BIASHARA 1 YENYE FURSA YA KIPEKEE NCHINI WATU WENGI HAWAJAIGUNDUA BADO | JIFUNZE UJASIRIAMALI

BIASHARA 1 YENYE FURSA YA KIPEKEE NCHINI WATU WENGI HAWAJAIGUNDUA BADO

Biashara/Hazina iliyojificha
Hebu tuache utani jamani, ukiondoa hizi biashara ndogondogo za rejareja, biashara nyingine karibu zote unapokuwa unataka kuzianzisha hakuna mahali mjasiriamali unapoumiza kichwa kama pale unapoanza kufikiria jinsi utakavyopata vifaa(zana) kwa ajili ya kuendesha biashara hiyo. Vifaa huweza kuchukua sehemu kubwa sana ya gharama za kuanzia kiasi kwamba huwawia vigumu sana wajasiriamali hasa wale wadogo ambao ndio kwanza wanaanzisha biashara zao.

Na vifaa mara nyingi ndiyo kitu muhimu kinachosababisha biashara iweze kuingiza pesa vinginevyo hakuna mtiririko wowote ule wa fedha utakaouona katika biashara yako. Hebu fikiria biashara kama ya kuuza soda na maji baridi kama huna friji au friza inakuwaje? Kuuza soda na maji kwa kutumia mabarafu katika deli au ndoo ya kawaida inachosha sana na hakuna ufanisi mzuri. Wateja wengi kwanza wanapendelea vinywaji vilivyopoa vizuri  kwa ubaridi sahihi vikiwa ndani ya friji au friza.

SOMA: Ili kuongeza mauzo ya biashara ya juisi na soda tumia mbinu hizi. 

Umewahi kufikiria kufungua biashara ya steshenary kwa ajili ya kuuza vifaa vya mashuleni na kutoa photocopy? Ni nini kilichokukatishaa tamaa kufungua steshenari? Bila shaka utaniambia ni gharama kubwa za kununulia mashine yenyewe ya fotokopi. Mashine mpya ya kutolea photokopi sijui inaanzia milioni moja na nusu, sijui milioni mbili…., lakini kwa ujumla ni gharama ambazo kwa mtu anayeanza ni nadra sana kumudu.



Biashara ambazo mjasiriamali utahitaji vifaa kwa ajili ya uendeshaji mzuri zipo nyingi sana mbali na steshenary na biashara ya kuuza vinywaji baridi soda na maji . Kuna biashara kama vile; biashara ya kujaza matairi ya magari upepo, biashara ya kuranda na kuuza mbao, biashara ya usafirishaji wa abiria na mizigo, biashara za uokaji wa vitu mbalimbali na mikate, biashara za viwanda mbalimbali mfano, usagishaji na ukoboaji wa nafaka, utengenezaji wa juisi  nk.

SOMA: Jinsi kiwanda kidogo kinavyoweza kukutoa kimaisha na kukufanya tajiri wa kutupa.

Baada ya kuona biashara hizo sasa moja kwa moja hebu tukaifahamu biashara hiyo niliyokuahidi ambayo ni watu wachache mno mpaka sasa hivi hapa Tanzania waliokwishaigundua na wengi wao wala hawajui kama inaweza kuwaletea pesa nyingi ndani ya kipindi kifupi bila changamoto nyingi kama zilivyo biashara nyingine ambazo kila mtu anazifanya.

BIASHARA ILIYO NA FURSA KUBWA TANZANIA AMBAYO WATU WENGI BADO HAWAJAISHITUKIA.

Ikiwa basi kuna mahitaji makubwa kiasi hicho kwa vifaa mbalimbali kwa ajili ya kuanzisha biashara tofautitofauti kama nilivyozitaja baadhi na wajasiriamali wengi hawawezi kumudu gharama, basi kwa upande mwingine kuna fursa kubwa kwa mtu atakayeanzisha biashara ya............................................................................................................ .......................................................................................................................................................................................................................................... SOMO HILI LITAENDELEA KATIKA GROUP LA MICHANGANUOONLINE LEO SAA 3 USIKU TAREHE 14/6/2023 


Mpenzi msomaji na mdau wangu muhimu sana, si nia yangu kukukatishia uhondo ninapoweka baadhi ya makala ‘nusu nusu’ katika blogu hii hasa zile tunazopost kwenye group la wasap la MICHANGANUO-ONLINE, bali nafanya hivi kwa lengo tu la kuweza kukujulisha kuwa katika huduma nzuri tunazojitahidi kukuletea, wakati mwingine kuna watu wanaohitaji kujifunza zaidi na wengine hawapendi, hivyo kwa wale wanaohitaji basi tumeweka ada kidogo ya mwaka sh. 10,000/= kwa ajili ya wao kuonyesha utayari wao. 

Nasema ni gharama kidogo kwani kwa kweli unapolinganisha yale mtu anayoyapata baada ya kujiunga na group letu hili utaona ni sawa na tone dogo tu la maji ndani ya maji mengi. Hata hivyo makala nyingi kwenye blogu hii tunaahidi na tutahakikisha kwamba ni zile za kawaida zinazokuwa kamili pasipo kukatwakatwa.


Makala kama hii ya leo ya BIASHARA ILIYO NA FURSA KUBWA YA KUSHANGAZA unaweza kudhania labda ni porojo au lugha tu ya kuvutia kama yalivyokuwa matangazo mengine mengi mitandaoni lakini ukweli ni kwamba ni fursa ambayo inaweza ikabadilisha maisha ya mtu yeyote yule kama ataamua kuitia katika vitendo bila kuchelewa. 

(Binafsi mimi biashara hii naifananisha na hazina ya vito iliyojificha chini ya ardhi na ambayo bado watu wengi hawajaigundua kama ipo).

Tafadhali wote tukutane kwenye group saa 3 mpaka 4 usiku wa leo tarehe 14/06/2023  kwa wale wote waliokwishajiunga na kwa anayependa kujiunga anaweza kutuma kiingilio chake sh. Elfu 10 kupitia namba, 0712202244  au  0765553030. Unaweza pia kuwasiliana nasi moja kwa moja kwa wasap au ujumbe mfupi wa maneno kupitia 0765553030. Baada ya malipo tuma ujumbe usemao, “NIUNGANISHE NA GROUP LA MICHANGANUO-ONLINE NA OFFA YA VITU 12

Masomo yote yaliyopita tangu kuanza kwa group hili yapo na unapojiunga tunakutumia yote pamoja na OFFA ya vitu 12 iliyo mchanganyiko wa Vitabu na Michanganuo kamili ya Biashara zinazolipa Tanzania.

Unapolipia tu, nasisi tunakutumia kila kitu papo hapo na kukuunganisha na Group la masomo ya fedha. Ikiwa hupendi kujiunga na magroup basi tujulishe tukutumie tu offa zako.

VITU HIVYO 12 VYA OFFA NI HIVI VIFUATAVYO;-

                 1.      COURSE/SEMINA: (compiled complete course) ya Jinsi ya kuandika Mchanganuo wa biashara –(Ukishindwa kuandika mchanganuo wako mwenyewe utarudishiwa pesa zako) - kwa kiswahili

                 2.       KITABU: Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali chenye course zote muhimu za BIASHARA, jinsi ya kuandaa michanganuo ya biashara na sample za michanganuo mbalimbali 10 iliyokamilika kila kitu.kwa kiswahili

                 3.      KITABU: Mifereji 7 ya Pesa na Siri Matajiri wasiyopenda kuitoa -kiswahili

                 4.      KITABU: Siri za upishi wa chapati laini-UPENDO CAFE pamoja na Mchanganuo wake kamili.-kwa kiswahili

                 5.       KITABU: Njia rahisi ya kuandika mpango wa biashara-dakika 30 - kwa kiswahili

                 6.       KITABU: HOW TO WRITE A BUSINESS PLAN  ni maarufu sana duniani na ndio hutumika vyuo vikuu vingi.-kwa kiingereza

                 7.       MCHANGANUO: Kuku wa nyama -Tumaini Broilers - kwa kiswahili

                 8.      MCHANGANUO: Kuku wa nyama –kwa kiingereza

                 9.      MCHANGANUO: Ufyatuaji tofali za saruji- kwa kiswahili

              10.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa Kiswahili

              11.    MCHANGANUO: Mgahawa wa chakula-Jane Restaurant –kwa kiingereza

              12.    MCHANGANUO: Kiwanda cha usagishaji Dona (Usado milling) - kwa Kiswahili

              13.    Kuunganishwa Group la masomo ya kila siku ya fedha na michanganuo mwaka mzima ukitaka. (Mentorship group) (Ni hiyari yako lakini, usipotaka hatukuunganishi)


KARIBU SANA!

Peter Augustino Tarimo

Mtaalamu wa michanganuo ya biashara aina zote

Simu/Whatsap: 0765553030  /  0712202244

0 Response to "BIASHARA 1 YENYE FURSA YA KIPEKEE NCHINI WATU WENGI HAWAJAIGUNDUA BADO"

Post a Comment