MCHANGANUO WA KUANZISHA BIASHARA/KAMPUNI BINAFSI YA ULINZI, NYUKI SECURITY SERVICESS | JIFUNZE UJASIRIAMALI

MCHANGANUO WA KUANZISHA BIASHARA/KAMPUNI BINAFSI YA ULINZI, NYUKI SECURITY SERVICESS


KAMPUNI BINAFSI YA ULINZI
Jinsi ya kuanzisha kampuni ya ulinzi hakuna tofauti na namna biashara nyingine zote zinavyoanzisha isipokuwa tu ni lazima upitie wizara ya Mambo ya ndani au makao makuu ya jeshi la Polisi ili kuwathibitishia uwezo wako uliokuwa nao kimtaji, umiliki wa silaha, na rekodi zako kiusalama kwani wanapendekeza zaidi kuwa na rekodi nzuri kama kutokuwa na rekodi za kutenda uhalifu nk. Pia watendaji wa kampuni inafaa zaidi wawe wamepitia mafunzo ya kijeshi au wastaafu kutoka majeshi mbalimbali na walio na rekodi safi.

Jeshi la Polisi watakapohakikisha una sifa za kupewa kibali cha kuanzisha biashara ya ulinzi binafsi ndipo sasa unaweza kuanza kufanya mambo mengine kama vile kuandaa mpango wa biashara yako utakavyokuwa pamoja na kutafuta walinzi watakaolinda malindo mbalimbali ya wateja. Ni lazima pia uhakikishe umekata leseni, kuwa na namba ya mlipa kodi TIN namba, eneo la ofisi la kudumu kampuni yako ya ulinzi itakapokuwa ikiendeshea shughuli zake pamoja na timu yako ya usimamizi na wafanyakazi.

Katika kitabu cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI, kuna mpango wa biashara ifuatayo ya Ulinzi binafsi iitwayo NYUKI SECURITY SERVICES. Hapa chini ni muhtasari wake ukiangazia yale mambo muhimu tu, mchanganuo wake kamili unapatikana katika kitabu hicho.

KAMPUNI YA ULINZI.
Nyuki  Security Services. 
Muhtasari.
Nyuki Security Services  ni kampuni itakayowahakikisha wateja wake na mali zao ulinzi wa uhakika. Inatarajjia kuanza rasmi mwaka 2013 chini ya   wamiliki wake, bwana  Silas John na William Wambura; wote  wawili ni wastaafu kutoka  Jeshi la ulinzi la Wananchi wa Tanzania TPDF na Polisi katika  vyeo vya Meja  Jenerali na Sajenti.
Kampuni itajihusisha na utoaji wa huduma za ulinzi katika ofisi mbalimbali za mashirika  ya umma na binafsi, maduka ya watu, majumbani na katika shughuli mbalimbali  za mikusanyiko.
Mtaji wa kuanzia  utapatikana kutoka kwa wamilliki wenyewe kwa kutoa jumla ya shilingi milioni 11 pamoja na mkopo wa muda mrefu benki, kiasi cha shilingi milioni 10. Kwa kuanza  watahudumia  jiji la Dar es salaam na baadaye katika mikoa mingine Tanzania. 
Biashara hii inafunguliwa  kipindi muafaka kwani ongezeko la shughuli za kiuchumi hasa kupanuka kwa sekta binafsi na serikali kujiondoa katika biashara  ndio kunazidi kushika kasi. Nyuki watalenga  kundi la ofisi na magodown  ya makampuni binafsi katika juhudi zake za kukamata sehemu kubwa ya soko  la ulinzi katika jiji la Dar es salaam.
Wafanyakazi watakaoajiriwa na Nyuki  watachukuliwa  kutegemeana  na mahitaji yaliyopo tu, hakuna wafanyakazi watakaoajiriwa bila kupewa lindo isipokuwa wale wa akiba  ambao ni watatu tu.
Kampuni inatarajia kupata mauzo mazuri  na faida mwaka wake wa kwanza  na mauzo hayo yataongezeka  mara dufu ifikapo mwaka  wa tatu. Itakapofika mwaka wa tatu kampuni imepanga kukaribisha wabia ikiwa ni juhudi za kuongeza mtaji wake ili iweze kulifikia soko la nje ya mkoa wa Dar es salaam.
1.1 Dhamira kuu.
Nyuki   Security  imedhamiria  kuwahakikishia wateja wake ulinzi wa uhakika pamoja na mali zao kwa kuajiri wafanyakazi walioiva kimafunzo na wenye rekodi nzuri. 
1.2 Malengo  ya  kampuni.
Mafanikio ya kampuni yatategemea kutimizwa kwa malengo yafuatayo;
(i)          Kufikisha mauzo yapatayo shilingi millioni 244 mwaka wa tatu.
(ii)        Kupata wateja wakudumu wapatao 12 ifikapo mwaka 2015.
(iii)       Kuajiri  walinzi wa kudumu wapatao  23 ifikapo mwaka 2015
(iv)      Kupata faida ipatayo shilingi milioni 60 ifikapo  mwaka 2015.
(v)        Kufikisha huduma zetu mikoani tukianza na Morogoro na Pwani kuanzia mwaka 2015
1.3  Siri za mafanikio.
Nyuki pia watahakikisha yafutayo yanatekelezwa katika kuhakikisha mafanikio yanapatikana.
·       Kuajiri wafanyakazi wenye uzoefu na mafunzo ya kutosha.
·       Kuwalipa wafanyakazi mishahara mizuri na kwa wakati.
·       Kuwatembelea wafanyakazi wawapo lindoni(patrol) mara kwa mara kujua matatizo au udhuru, hivyo kubadilishana na wafanyakazi wa akiba.
·       Sare(Yunifomu) kwa kila mlinzi yenye nembo ya kampuni na wakati wote kuhakikisha wanakuwa nadhifu na wakakamavu.
…………………………………………..
Kwa mahitaji ya vitabu kutoka Self Help Books Tanzania tembelea; SMART BOOKSTANZANIA
Semina za michanganuo pia zinaendelea katika group la whatsapp la MICHANGANUO ONLINE, email na blogu ya private karibu tujifunze kwa kina jinsi ya kuchanganua biashara pamoja na mzunguko wa fedha kwenye biashara zetu kila siku saa 3 usiku mpaka saa 4.

SIMU: 0712202244
WHATSAPP: 0765553030

4 Responses to "MCHANGANUO WA KUANZISHA BIASHARA/KAMPUNI BINAFSI YA ULINZI, NYUKI SECURITY SERVICESS"

  1. Je kama haujawahi kupitia jeshi lolote hauruhusiwi kumiliki kampuni ya ulinzi?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Unaruhusiwa ila ni lazima katika timu yako wale key person kuwe na watu waliopita katika majeshi

      Delete