MASOMO YOTE 11 YA SEMINA YAMEKAMILIKA, LINGANISHA THAMANI, UBORA NA BEI | JIFUNZE UJASIRIAMALI

MASOMO YOTE 11 YA SEMINA YAMEKAMILIKA, LINGANISHA THAMANI, UBORA NA BEI

Habari za shughuli ndugu msomaji wa blogu hii, ni matumaini yangu kuwa unaendelea vyema na biashara ama kazi yako popote pale ulipo. Siku chache umeweza kuona watendaji katika blogu yako hii tumekuwa bize sana kiasi ambacho hata utaratibu wetu wa kawaida tumekuwa wakati mwingine tukiuhujumu.

Lakini hii imetokana na kazi kubwa ya kuhakikisha ile semina yetu ya Michanganuo ya biashara tuliyotangaza wiki chache zilizopita inakamilika katika ubora wake na kwa kiwango cha hali ya juu kabisa kusudi kutimiza dhamira yetu ya kuwafanya washiriki waliojiunga na wanaoendelea kujiunga na semina hii kuhitimu semina wakiwa na cheti chao mkononi ambacho ni “document” ya mchanganuo wa biashara watakayoandika wenyewe kwa usaidizi wa karibu wa wakufunzi wa semina.

Sasa hivi tulichogundua ni kwamba Watu hususani Watanzania hawako tayari tena kulipia bidhaa ama huduma zisizoshikika au kuonekana dhahiri kwa macho kutokana na gharama za maisha kuwa juu na fedha kupatikana kwa jasho jingi.Hivyo watu wanapenda thamani ya kutosha kwa kila senti yao wanayoitoa. Kwa maana nyingine watu hawapendi longolongo linapokuja suala la kutoa fedha yao mifukoni, wanahitaji vitu vya ukweli

Sababu hii ndiyo iliyotufanya Self Help tuhakikishe semina hii kwanza inakuwa ya hali ya juu sana na washiriki mbali ya kushiriki semina lakini mwishoni watoke na kitu wanachoweza kukiona ambacho ni ujuzi wa kuandaa mpango wa biashara.

Tumefanya hivyo kwa karibu kila bidhaa ama huduma tunazozitooa, kwa mfano sasa hivi pale juu ya blogu ya jifunzeujasiriamali utaona page ya, HUDUMA ZETU, ambayo tumeorodhesha huduma mbalimbali tunazozitoa. Huduma kama ya ushauri, mtu akishalipia shilingi elfu 5 atapata huduma nyingi ndani ya miezi 6 kulingana na yeye atakavyohitaji, kuna usaidizi katika kuanzisha na kuendeleza blogu, zawadi ya kitabu kipya kinachokaribia kutoka hivi karibuni, ushauri mbalimbali wa biashara ndogo atakaohitaji nk. vyote kwa sh. elfu 5 tu. Hapo utaona kwamba tunatoa thamani kubwa kwa fedha mteja anayoitoa.

Kingine ni vitabu vyetu ambavyo tumekuwa tukiviuza kila siku, gharama ya kitabu kwa mfano MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI, unapolinganisha wingi na umuhimu wa masomo yaliyopo ndani yake na bei ya kitabu kwa kweli utasema, “mbona wanapata hasara?” Na sasa hivi tena unaweza kukipata kitabu hicho mpaka bure kikiwa softcopy baada ya kulipia semina ambapo hii ni ofa ya muda mfupi tu.

Ndugu msomaji wangu, ninaamini sana katika kushughulika kwa kina na jambo moja kwanza(concentration/focus) kabla ya kwenda kwenye jambo jingine kwa ajili ya matokeo mazuri zaidi, hivyo nitawaombeni radhi sana wasomaji ikiwa ratiba zetu za kawaida zitakiukwa kwa muda. Kwa kipindi kama cha wiki 2 hivi mpapa 6 kwa kweli nitakuwa nikishughulika zaidi na semina hii ya michanganuo, hata makala nyingi zitakazoandikwa zitahusiana na semina hiyo kusudi kutimiza ahadi niliyoitoa kwa washiriki.

Washiriki ambao bado hawajajiunga nafasi bado ipo, mfumo wa semina hii haubagui mtu kwa muda anaoingia ingawa ukichelewa sana utakuja kukuta kile kipindi ambacho wakufunzi tulichojitolea kwa hali na mali huku hata tukiacha majukumu mengine muhimu kimemalizika, ni sawa na mtu kuingia ukumbi wa harusi muda wa saa 6 za usiku. Unakuta mambo mazuri yanakaribiaa kuisha na DJ keshaanza kuchoka. Hivyo nakusihi kama Semina hii unaona kuna kitu cha manufaa kwako usisite tuma ada yalo shilingi elfu 10 kwenye namba 0712 202244  au 0765 553030 jina Peter Augustino Tarimo pamoja na anuani yako ya Gmail. Nitakupa link haraka uanze kusoma masomo yako.
………………………………………………………………..................

ØKwa HUDUMA ZETU nyingine mbalimbali bonyeza maandishi hayo.

Ø Sikiliza utambulisho rasmi wa Semina hapa kwa SAUTI(MP3)

Ø Soma hapa, RATIBA YA MASOMO yote.


Ø Soma MASOMO YOTE 11 HAPA



0 Response to "MASOMO YOTE 11 YA SEMINA YAMEKAMILIKA, LINGANISHA THAMANI, UBORA NA BEI"

Post a Comment