UTAMBULISHO RASMI WA SEMINA YA MICHANGANUO YA BIASHARA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

UTAMBULISHO RASMI WA SEMINA YA MICHANGANUO YA BIASHARA

Utambulisho rasmi wa semina ya michanganuo ya biashara
Utangulizi.
Ndugu msomaji na mfuatiliaji wa makala katika blogu yako hii ya jifunzeujasiriamali, ninayezungumza hapa ni Bwana Peter Augustino, Mhamasishaji mkuu na mwandishi katika blogu yako hii.

Ninayofuraha kubwa kukujulisha kwamba ile semina yetu ya kujifunza jinsi ya kuandika mpango wa biashara sasa imeanza rasmi katika blogu maalumu ya DARASA LA SEMINA YA MICHANGANUO YA BIASHARA. Pia hapa nitakuelezea mambo machache kuhusiana na Semina hiyo, tafadhali nakuomba tuwe pamoja.

Madhumuni ya Semina
Madhumuni makubwa ya kuanzisha semina hii ya kuandaa mpango wa biashara ni kuhakikisha wasomaji wote wanaonunua au waliokwishanunua kitabu chetu cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI wanatimiza lengo lao la kujifunza na kufahamu kwa uhakika kabisa namna ya kuandaa au kuandika mpango wa biashara.

Namna Semina Itakavyoendeshwa.
Masomo ya semina hii ambayo jumla yake ni 11 yatatolewa kwa kupitia mtandao wa intaneti kwa njia tatu, ya kwanza ni kupitia e-mail ambapo masomo yatatumwa moja kwa moja kwenye email ya mshiriki. Njia ya pili ni kwa njia ya sauti(MP3) ambapo masomo yatapatikana katika blogu ya Darasa la semina ya michanganuo ya biashara na mshiriki atapakua masomo hayo. Njia ya tatu masomo yatatolewa katika mtindo wa PDF kwenye blogu hiyo maalum na washiriki pia watapakua ama kudownload masomo wakiwa ndani ya blogu hiyo.

Kwanini tunasema semia hii ni ya kipekee na haijawahi kutokea?
Ndugu msomaji, gharama za semina hii ukilinganisha na faida mshiriki atakazozipata ni ndogo sana kiasi kwamba haijawahi kutokea semina nyingine hapa nchini ya namna hiyo. Hebu fikiria, shilingi elfu 10 tu, unajifunza michanganuo ya biashara kwa kina kabisa sambamba na kupewa bure softcopy ya kitabu cha Michanganuo ya biashara na ujasiriamali. Na ikiwa basi hupendi softcopy unapenda kitabu halisi cha karatasi unaongeza hapo shilingi elfu 10 tu kwa ajili ya uchapaji.

Tunatambua hali ngumu ya kiuchumi iliyokuwepo sasa hivi nchini, lakini nikutoe tu wasiwasi kwa kukuhakikishia kwamba, kamwe hautaweza kuja kujutia fedha yako unayotoa kwa ajili ya semina hii.

Muda wa kutosha wa kuwa karibu na mkufunzi wa semina hii huku ukipewa msaada wowote ule utakaohitaji mpaka umeelewa na kuandika mpango wako mwenyewe wa biashara. Waandaaji tumejitolea kwa hali zote katika kipindi chote cha semina kuhakikisha hakuna mshiriki atakayeachwa nyuma au kushindwa kutimiza lengo lake la kuandika mpango wa biashara. Na zaidi ya yote tutahakikisha mshiriki anapata huduma zitakazopita matazamio yake na gharama aliyotoa.

Muda wa semina
Ndugu Msomaji, tunatambua kujifunza Mchanganuo wa biashara siyo zoezi unaloweza ukalifanya siku moja ndiyo maana hatukuweka ukomo maalumu wa muda tutakaokuhudumia. Mwisho wa idadi ya masomo ni 11, lakini mwisho wa darasa ni pale mshiriki atakapohitimu kwa kuandika mpango wa biashara anayopenda mwenyewe ambao ndiyo cheti cha kuhitimu semina.

Ndugu msomaji wangu, kushiriki semina hii ni rahisi sana, lipia semina kupitia namba ya simu 0712 202244 jina ni Peter Augustino Tarimo, au namba zetu nyingine zilizomo kwenye blogu hii. Kisha tuma kwa meseji anuani yako ya baruapepe ya Gmail ili niweze kukuunganisha na Blogu ya semina ya michanganuo uanze mara moja kujifunza na kuuliza maswali sambamba na kupokea masomo hayo kupitia hiyo email.

Hii siyo semina ya kukosa hata kidogo ikiwa wewe una dhamira ya dhati ya kujifunza michanganuo ya biashara, hii ni fursa pekee na adimu kabisa ambayo unaweza usijekuipata tena, sisemi kwamba hazitatokea tena semina nyingine kama hii hapana, bali hata kama zitatokea basi inawezekana kabisa isije tena kutokea semina  ya namna hii kwa gharama ya chini kiasi hiki ambayo unahakikishiwa kupata kile unachokihitaji katika muda ambao ni uelewa wako utakaoamua.

Wahi wakati huu, wiki mbili mpaka 4 ambazo wakufunzi wako tumeamua kuacha kila kitu ili tukuhudumie wewe kikamilifu. Kipindi hiki kikimalizika japo semina inaweza kuwa bado ipo lakini tutakuwa hatuna tena muda mwingi wa kutosha kama sasa.

Mwisho nakushukuru sana kwa muda wako ulionisikiliza hapa, naamini pia umekuwa ukifuatilia makala zetu katika blogu hii kwa muda mrefu lakini sasa nakusihi, njoo tukuthibitishie kwa vitendo kile tunachokifanya. Mwaka huu hakikisha unarudisha ama kudumisha ukuu wako, #Makeyourselfgreatagain, #jirudishieukuuwakotena



ASANTE SANA NA MUNGU AKUBARIKI    

0 Response to "UTAMBULISHO RASMI WA SEMINA YA MICHANGANUO YA BIASHARA"

Post a Comment