MREMBO ANAYECHOMOA MACHO MITHILI YA KINYONGA AU KAMERA YA KUZOOM: UKIMUONA LAZIMA UTOKE MBIO | JIFUNZE UJASIRIAMALI

MREMBO ANAYECHOMOA MACHO MITHILI YA KINYONGA AU KAMERA YA KUZOOM: UKIMUONA LAZIMA UTOKE MBIO

Pichani juu, Mrembo akiwa katika hali ya kawaida kabla hajaanza kuyachomoa macho yake nje na kuyarudisha  tena ndani mithili ya kinyonga.

Chini ni video ya mrembo akionyesha namna anavyoyachomoa macho yake na kuyarudisha tena ndani mithili ya kinyonga au kamera ya 'kuzoom'.





Unakutana na msichana mrembo anayevutia mwenye umbo namba nane, baada ya kukubaliana mnaamua muende mahala pa faragha, halafu mkiwa mnaendelea na mazungumzo ya hapa na pale kabla hata hamjafanya jambo lolote, ghafla mrembo yule anaanza kuyachomoa macho yake dizaidi kama afanyavyo kinyonga ama zile kamera za “kuzoom” out na “kuzoom in”, ukitaka kupata picha kamili ya kile ninachoelezea, download na uitazame video hii hapa chini.

Hebu nieleze ndugu yangu ikiwa ni wewe umekumbwa na mkasa kama huo na haukuwa umekutana tena na mtu wa namna ile katika maisha yako yote huko nyuma ungelichukua hatua gani?. Utafunga mlango utoke nje mbio…., utaanguka chini na kuzimia.……, au utafanya kitu gani? Hebu toa maoni yako hapo chini baada ya kumaliza kuisoma hii habari tafadhali.

Pichani chini ni mrembo katika hatua za mwazo za kuchomoa macho yake nje na kisha kuyarudisha tena ndani.














Pichani chini ni mrembo jicho likiwa limeshamtoka pima.










Kitendo au tuseme kipaji cha kuyachomoa macho nje na kuyarudisha ndani “Eye popping” kwa kimombo siyo cha kawaida sana kwa watu wengi. Hata mtu unapofikiria kufanya hivyo, unashangaa ni vipi inawezekana lakini  Dunia hii imejaa maajabu mengi, kuna watu tena wengi tu wenye uwezo wa kufanya hivyo. Tena wengine wameweza kuufikia uwezo huo ‘simply’ tu kwa kufanya mazoezi kidogokidogo na wala siyo ndumba(uchawi) kama baadhi ya watu wanavyoweza kudhania.

Kitaalamu Madaktari kitendo hiki hukiita “Globe Luxation” Wanasema kwamba mhusika anachofanya ni kuikaza kwa nguvu misuli na  mishipa yake ya damu  iliyoko kati ya macho na kichwa, kitendo ambacho humfanya mhusika kuhisi vibaya lakini kwa kawaida hali hiyo haiwezi ikasababisha madhara ya kudumu.

Mbrazili mmoja aitwaye “Claudio Paulo Pinto” ambaye hapo mwaka 2006 aliwahi kupigania ili awekwe katika kitabu cha kumbukumbu za rekodi za Dunia “Guiness Book of Records” aliwahi kusema kwamba, yeye alianza kufanya mchezo huo tangu alipokuwa na umri wa miaka 9 na wala huwa hasikii maumivu anapoyachomoa na kujarudisha ndani macho yake kama watu wanavyofikiria.
"Claudio Paulo Pinto" kabla na baada ya kuyachomoa macho yake
Hapa ni Pinto akizidi kuyachomoa macho yake nje.
Pinto alikuwa na uwezo wa kuyachomoa macho yake kwa urefu wa milimeta 7 sawa na inchi 0.3 na alidai kuwa  kwa wakati huo alikuwa na uwezo mara mbili ya huo. Hii inamaanisha kwamba ikiwa ni kweli basi  angeweza kumpiku “Kim Goodman” wa Chicago ambaye kwa wakati huo ndiye aliyekuwa akishikilia rekodi ya dunia katika ‘Guiness book’  kwa kuwa na uwezo wa kuyachomoa macho yake  hadi kufikia urefu wa milimeta 11 sawa na inchi (0.43)

Macho kutoka nje ‘dizaini’ hiyo pia kunaweza kusababishwa na magojwa fulani ya macho ambapo miwani maalumu au lensi huhitajika ili mgonjwa aweze kuona vizuri. Yupo jamaa mwingine huko Liverpool nchini Uingereza kwa jina “John Doyle” mwaka huu amewashangaza watu kwa kitendo chake cha kuyachomoa macho. Ameweka hadi video yake kwenye “You Tube” akichomoa macho huku muziki mzuri ukipigwa jambo ambalo limewafanya maelfu ya watu kuvutiwa na video hiyo.
"John Doyle" naye akifanya vitu vyake
"John Doyle" akipimwa urefu macho yake yalipofikia. 
Hebu na wewe mtazame hapo chini na kusikiliza muziki mtamu alioutumia katika video hiyo huku akiyatoa macho yake utadhani kinyonga vile. Amesema anayo matumaini ya kujitengenezea ajira ya uhakika  kupitia kipaji chake hicho cha kuchomoa macho ikiwa ni pamoja na kuvunja rekodi ya dunia ili aingie katika kitabu cha kumbukumbu za ‘Guiness’.



Kama umewahi kuziona zile kamera zenye uwezo wa “kuzoom out” na “kuzoom in”  basi watu hawa macho yao hayana tofauti na hizo kamera. Mwanamke ambaye video yake unaiona ple mwanzoni kabisa mwa hii stori alipoulizwa ni jinsi gani anaweza kufanya vile alijibu mbele ya umati wa watu kwamba anaweza kutokana na kufahamu namna ya ‘kuicontol’ (kuidhibiti) misuli yake ya macho na alipotakiwa kusema  ni muda gani amekuwa akifanya vile alijibu ni miaka 10.



1 Response to "MREMBO ANAYECHOMOA MACHO MITHILI YA KINYONGA AU KAMERA YA KUZOOM: UKIMUONA LAZIMA UTOKE MBIO"

  1. Kweli dunia imejaa maajabu, hata mimi hapo kabla sikuwa nafahamu kabisa kitu hiki mpaka hivi karibuni nilipokutana nacho mtandaoni.

    ReplyDelete