hoja kwamba kamati ya Uhusiano ianzishwe ikiwa na wajumbe kamili waliochaguliwa katika kila koloni “kwa lengo la ushirikiano wa kirafiki kwa manufaa ya makoloni ya Uingereza Marekani”

Zingatia vizuri tukio hili! Ulikuwa ni mwanzo wa muungano wa nguvu kubwa sana iliyohitajika kutoa uhuru kwa Wamarekani. Ushirika tayari ulikuwa umekwishaundwa, ulimjumuisha Adams, Lee na Hancock. Kamati ya Mahusiano iliundwa. Shuhudia kwamba kitendo hiki kilitoa njia ya kuongeza nguvu ya ushirika kwa kuongeza watu kutoka makoloni yote. Zingatia kwamba utaratibu huu ulibeba mpango madhubuti wa kwanza kabisa wa wakoloni waliokuwa wamegadhabika

Katika Umoja kuna nguvu! Wananchi wa Makoloni  walikuwa wamepigana vita isiyokuwa rasmi dhidi ya Wanajeshi wa Uingereza kupitia matukio yanayofanana na maandamano ya Boston lakini hakukuwa na la maana lililotimizwa. Malalamiko yao mmojammoja hayakuwa yameunganishwa chini ya ushirika mmoja. Hakukuwa na kundi la watu walioweka mioyo yao, akili, roho na mwili pamoja katika uamuzi mmoja kamili kusuluhisha matatizo yao na Waingereza mara moja na daima, mpaka pale Adams, Hancock na Lee walipokuja kukaa pamoja.

Wakati huohuo Waingereza hawakuwa wamekaa kimya, wao pia walikuwa wakipanga mipango na kushirikiana katika mambo yao wenyewe wakiwa na faida ya kuwa na pesa pamoja na jeshi thabiti nyuma yao.

Ufalme ulimteua Gage kuchukua nafasi ya Hutchinson kama Gavana wa Massachusetts. Moja kati ya vitendo vya mwanzo vya Gavana ilikuwa ni kutuma ujumbe kumwambia Samuel Adams kwa lengo la kujaribu kuzima upinzani wake kwa hofu. Tunaweza kuelewa vizuri zaidi kiini cha kile kilichotokea kwa kunukuu mazungumzo kati ya Kanali Fenton(mjumbe aliyetumwa na Gage) na Adams.

Kanali Fenton: ‘Nimeruhusiwa na Gavana Gage kukuhakikishia wewe  Bwana Adams, kwamba Gavana amepewa uwezo wa kukutunukia zawadi kadiri itakavyofaa(akijaribu kumshawishi Adams kwa ahadi ya hongo) kwa masharti kwamba  uingie katika kuzima upinzani wako kwa amri za serikali. Ni ushauri wa Gavana kwako Bwana, kutokusababisha maudhi zaidi kwa Mheshimiwa. Mwenendo wako unakufanya uwajibike kwa adhabu za kuvunja sheria ya Mfalme Henry viii, ambayo mtu anaweza kupelekwa Uingereza kwa mashitaka ya Uhaini au kuficha kosa la uhaini kwa mamlaka ya Gavana wa jimbo. Lakini kwa kubadilisha muelekeo wako kisiasa, siyo tu utapata faida kubwa binafsi, lakini utatengeneza amani yako na mfalme!”

Samuel Adams alikuwa na uchaguzi wa maamuzi mawili, angeweza kusitisha upinzani wake na kupata hongo binafsi, au angeliweza kuendelea na kuwa katika hatari ya kunyongwa!

Ukweli, muda ulikuwa umefika wa Adams kulazimika kufikia mara moja uamuzi ambao ungeweza kuyagharimu maisha yake. Wengi wa watu wangeliweza kuona ni vigumu kufikia uamuzi wa namna hiyo. Wengi wangeweza kurudisha jibu la kukwepakwepa, lakini siyo Adams! Alimsisitizia Kanali Fenton kumfikishia Gavana jibu kamili kama Adams alivyolitoa kwake.


Jibu la Adams lilikuwa hivi; ‘Hivyo unaweza kumwambia Gavana Gage kuwa natumaini ni muda mrefu tangu nifanye amani yangu na Mfalme wa Wafalme. Hakuna sababu binafsi zitakazonisukuma mimi kuachana na mkondo wa maadili ya nchi yangu. Na mwambie Gavana Gage ni ushauri wa Samuel Adams kwake, aache kutukana hisia za watu waliogadhabishwa.’


Mpenzi msomaji, usikose sehemu ya 3 ya sura hii ya 8 siku ya Jumatatu, pia zile semina za michanganuo ya biashara bunifu kwa mwaka huu zinaanza rasmi kesho Ijumaa katika darasa letu la mtandaoni kupitia Blogu maalumu, email na Whatsapp, ikiwa bado hujatuma namba yako ya wassap fanya hivyo hujachelewa, usisahau pia kutoa ada yako sh. 10,000/=. Namba zetu ni 0712202244  Whatsapp,  0765553030





0 Response to "UAMUZI HATARI WA KUSHANGAZA ULIO CHANZO CHA UHURU WA TAIFA LA MAREKANI"

Post a Comment