ILE CHANJO YA KWANZA YA MALARIA SASA IMEKAMILIKA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

ILE CHANJO YA KWANZA YA MALARIA SASA IMEKAMILIKA

Chanjo ya kwanza dhidi ya Malaria duniani iko mbioni kuidhinishwa kwa ajili ya matumizi barani Afrika.
Shirika la Dawa barani Ulaya, limetoa matumaini hayo baada ya kutathimini usalama wake na uwezo wake wa kufanya kazi
Shirika la Afya duniani,WHO linatazamia kuidhinisha chanjo hii kutumika kwa watoto, ambao miongoni mwao chanjo hiyoilileta majibu ya mchanganyiko.
Ugonjwa wa Malaria huua watu takriban 584,000 kwa mwaka dunia nzima, wengi wao watoto wa umri wa chini ya miaka mitano kusini mwa jangwa la Sahara.

Ndoto yawa kweli
chanjo iitwayo Mosquirix, au RTS,S ni ya kwanza dhidi ya vijidudu vinavyosababisha malaria kwa binadamu.
Daktari Ripley Ballou, ni mtafiti toka Kampuni ya Glaxo Smith Kline vaccines anasema huu ni wakati mzuri, amekuwa akifanyia kazi Chanjo hii kwa miaka 30, anasema ndoto imetimia.
Kampuni hiyo haijaweka wazi gharama ya chanjo, lakini imeahidi kutopata faida kutokana na chanjo hiyo.
Chanjo hii imetengenezwa mahususi kupambana na malaria kwa watoto barani Afrika na haitaruhusiwa kutumika kwa wasafiri.
Watoto kati ya miaka mitano mpaka 17 wamekusudiwa kwenye chanjo hii, ambapo walipatiwa chanjo tofauti aina tatu katika kipindi cha mwezi mmoja kisha dawa ya chanjo nyingine katika kipindi cha miezi 20.
Katika kundi hili, watafiti walifanikiwa kupunguza athari za ugonjwa huu kwa theluthi moja kwa kipindi cha miaka minne.
Bila dawa ya kuongezea nguvu chanjo isingeweza kupambana na malaria kwa kipindi hicho cha majaribio.
changamoto iliyoonekana ni kuwa chanjo hiyo haikuonyesha uwezo wake wa kuwakinga watoto wachanga dhidi ya malaria.
Hali hii inaiweka WHO katika njia panda, shirika hilo litaamua mwezi Oktoba kuwa chanjo hiyo itumike au la, kwa sababu haikuwa na mafanikio makubwa kama ambavyo wanasayansi walitegemea.

CHANZO CHA HABARI HII NI BBC SWAHILI


0 Response to "ILE CHANJO YA KWANZA YA MALARIA SASA IMEKAMILIKA"

Post a Comment