MTU WA SITA MZEE KULIKO WOTE DUNIANI AFIA HOSPITALI ALIYOFIA BABA WA TAIFA MWALIMU NYERERE, AMEISHI NA KUSHUHUDIA KARNE ZOTE 3 | JIFUNZE UJASIRIAMALI

MTU WA SITA MZEE KULIKO WOTE DUNIANI AFIA HOSPITALI ALIYOFIA BABA WA TAIFA MWALIMU NYERERE, AMEISHI NA KUSHUHUDIA KARNE ZOTE 3

Bi Jone katikati
Mwanamke, aliyezaliwa mwaka 1899 tarehe 7 Disemba, karne ya 19, Miss Jones amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 113. Aliishi katika jiji la London kitongoji kiitwacho Bermondsey, na alikuwa akishikilia namba sita katika orodha ya watu wenye umri mkubwa zaidi wanaoishi duniani kwa sasa. Baada ya afya yake kuanza kudorora siku za hivi karibuni alilazwa katika Hospitali ya St.Thomas  ambayo ndiyo hospitali alikolazwa Baba wa Taifa la Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerre kabla hajafariki dunia hapo mwaka 1999.


Jirani yake mmoja aitwaye Hughes anasimulia kwamba, hadi kifo chake Bi Jones alikuwa na akili timamu tena hakuonyesha kabisa kuhofia kifo na anasema pia kwamba alishiriki katika vita kuu ya 1 ya Dunia na mchumba wake alikufa akiwa anahudumu katika vita hiyo. Alikuwa akiishi ghorofani katika chumba chake mwenyewe na mpaka siku za hivi karibuni alikuwa akifanya shopping mwenyewe sokoni.


Majirani zake wote na marafiki wanaelezea kusikitishwa sana na kifo chake na wanasema kamwe hawatamsahau. Kifo cha Bi Jones kina maanisha kwamba kwa sasa mtu mzee kuliko wote nchini Uingereza ni Ethel Lang kutoka Barnsley aliyezaliwa mwezi  wa 5 mwaka 1900. Ina maana kwamba Bi Jones ni mtu wa mwisho aliyezaliwa miaka ya 1800 au karne ya 19 kufariki dunia. Alizaliwa Karne ya 19, akaishi Karne ya 20 na amefariki Karne ya 21. Mungu ailaze roho yake Mahala pema peponi Amen.

0 Response to "MTU WA SITA MZEE KULIKO WOTE DUNIANI AFIA HOSPITALI ALIYOFIA BABA WA TAIFA MWALIMU NYERERE, AMEISHI NA KUSHUHUDIA KARNE ZOTE 3 "

Post a Comment