BILIONEA NAMBA 1 AFRIKA AWATAKA WAAFRIKA WAKOPE | JIFUNZE UJASIRIAMALI

BILIONEA NAMBA 1 AFRIKA AWATAKA WAAFRIKA WAKOPE

Aliko Dangote
Bilionea anayeongoza kwa utajiri Barani Afrika, Aliko Dangote ameiambia BBC kwamba wajasiriamali kote Barani Afrika wanapaswa kuweka mipango ya kukopa fedha ili kuendeleza biashara na miradi mbalimbali wanayoianzisha. Amezitaka pia serikali kuacha kutegemea uwekezaji kutoka nje.

Akielezea jinsi alivyoanza biashara hapo mwaka 1978, alisema kuwa fedha za mtaji ‘SEED MONEY” alizipata kutoka kwa marehemu babu yake kiasi cha Naira elfu tano za Kinaijeria baada ya kuingia jijini Logos kujaribu kutafuta biashara ya kufanya.

Alisema biashara ilichanganya  harakaharaka kinyume na matarajio yake kiasi kwamba baada tu ya miezi 6 tu aliweza kurejesha kiasi chote cha fedha alizokopeshwa na babu yake. Alianza na biashara ya kuagiza bidhaa chache kwanza ambazo zilikuwa ni sukari, mchele na samaki wabichi hapo  mwaka 1980 na baada ya hapo mtaji uliendelea kukua na kukua zaidi.

Alipoulizwa ni kwa nini hakuingia kwenye biashara ya mafuta wakati huo ambapo ilikuwa inasadikika kuwa ndiyo yenye kutajirisha haraka alisema kwamba, kwa bahati mbaya watu hudhania hivyo lakini kumbe sivyo na yeye binafsi amelithibitisha hilo kwa kutajirika na kuwa mtu tajiri zaidi Barani Afrika kupitia biashara isiyokuwa ya mafuta.


“Mafuta nadhani humfanya mtu kuwa mvivu”  Alimalizia Bilionea huyo mwenye pesa nyingi kushinda matajiri wengine wote barani Afrika.

Msikilize Dangote mwenyewe hapa chini akizungumza ;

1 Response to "BILIONEA NAMBA 1 AFRIKA AWATAKA WAAFRIKA WAKOPE"

  1. Ilike the message from Aliko Dangote that we entrepreneurs must borrow to increase investment regime

    ReplyDelete