HAICHACHI, SEMINA YA MPANGO WA BIASHARA, TUNAWASHUKURU WALE WOTE WALIOSHIRIKI | JIFUNZE UJASIRIAMALI

HAICHACHI, SEMINA YA MPANGO WA BIASHARA, TUNAWASHUKURU WALE WOTE WALIOSHIRIKI

Mwishoni mwa juma lililopita mpaka juzi jumanne, katika blogu yako ya jifunzeujasiriamali tulitangaza kuendesha semina juu ya jinsi ya kuandika mchanganuo wa biashara, semina ambayo ni mfululizo wa semina za mara kwa mara na hii ilikuwa ni awamu ya tatu ya mfululizo huo ambapo tulichanganua mpango wa biashara ya saluni ya kike.Tunashukuru, washiriki walijitokeza wengi na semina ilikuwa ya kufana.

Kwanini tumeiita HAICHACHI SEMINA?
Ni semina isiyochacha kwa maana kwamba, tofauti na semina nyingine zilizozoeleka, hii hata kama ikiwa kwa bahati mbaya hukuweza  kushiriki lakini ulikuwa nayo nia ya kushiriki, basi fursa hiyo bado inakuwepo, masomo ya awamu zote za semina zilizokwisha pita huhifadhiwa katika blogu maalumu wanayoingia washiriki tu peke yao. Vilevile ukishalipia awamu moja ya semina unapata fursa ya kusoma awamu zote za nyuma na zile zitakazofuata, unapata tiketi ya kudumu.

HAICHACHI SEMINA
Pamoja na kwamba semina hii haiwezi kuchacha, lakini utafika wakati itamalizika hivyo haitadumu milele, ni vyema basi kama unaihitaji ukapata tiketi yako mapema kabla semina haijamalizika na kufungwa rasmi kwa ajili ya kuanza semina mpya yenye maudhui tofauti na michanganuo ya biashara.

Kitu kingine kikubwa katika semina hii, ni fursa ya kipekee ya kupata kitabu cha Michanganuo ya biashara na ujasiriamali (softcopy) bila malipo, kitabu hiki ni ofa kwa anayelipia semina lakini ofa yenyewe nayo ni ya muda mfupi tu, muda ukimalizika kitabu kitaendelea kuuzwa peke yake na semina peke yake, hivyo wahi sasa badala ya kulipa shilingi elfu 20 kitabu pamoja na semina utalipa shilingi elfu 10 tu kwa vyote viwili.

………………………………………………………………………

Kwa mahitaji yako ya vitabu mbalimbali hardcopy na Softcopy kutoka self help books Tanzania, tembelea ukurasa huu, SMARTBOOKS RANZANIA.

0 Response to "HAICHACHI, SEMINA YA MPANGO WA BIASHARA, TUNAWASHUKURU WALE WOTE WALIOSHIRIKI"

Post a Comment