JINSI YA KUANZISHA BIASHARA ITAKAYODUMU MIAKA 100 NA ZAIDI IJAYO | JIFUNZE UJASIRIAMALI

JINSI YA KUANZISHA BIASHARA ITAKAYODUMU MIAKA 100 NA ZAIDI IJAYO

Utajua vipi kama biashara yako itaweza kudumu miaka mingi ijayo, tuseme labda miaka hata mia moja(100) na zaidi? Kuna watu na hasa wa asili ya Bara la Asia utakuta biashara zao walirithi tangu enzi za mababu na mpaka leo hii bado zipo na zitaendelea kuwepo. Siri yao kubwa ni kitu gani?

Mtu yeyote yule anapoanzisha biashara, kichwani mwake ni lazima awe na vitu hivi muhimu vitatu, Dhamira kuu, Malengo na Dira. Vitu hivi ndiyo humuongoza katika mchakato wake huo wa kuanzisha biashara hata ikiwa yeye mwenyewe haelewi kama anavyo kichwani. Na vitu vyote hivi vitatu ni sehemu ya kitu kingine kikubwa zaidi kinachoitwa, MPANGO WA BIASHARA.

SOMA: Mpango wa biashara unavyoweza kuongeza mafanikio ya biashara yako.

Unapokuwa na maono au picha halisi ya biashara yako kwamba unataka baada ya miaka, hamsini, mia nk.iwe vipi, hautayumbishwa na vikwazo vya kupita utakavyokutana navyo njiani. Kuna baadhi ya vipengele vingine katika mpango wako wa biashara vinavyoweza kubadilika kulingana na muda na hiyo ndiyo tabia ya mipango, inabidi uifanyie marekebisho kila baada ya muda mfupi kulingana na hali halisi inavyojitokeza lakini pia kuna vitu vingine kama hivyo vitatu nilivyokutajia vinavyodumu kwa muda mrefu biashara yako utakaotaka idumu.

Kinacho ua biasharayingi siyo tukio moja linalotokea ghafla, hapana bali muunganiko wa matukio na makosa madogomadogo mengi ambayo kama utayawekea mpango mapema wa kukabiliana nayo basi unakuwa na uwezo wa kuyazuia kabla hayajatokea. Mpango wa biashara hukulazimisha kuifikiria biashara yako na kuielewa vizuri kwa undani kabla hata haujaanza kuifanya. Unaanza tu kuifanya, tayari unakuwa umeshaweka mpango wako kwamba wewe baada ya kuacha biashara hiyo au pengine hata baada ya kufa, ni nani utakayemuachia aendelee kuiongoza hiyo biashara. Kwa mtindo huo unaweza kuona biashara itaweza hata kudumu baada ya wewe kuondoka hapa duniani.

Katika mpango wa biashara yako usipange kufaulu tu peke yake, tambua pia kuna kuanguka na majanga mbalimbali. Hakikisha vyote unavizungumzia na kuweka mpango mbadala ikiwa vitatokea ufanyeje ili kupunguza hatari zake. Mpango wa Biashara unakuwa na vipengele muhimu vifuatavyo lakini siyo lazima uwe navyo vyote kulingana na aina na malengo ya mpango wako.

Jalada la nje
Yaliyomo
1.Dhamira kuu
2.Maelezo kuhusu biashara
3.Maelezo kuhusu bidhaa
4.Maelezo ya soko
5.Mikakati na utekelezaji
6.Utawala na wafanyakazi
7.Maswala ya fedha
Vielelezo.

Kumbuka mpango wa biashara siyo lazima uandike kwenye karatasi, unaweza tu kupanga kichwani kwako kama walivyokwisha kufanya watu wengi hapo kabla, sasa na hata baadaye. Lakini ni jambo la faida zaidi kwako ikiwa utaelewa japo kwa kusoma tu ni jinsi gani mpango wa biashara unavyokuwa.

Ni jambo zuri pia kuhakikisha mpango wa biashara yako ikiwa utataka ukupe matokeo mazuri, basi uhakikishe unauandaa mwenyewe au ikiwa atakuandalia mtu mwingine au mtaalamu, fahamu kila hatua ni kitu gani kinatakiwa kufanyika, kifupi utafiti wa vipengele mbalimbali unatakiwa uufanye mwenyewe kwani wewe mwenyewe ndiye utakayeifanya hiyo biashara na wala si yule atakayekuandikia au mtaalamu. Kwa hiyo ni muhimu sana mtu kufahamu ni kitu gani huwa ndani ya mpango wa biashara.

SOMA: Kwanini mpango wa biashara wa kuandikiwa siyo mzuri kwako?

Sisi Self Help Books Tanzania, tuna kila kitu unachohitaji kufahamu namna mpango wa biashara unavyokuwa, unavyoandikwa na hata mipango/michanganuo yenyewe halisi iliyokwisha andikwa ya biashara mbalimbali zinazofanywa hapa Tanzania.

Tuna Kitabu, MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI pamoja na  SEMINA YA MPANGO WA BIASHARA inayoendeshwa kupitia blogu maalumu ya kulipia. Unaweza kupata vitu vyote hivi, kitabu na semina kwa gharama ndogo tu ya shilingi Elfu 10, badala ya shilingi elfu 20 bei halisi kupitia email yako.


Lipa kupitia namba za simu; 0712202244  au  0765553030, jina litokee Peter Augustino Tarimo, pamoja na kutuma anani yako ya email, utatumiwa kitabu ndani ya dakika chache. Ukihitaji kitabu cha karatasi wasiliana na sisi, tupo Mbezi kwa Msuguri stendi.

0 Response to "JINSI YA KUANZISHA BIASHARA ITAKAYODUMU MIAKA 100 NA ZAIDI IJAYO"

Post a Comment