NJIA 10 ZA KUHAMASIKA NA KUENDELEA KUBAKIA NA HAMASA HIYO KWA MUDA MREFU UJAO | JIFUNZE UJASIRIAMALI

NJIA 10 ZA KUHAMASIKA NA KUENDELEA KUBAKIA NA HAMASA HIYO KWA MUDA MREFU UJAO

HAMASA, HAMASIKA DAIMA
Hamasa binafsi ndani ya mtu ni jambo la msingi sana katika kuleta mafanikio na maendeleo binafsi. Ikiwa mtu atakosa ama kupoteza  hamasa inakuwa rahisi kujikuta akishindwa kuutumia vizuri muda wake kitu ambacho ndicho chenye thamani kubwa kushinda kila kitu. Ukishashindwa kutumia muda wako kikamilifu ni dhahiri kabisa kuwa utashindwa pia kutimiza malengo yako binafsi pamoja na yale ya kibiashara au kazi.

Kuna nyakati binadamu huwa tunajikuta katika wakati mgumu wa kupoteza hamasa(lose attitude) na hutokea siyo kwa kundi moja tu la watu bali kwa kila mtu hata na wale watu wanaodhaniwa kuwa ni wenye hamasa kubwa, waliofanikiwa au walio na malengo makubwa maishani, lakini hutumia mbinu mbalimbali zinazowawezesha kurudi tena kwenye mstari kwa kupandisha viwango vyao vya hamasa kuwa juu mbinu kama hizi tunazokwenda kuziona hapa chini sasa hivi;

1. Jikumbushe malengo uliyojiwekea mara kwa mara.
Kitu cha kwanza kabisa wakati  unapokuwa ukijiwekea malengo yako yawe ni ya muda mfupi ama ni ya muda mrefu, hakikisha malengo hayo ni halisi kusudi usije ukavunjika moyo pindi pale malengo yako kwa bahati mbaya yatakapokataa kutimia kama ulivyoyapanga. Kila wakati pima ni kiasi gani umetimiza malengo yako na hakikisha malengo yako yanakupa changamoto, ikiwa hayakupi changamoto yeyote basi ujue hayo siyo malengo. Kupima, malengo yako kila mara na kuona maendeleo yake kutaifanya hamasa yako kubakia kuwa juu muda wote kwa kipindi kirefu. Pima malengo yako kwa siku, wiki nk.
2.Hakikisha unajipa zawadi.
Unapotimiza malengo yako, tuseme uliyojiwekea labda kwa siku, wiki au hata kwa mwezi, jipe motisha au zawadi na zawadi inaweza ikawa ni kitu chochote kile mfano kinywaji, kusikiliza muziki mzuri au hata kula chakula kizuri unachokipenda.

3. Jipe mapumziko.
Baada ya kufanya kazi muda mrefu na kwa nguvu zako zote, jitengee muda wa mapumziko na hili litasaidia sana kurudisha hamasa yako upya kama ilikuwa imeshuka chini.

4. Unapoanguka, amka,  jifunze na kusonga mbele.
Badala ya kuanza kuwaza jinsi ulivyoshindwa kutimiza malengo uliyojiwekea, chukua kushindwa kwako huko kama funzo na uhakikishe  lengo au jukumu linalofuata unalifanya kwa umakini zaidi, likamilishe kabla ya muda uliopanga kusudi muda wa ziada urekebishe lile uliloshindwa kutimiza. Kumbuka kuwa kila binadamu hukosea na kuanguka katika safari yake ya maisha.

5. Pendelea kusoma na kutazama habari na hotuba zinazohamasisha.
Tafuta vipindi kwenye redio au televisheni vinavyohamasisha au DVD na vitabu vya namna hiyo, unaweza pia ukasoma historia za watu mashuhuri wanaokugusa na kukupa hamasa ya maisha katika vitabu, kwenye mitandao au kwingineko kokote kule.

6. Jiepushe kabisa na mambo yanayoingilia ratiba zako(vidakizi).
Baini vidakizi vyote na uviondoe mara moja au kuviweka mbali na wewe. Unaweza kuuza, kuhifadhi au hata kukitupa kitu chochote unachohisi kinaingilia ratiba zako na kukufanya ushindwe kutimiza malengo yako kwa wakati. Vitu kwa mfano redio, tv, simu, magazeti nk.

7. Jiwajibishe mwenyewe kwa kukosa kutimiza yale unayojipangia kufanya.
Unaweza ukajiwekea adhabu mbalimbali kama vile, kujinyima vitu unavyopendelea, kuwajulisha ndugu jamaa na marafiki juu ya mambo unayopanga kuyafanya, kusudi usipokuja kutimiza wakuchekeau kukusema na hii itakupa motisha wa kutokushindwa tena.

SOMA: Uamuzi mgumu kwako kuchukua ili biashara yako iweze kupenya wakati huu mgumu kiuchumi.

8. Pata kikombe cha kahawa au chai.
Viburudisho ni muhimu lakini chunga sana usije ukageuka mraibu wa caffeineau pombe, tumia kiasi kidogo sana kwa ajili tu ya kukuchangamsha.

9. Fanya mazoezi ya mwili.
Mazoezi hata kwa kiasi kidogo tu yamethibitika kupandisha hamasa ya mtu, kuondoa msongo wa mawazo na kuongeza fikra chanya vitu vinavyochangia kuongeza hamasa .

10. Yagawanye majukumu yako katika vipande vidogovidogo vinavyotekelezeka kiurahisi.
Iwe ni kazi au hata ni tatizo linalohitaji suluhisho, kisaikolojia kuligawa katika mafungu wakati unapolishughulikia kunakufanya uone ni rahisi zaidi kulitekeleza au kulitatua kuliko ungelitekeleza likiwa zima kama lilivyo.


………………………………………………………………………........

Mpenzi msomaji wa makala hii, hakikisha hukosi makala hata moja zinazowekwa katika blogu yako hii, tunajitahidi kukuletea kile kilichokuwa bora kabisa kwa lengo la kubadilisha fikra na mitazamo kutoka ile isiyokuwa na hamasa kubwa kwenda katika ile iliyojaa hamasa na mtazamo chanya wenye tija katika biashara au kazi yeyote ile mtu aifanyayo.

Kwa matokeo bora zaidi ya programu yetu hii, tunashauri pia mtu kusoma vitabu mbalimbali tulivyokuandalia, na siyo lazima usome vile vinavyouzwa kama hali yako kipesa haiko vizuri sana, tunafahamu watu wengi “tunastruggle” shilingi elfu 3, 5 au 10 kwa kweli wakati mwingine ni mtihani kuipata.

Wengi wetu tunapitia huko na wengine tayari walishapitia huko, ndiyo maana tuna vitabu pia bila malipo kama hiki cha SIRINA KANUNI YA KUJIFUNZA ELIMU YA BIASHARA, au hata hiki kingine, MSAHAFU WAMAFANIKIO(Think & Grow Rich) unachoweza ukakisoma bila kulipa chochote ndani ya blogu yako hii.

Ikiwa bajeti yako itaruhusu basi siyo vibaya pia ukajipatia moja kati ya vitabu hivi vitatu vifuatavyo, viwili au hata vyote kwa pamoja kama utapenda;



 BEI Tsh. 20,000/= hardcopy na  10,000/= softcopy kwa email



  BEI:  Tsh. 10,000/= hardcopy na  5,000/= softcopy kwa email




  BEI:  Tsh. 5,000/= hardcopy na  3,000/= softcopy kwa email


Kuona vitabu zaidi na maelezo yake tembelea SMARTBOOKS TANZANIA


1 Response to "NJIA 10 ZA KUHAMASIKA NA KUENDELEA KUBAKIA NA HAMASA HIYO KWA MUDA MREFU UJAO"