SOMO LA 7: TATHMINI YA SOKO | JIFUNZE UJASIRIAMALI

SOMO LA 7: TATHMINI YA SOKO


Tathmini ya soko imegawanyika katika vipengele vidogo kadhaa ambavyo vyote ili uweze kuviandika unahitaji kupata takwimu na taarifa mbalimbali nje ya biashara yako zinazohusiana na soko au wateja watarajiwa, sekta ya biashara uliyopo pamoja na ushindani.

Taarifa hizi na takwinu mbalimbali utaweza kuzipata kupitia kufanya utafiti wa soko ambao unaweza kwenda moja kwa moja kuwauliza wateja wanaonunua bidhaa/huduma kama unazotarajia kuuza au kwa njia ya machapisho mbalimbali kutoka taasisi na vyombo vya habari kama vile majarida, mtandao wa intaneti, maktaba, vituo vya kuwasaidia wajasiriamali, wizara za serikali kama Wizara ya viwanda na biashara, ofisi au tovuti ya takwimu ya Taifa nk.

Kwenye utafiti wako wa soko hakikisha unawajua vizuri wateja wako, fahamu idadi yao na unaweza kujua idadi hiyo kwa kuangalia katika takwimu mbalimbali kama za sensa ya watu na makazi au ofisi za serikali za mitaa kama katika eneo lako kuna idadi ya watu wangapi, au kuna biashara ngapi ambazo ndizo unategemea kuwa soko lako nk. Kwa mfano ikiwa wewe biashara yako unatarajia kusambaza vifaa vya usafi mahospitalini na mashuleni, nenda kaulize katika eneo hilo kuna jumla ya mashule na mahospitali mangapi?

Mbali na kufahamu idadi ya wateja wako pia utatakiwa kufahamu mahitaji yao na ni kigezo kipi kinachowafanya wanunue. Ikiwa ni mteja mmoja mmoja basi fahamu wastani wa umri wao, kipato chao, idadi ya wanafamilia, na tabia zao za manunuzi zinazohusiana na biashara yako. Na taarifa kama hizi unaweza kuzipata aidha kwa kuuliza watu moja kwa moja mitaani au kwa kutumia machapisho na taarifa mbalimbali kama za sensa ya watu na makazin nk. Utafiti wa soko umefafanuliwa vizuri kwenye kitabu cha Michanganuo ya biashara na ujasiriamali uk. wa 20

Vipengele vidogo kwenye sehemu hii ya Soko ni hivi vifuatavyo;

4.1 Mgawanyo wa soko
4.2 Mkakati wa soko lengwa
4.2.1 Mahitaji ya soko
4.2.2 Mwelekeo wa soko
4.2.3 Ukuaji wa soko
4.3 Tathmini ya sekta
4.3.1Washiriki katika sekta
4.3.2 Usambazaji ulivyo
4.3.3 Vigezo vya ushindani
4.3.4 Washindani wakuu

Ngugu msomaji wa blogu hii huu ni utangulizi tu wa somo lenyewe la 7, ukitaka kusoma somo zima na masomo mengine yote 10, jiunge na darasa hili la semina ya kuandika mpango wa biashara kwa kulipa shilingi elfu 10 kupitia namba 0712202244  au 0765 553030 jina ni “Peter Augustino” kisha tuma na email yako ili kuunganishwa na blogu hii ya semina hapa.

Ili kufahamu huduma nyingine tunazotoa fungua ukurasa huu hapa.









0 Response to "SOMO LA 7: TATHMINI YA SOKO "

Post a Comment