JE, WAJUA MSWAKI NI HATARI WAWEZA KUKUUA? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

JE, WAJUA MSWAKI NI HATARI WAWEZA KUKUUA?


Duniani hapa kuna vitu vidogo vidogo na vya kawaida sana kiasi kwamba mtu akikuambia vinaweza vikakatisha uhai wako mara moja inakuwa vigumu sana kuamini. Ni mpaka pale janga hilo lilkukumbe au limkute mtu wako wa karibu kama vile mtoto, kaka, dada shangazi, mjomba nk.


Mimi binafsi sikuwa nalijua hili hapo kabla, mpaka pale mteja wangu mmoja alipokuwa akinunua mswaki. Kila mara anapofika dukani kununua mswaki, huwa nashangaa vile anavyokuwa makini na aina ya mswaki anaotaka, anauliza ikiwa mswaki niliokuwa nao unatoa nyuzinyuzi kirahisi, maana yake ni kwamba huwa anataka kuhakikisha kuwa mswaki anaonunua ni bora na imara usiopukutika kirahisi.

Nilipotaka kujua ni kwa nini anakuwa makini kiasi kile alinieleza kisa kizima, kwa kweli nikabaki “mdomo wazi” kwani sikuamini kabisa alichokuwa akinisimulia;

“Siku moja asubuhi Shangazi yangu alikuwa akipiga mswaki kama kawaida yake, lakini ghafla akasikia kitu kama kiuzi kimeingia katika koo lake la hewa, kikaanza kumpalia. Yeye alidhani kama kawaida kitatulia tu na kutoka chenyewe lakini kumbe haikuwa hivyo, ikabidi apelekwe hospitali teule ya Tumbi ambako alilazwa kwa ajili ya uchunguzi zaidi. Hata operesheni ilikuwa ni vigumu kumfanyia hadi mgonjwa anakata roho” Alimaliza kunisimulia mteja wangu anayejulikana kwa jina la  Sefu.

Inavyosemekana ni kwamba, kitu kidogo sana kama vile ‘unywele’ wa mswaki unapoingia kwenye koo la hewa na kwenda kuganda katika kuta zake inakuwa vigumu sana kwa madaktari kukiondoa pale kwani hata kwa njia ya upasuaji inaweza isiwezekane kutokana na sehemu yenyewe kuwa tete mno (delicate) Hivyo inashauriwa watu kuwa makini siyo na miswaki tu bali hata na vitu vingine vyovyote vile vya jamii ya manyoyanyoya au nywele.

Mwanadada akipiga mswaki.

Hakikisha unaponunua miswaki kwa familia yako, basi angalao uchague ile imara na yenye ubora unaoaminika hata ikiwa bei yake ni kubwa. Ni heri kujikinga kuliko kujitibu”.


Halikadhalika pia inashauriwa na wataalamu wa kinywa kwamba mswaki ukitumiwa baada ya miezi mitatu, basi kiafya ikiwa ni pamoja na kuzuia madhara kama hayo ya kupukuchika kwa mswaki basi ni bora utupwe na kununuliwa mwingine mpya.

*Ndugu msomaji ikiwa unawajali ndugu na jamaa zako, basi usisite kushare nao makala hii katika mitandao ya kijamii au hata kwa kuwaambia tu kwa njia ya mdomo.

0 Response to "JE, WAJUA MSWAKI NI HATARI WAWEZA KUKUUA?"

Post a Comment