Katika Ongea na Mshauri leo hii tumepokea
swali kutoka kwa msomaji mmoja wa blogu hii, hajajitambulisha anatokea wapi ila
swali lake ametuma kwa njia ya email kama ifuatavyo na mimi hapa chini siongezi
wala kupunguza neno kwenye email hiyo;
“Naomba
kusaidiwa nawezaje kuendesha biashara yangu kwa mfumo wa kampuni? Hatua zipi
nifuate?”
NAWEZAJE KUENDESHA BIASHARA YANGU KWA MTINDO
WA KAMPUNI?
Jibu ni ndiyo, biashara yeyote ile iwe kubwa
au ndogo, ya jumla au biashara ya rejareja, utoaji wa huduma na hata biashara
ya kuzalisha bidhaa kama kiwanda, unaweza ukaiendesha kwa mfumo wa kampuni.
Kisheria mifumo ya biashara ipo zaidi ya minne lakini ile iliyozoeleka zaidi na
inayotumika mara kwa mara na watu wengi ni hii mitatu ifuatayo;
1. MTU
BINAFSI(sole proprietorship
2. UBIA(Partnership)
3. KMPUNI
YENYE DHIMA YA UKOMO(Limited company)
Kampuni kama ulivyouliza tofauti yake na
mifumo hiyo mingine miwili ni kwamba, wamiliki mnaweza kuwa ni watu 2 mpaka
watu 50 na faida yake kubwa ni kuwa mali binafsi za wanahisa hazihusiani kabisa
na zile za kampuni na haziwezi kuwajibika kulipia mdeni yaliyosababishwa na
kampuni ikitokea labda kampuni inataka kufilisika au inadaiwa. Ni kampuni
yenyewe kama kampuni itawajibika kulipa deni siyo wamiliki wake waingie
mifukoni mwao au wakauze mali zao binafsi. Kampuni huchukuliwa kama nafsi ya
mtu binafsi kisheria.
Tukirudi katika swali lako ni kwamba, hakuna
taratibu maalumu au za kipekee za uendeshaji wa biashara katika mtindo wa
kampuni isipokuwa tu maswala hayo ya kisheria yaliyotajwa. Hata hivyo kampuni
mtu unakuwa na wigo au uhuru mpana zaidi wa kuendesha biashara yako kutokana na
kuaminika zaidi na watu wakiwemo wateja wale unaofanya nao biashara, makampuni
mengine na hata wakati mwingine serikali.
Kwahiyo unaweza kuona ya kwamba kampuni inao uwezo wa kutanua biashara zake zaidi kuliko mifumo ya Mtu
mmoja na Ubia.
· Gharama
za kwanza ni zile za usajili. Gharama hizi ukilinganisha na za mifumo mingine
2, zipo juu zaidi na huhusisha shughuli nyingi za makaratasi.
· Ghrama
kwenye uendeshaji kutokana na sababu kwamba kampuni licha ya kuwa na
wamiliki/wakurugenzi mbao ndio wenye hisa, kampuni pia inatakiwa kuwa na meneja
pamoja na timu yote ya uongozi na wafanyakazi kama vile mhasibu nk.
· Ukaguzi
wa mahesabu kila mwaka na hesabu hizo kuwasilishwa kwa msajili wa makampuni. Shughuli
zote hizo zina gharama ya fedha na muda tofauti na kutumi mifumo mingine miwili
ya biashara kisheria.
HATUA
ZA KUFUATA WAKATI WA KUANZISHA KAMPUNI TANZANIA.
1) Kwanza
kabisa unapeleka majina yako matatu pale BRELA ambayo ungependa mojawapo ndilo
litumike ukianza na lile unalopenda zaidi liwe ndio jina la kampuni yako.
Sababu ya kupeleka majina matatu ni ili kama itaonekana jina la mwanzo
lilishatumika na mtu mwingine basi waangalie uwezekano wa hayo mengine 2.
2) BRELA
ndiyo taasisi inayohusika na usajili wa makampuni na pia majina ya biashara kwa
biashara ya mtu mmoja na ubia. Makao yake makuu yapo jijini Dar es salaam
katika jengo la Ushirika pale Mnazimmoja. Unaweza pia kutembelea mtandao wao
kwenye intaneti ambapo unaweza kudownload fomu za kusajili kampuni na mjina ya
biashara.
3) Jina
likishakubalika na Brela, nenda katika ofisi yeyote ile ya mwanasheria
wakuandalie katiba ya kampuni yako(Memorandum and Articles of Associations) pamoja
na kukujazia makabrasha mengine ya kisheria
na kugonga mihuri. Ikiwa wewe mwenyewe unao uwezo wa kuandaa makabrasha
hayo, kwa mwanasheria ni lazima uende kwa ajili ya kugongewa mihuri au
kusaidiwa kupitia kama kuna makosa yeyote kisheria.
4) Ukishamaliza
hapo peleka makabrasha hayo Brela, watakupa fomu za kujaza, ikiwa ni pamoja na
kulipia ada kulingana na ukubwa wa mtaji uliopendekeza wa kampuni yako. Baada
ya hapo Brela watakupa cheti chako cha usajili wa kampuni ndani ya siku 5 mpaka
7.
HITIMISHO.
Unapoanzisha ,biashara yeyote ile, cha kwanza
kabisa angalia kwanza uwezo wako uliokuwa nao hasa katika mtaji, kisha ndipo
uamue kama ni mfumo upi utakaoanza nao. Kama mtaji ni kidogo unaweza ukaanza na
mfumo wa mtu mmoja au ubia kwani unaweza kuja kubadilisha hapo baadae, lakini
kama hali kifedha inaruhusu ni vizuri zaidi ukaanza moja kwa moja na mfumo wa
kampuni.
...............................................................
Kwa vitabu vyako bora kabisa vy ujasiriamali, wasiliana nasi kwa namba 0712202244 au 0765553030 wasap 0765553030 au tembelea; SMART BOOKS TANZANIA
Mkataba kati ya kampuni ya mifugo na mawakala unakuwaje
ReplyDeleteHabari,,, Je nilazima kampuni iwe na mwanasheria ama akimaliza kaz ya kuandaa memorandum/kugonga mhur tunaachana🙏🙏
ReplyDelete