KITABU BABA TAJIRI NA BABA MASIKINI(RICH DAD, POOR DAD) CHA ROBERT KIYOSAKI | JIFUNZE UJASIRIAMALI

KITABU BABA TAJIRI NA BABA MASIKINI(RICH DAD, POOR DAD) CHA ROBERT KIYOSAKI

Mwandshi wa kitabu hiki, Rich Dad Poor Dad bwana Robert Kiyosaki, anaamua kuivalia njuga elimu ya fedha, elimu ambayo kwa miaka mingi sasa duniani kote nahata katika zile nchi zilizoendelea kama Marekani Uingereza na China, imekuwa kamwe haifundishwi mashuleni wala katika vyuo vya kawaida  vya jadi vilivyozoeleka. Hiki ni kitabu cha 3 katika mfululizo wetu wa viatu 300 vya pesa na mafanikio maarufu na vilivyosomwa zaidi duniani.
KITABU CHA RICH DAD POOR DAD( BABA TAJIRI NA BABA MASIKINI)
Kiyosaki anasimulia jinsi alivyokuwa na mababa wawili, baba yake halisi  aliyempa jina la “Baba masikini au Poor Dad” ambaye maisha yake yote alikuwa kutwa kucha katika miezi yote 12 ya mwaka yeye ni kukimbizana na ajira ya mshahara tu iliyomwacha kila wakati akihangaika kulipa madeni yasiyokauka.
Kwa upande mwingine baba yake wa pili, huyu hakuwa baba yake halisi bali alikuwa ni baba wa hiyari na alimpa jina la “Baba tajiri au Rich Dd” Baba huyu sifa yake kubwa alikuwa ni mtu tajiri sana(Milionea) aliyeacha shule(drop out) na kuamua kuwekeza katika vitegauchumi mbalimbali huku akizingatia zaidi elimu ya pesa isiyofundishwa rasmi katika mashule na vyuo vya kawaida.
·     Ni kwa kupitia kwa baba huyu tajiri, Kiyosaki ndipo alipoweza kujifunza na kuiga maarifa adimu sana ya pesa, kama vile;
·     Tofauti iliyopo baina ya rasilimali na madeni(asset & liability)
·     Kile matajiri wanachowafundisha watoto wao kuhusiana na pesa.
·     Ukweli kwamba hata nyumba ya kuishi unayomiliki kumbe siyo rasilimali kwako bali  ni deni!, na
·     Umuhimu wa kufahamu namna ya kuwekeza na elimu ya ujasiriamali kwa ujumla katika kujipatia uhuru kifedha kwenye dunia hii ya utandawazi uliojaa ushindani kila kona.
Maudhui makuu yaliyomo kwenye kitabu hiki kilichojipatia umaarufu mkubwa sana duniani ni kwamba, siri kuu iliyojifichanyuma ya matajiri wote duniani si nyingine bali siku zote matajiri ndio wanaotumikiwa au kufanyiwa kazi na fedha zao wakati masikini wao ndiyo huzitumikia fedha au kuzifanyia fedha kazi.
Ndugu msomaji, hebu kitafute kitabu hiki ukisome ili uweze kuijua elimu hii ya fedha isiyofundishwa mashuleni wala vyuoni, uweze kufahamu jinsi unavyoweza kuzifanya fedha zikutumikie badala ya wewe kuzitumikia.





3 Responses to "KITABU BABA TAJIRI NA BABA MASIKINI(RICH DAD, POOR DAD) CHA ROBERT KIYOSAKI"

  1. So fortunes to keep running over your mind boggling on the web diary. Your online diary presents to me a great deal of fun.. Favorable circumstances with the site.
    Bookzhub

    ReplyDelete
  2. How can I download this book??

    ReplyDelete