SURA YA TATU, THINK AND GROW RICH KWA UFUPI, IMANI NDOTO NA KUJIAMINI. | JIFUNZE UJASIRIAMALI

SURA YA TATU, THINK AND GROW RICH KWA UFUPI, IMANI NDOTO NA KUJIAMINI.

Sura ya 3.
Hatua ya 2 Kuelekea mafanikio.
Akili ya binadamu (mind) imegawanyika katika sehemu mbili, upande mmoja unahusika na mawazo au hisia za ndani (Subconcious mind) na wa pili (conscious mind) eneo linalohusika na hisia za kawaida zinazotokana na ile milango mitano ya fahamu yaani, masikio, pua, macho, ngozi na ulimi. Mawazo  ya  ndani kazi yake ni kupokea  taarifa  kutoka mawazo  ya nje na kuzifanyia kazi. Taarifa hizo  zinapokaa muda mrefu  ndani ya mawazo ya ndani ndipo hutafsiriwa kuwa kitu halisi, kwa mfano ukiwaza kupata kitu fulani, ukanuwia kwa muda mrefu matokeo yake mawazo ya ndani yatakufanya kila unachokifanya uelekeze nguvu katika  kutimiza lengo hilo na hatima yake jambo hilo hutokea kuwa kweli. Ukinuwia kuumwa ugonjwa fulani, hutokea kuwa kweli, ukinuwia kuwa  iko  siku utaua, uwezekano wa kuja kuua mtu kweli huwa mkubwa nk.

Na hiki  ndicho hutokea katika imani zote duniani, iwe ni za dini au mila hata uchawi. Kuna nguvu isiyoshikika yenye uwezo wa kuwasiliana  na akili ya ndani  kwa kila mwanadamu, nguvu hiyo kuu wengi husema ndiyo Mungu na wengine hudai ni nguvu  tu isiyokuwa ya kawaida.(Super Natural Force)

Kwa hiyo katika akili zetu haijalishi ni mawazo ya aina gani, mazuri au mabaya tunayofikiri, yanaporudiwa rudiwa na kukaa muda mrefu akilini matokeo yake hutengeneza kitu halisi. Hivyo unaweza ukanufaika kwa kuingiza  akilini mwako mawazo mazuri kama ya kujipatia utajiri na mwishowe ukatajirika kweli. Ndiyo mana  katika sura hii mwandishi anashauri kuwa  unapokuwa na wazo lolote la kupata utajiri au mpango, basi andika mahali na kisha uwe unafanya  marudio kila mara kwa sauti mpaka mawimbi ya sauti hiyo yatakapofikia katika akili yako ya ndani.

Ushahidi wa suala hili la imani unaweza ukaupata kutoka  maeneo  mengi, kwa  mfano watu mashuhuri kama  Mahatna Ghandi wa India, hakuwa  na chochote zaidi ya imani ambayo mwishowe ilimfanya kuwa rais wa Taifa hilo, Yesu Kristo kwa imani aliamuru maji ya bahari kupisha watu wakatembea juu yake. Mtume  Muhamad aliweza, kwa imani kuwaunganisha mamilioni ya watu kumfuata na inasema kama pia huko  Mashariki ya mbali  wapo watu wenye imani ya Kibudha walio na uwezo wa kupasua vitu vigumu ajabu kwa kutumia vichwa vyao. Hii yote ni kutokana na Imani.


>>>Bofya kuendelea mbele>>>                   


>>>Bofya kurudi nyuma<<<<<                              

0 Response to "SURA YA TATU, THINK AND GROW RICH KWA UFUPI, IMANI NDOTO NA KUJIAMINI."

Post a Comment