KIMBUNGA YOLANDA (HAIYAN) NI KAMA MWISHO WA DUNIA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

KIMBUNGA YOLANDA (HAIYAN) NI KAMA MWISHO WA DUNIA

Manusura wa Tufani  kubwa na ambalo halijawahi kutokea katika historia ya visiwa vya Ufillipino, Haiyan au ‘Yolanda’ kama wenyeji wanavyoiita, wameilinganisha tufani hiyo na mwisho wa Dunia.


Kimbunga hicho kilichosababisha uharibifu wa kutisha tayari kinahofiwa kuangamiza maisha ya watu wapatao elfu kumi, wengi wakiwa ni wakazi wa mji mmoja peke yake uitwao Tacloban.


Kwa mujibu wa shirika la habari la BBC, majengo yote yameharibiwa vibaya, matope yametapakaa kila kona, na harufu mbaya ya miili ya watu na mifugo iliyooza ndiyo iliyotawala.

Tayari Rais wa visiwa hivyo Benigno Aquino ametangaza hali ya dharura huku akiiomba jumuiya ya Kimataifa kuwasaidia ili wahanga ambao hawana chochote waweze angalao kupata maji chakula na malazi.

Wakati huo huo huko Nchini Somalia katika jimbo la Puntland inaarifiwa kuwa watu wapatao mia moja wamekufa kutokana na gharika iliyopiga huko mwishoni mwa wiki. 

0 Response to "KIMBUNGA YOLANDA (HAIYAN) NI KAMA MWISHO WA DUNIA"

Post a Comment