Cameron: Serikali ya Assad ina nguvu sasa. | JIFUNZE UJASIRIAMALI

Cameron: Serikali ya Assad ina nguvu sasa.

David Cameron, Waziri Mkuu wa Uingereza, amekiri kuwa Rais Bashar al Assad wa Syria ameimarisha nafasi yake katika miezi ya hivi karibuni.

Akizungumza katika mahojiano ya BBC nchini humo, Waziri Mkuu wa Uingereza amesema, serikali ya Syria hivi sasa imepata nguvu zaidi ikilinganishwa na ilivyokuwa miezi michache iliyopita.

David Cameron hata hivyo amesema kuwa, London bado ina dhamira ya kuyasaidia makundi ya wanamgambo nchini Syria licha ya kutupilia mipango yake ya kuyapa silaha makundi hayo.
Ripoti mbalimbali zinasema kuwa, Waingereza wanapinga sana nchi yao kuwatumia silaha waasi wa Syria.

Nchi za Magharibi ikiwemo Uingereza pamoja na waitifaki wao wengine wa eneo la Mashariki ya Kati wamekuwa wakiyatumia silaha makundi ya kigaidi yanayofanya mauaji ya watu huko Syria kwa zaidi ya miaka miwili sasa.

0 Response to "Cameron: Serikali ya Assad ina nguvu sasa."

Post a Comment