Kitabu mashuhuri cha wakati wote katika tasnia ya elimu
ya fedha na mafanikio, THINK AND GROW RICH kilichoandikwa na mwanamafanikio
Napoleon Hill miaka zaidi ya 80 iliyopita kwa muda mrefu kimekuwa kikichapishwa
hapa katika blogu hii ya jifunzeujasiriamali katika lugha ya Kiswahili kwa
tafsiri ya FIKIRI UTAJIRIKE au MSAHAFU WA MAFANIKIO.
Lakini majuma machache yaliyopita tulibadilisha uamuzi
huo na kuanza kutoa tafsiri hiyo ndani ya Group la WAHATSAP la masomo ya
michanganuo na mzunguko wa fedha la MICHANGANUO ONLINE, group ambalo
kimsingi washiriki wake hujiunga kwa
kulipia kiingilio cha shilingi elfu 10. Baada ya kuchapisha sehemu chache za
kitabu hicho kwenye group hilo, wapenzi wengi wa mfululizo huo waliokuwa
wakifuatilia katika blogu walituma malalamiko yao wakitaka tafsiri hiyo
irudishwe kwenye blogu kiasi cha baadhi yao hata kutoa maneno makali.
Kwa kuwa sisi lengo letu kubwa halipo kwenye faida kama
wapenzi hao wengi walivyodai, kuweka kiingilio au kuuza baadhi ya huduma na
bidhaa kama vitabu lengo kubwa ni kuweza kuzitegemeza huduma hizi tu kwani
zinahitaji gharama mbalimbali ili kuendelea kuwepo hewani. Hata hivyo uogozi na
timu nzima ya jifunzeujasiriamali baada ya kutafakari kwa kina imeamua
kubatilisha uamuzi wake wa kuhamishia Think & Grow Rich kwenda katika Group
la Michanganuo na kurudi kwenye blogu hii kama zamani.
Uamuzi huo umezingatia
kwamba wote, wapenzi wa blogu hii waliopo katika group na hata wale walioko
kwenye utaratibu wetu wa masomo kwa njia ya email, tunawathamini wote na
tusingelipenda hata mmoja kujisikia anabaguliwa. Kwa kuwa wote waliopo katika
group wanaweza kuingia kwenye blogu basi nao wataendelea kufuatilia tafsiri
hiyo kwenye blogu kama kawaida.
ASANTE SANA.
Peter A. Tarimo
Self Help Books Tanzania.
Simu: 0712202244
Wasap: 0765553030
0 Response to "HABARI MUHIMU SANA KUHUSU KILE KITABU MASHUHURI ZAIDI CHA THINK & GROW RICH(FIKIRI UTAJIRIKE)"
Post a Comment