HATARI! BINADAMU BANDIA WA KUTENGENEZWA KUCHUKUA MAHALI PA BINADAMU WA KAWAIDA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

HATARI! BINADAMU BANDIA WA KUTENGENEZWA KUCHUKUA MAHALI PA BINADAMU WA KAWAIDA

Mwanasayansi mashuhuri nchini Uingereza ‘Stephen Hawking’ ameonya kwamba juhudi zinazoendelea za kuunda ‘roboti’, mashine inayofikiria a kutenda kama binadamu zinaweza zikasababisha maafa makubwa kwa kizazi cha binadamu siku za usoni na kusababisha kutoweka kwake.
Stephen Hawking
Alikuwa akijibu swali aliloulizwa juu ya mashine yake yenye uwezo wa kujibu maswali kama binadamu na iliyotengenezwa kwa teknolojia msingi katika kuunda binadamu huyo wa bandia mwenye uwezo sawa au hata kushinda ule wa binadamu wa kawaida. Teknolojia hiyo tayari imekwishaanza kutumiwa kwa watu waliokuwa na magonjwa yanayohusisha matatizo katika kuzungumza.

Alisema kuwa binadamu kamili wa bandia ataweza kuwa ametengenezwa miongo michache ijayo kutoka sasa na hatua zilizokwisha pigwa mpaka sasa zimethibitika kuwa na mafanikio makubwa, ila tu ni kwamba haijajulikana dhahiri endapo binadamu huyo ikiwa atakuwa na akili kutuzidi ataleta maafa makubwa kwa binadamu wa kawaida ama ataleta faida chanya.


Watu wengine wameanza kuingiwa na wasiwasi juu ya kazi zinazofanywa na binadamu mahali pake kuchukuliwa na “wanadamu hao wapya” wenye akili kupindukia.
Hata katika sekta ya 'malavidavi' pia watatumika, ukimwi  byebye!

Profesa Hawking pia alizungumzia faida na hasara za matumizi ya mtandao wa Intaneti, akionya intaneti kugeuka kuwa kituo kikuu cha Magaidi kutoa maelekezo ‘command centre for terrorists’. Alisema juhudi za makusudi zinafaa zichukuliwe na makampuni ya intaneti kuzuia kitisho cha magaidi hao lakini ugumu unabakia kuwa ni vipi itawezekana pasipo kuweka rehani uhuru wa kujieleza pamoja na faragha.

chanzo bbc

0 Response to "HATARI! BINADAMU BANDIA WA KUTENGENEZWA KUCHUKUA MAHALI PA BINADAMU WA KAWAIDA"

Post a Comment