UKUTA WA RAIS MAGUFULI MERERANI MJASIRIAMALI UMEJIFUNZA KITU GANI HAPO? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

UKUTA WA RAIS MAGUFULI MERERANI MJASIRIAMALI UMEJIFUNZA KITU GANI HAPO?


UKUTA WA RAIS MAGUFULI MERERANI MANYARA MJASIRIAMALI UNAJIFUNZA NINI?
Hazijapita siku nyingi tangu Rais John Pombe Magufuli azindue rasmi ukuta unaozuia eneo la machimbo ya madini ya Tanzanite huko Mererani Simanjiro mkoa wa Manyara. Ukuta huo ulio na urefu wa kilomita 24 na nusu na kimo cha mita 3 uligharimu Taifa kiasi cha shilingi bilioni 6 huku nguvukazi iliyotumika kuujenga ikiwa ni wanajeshi  wapatao 270.


Madhumuni makubwa ya kuujenga ukuta ule ni ili kuhakikisha mapato yote yanayotokana na madini ya Tanzanite yanayosadikiwa kuwa hayawezi kupatikana katika eneo jingine lolote lile duniani zaidi ya Tanzania yanadhibitiwa vilivyo yasiibiwe wala kutoroshwa tena kinyemela na watu wasiokuwa waaminifu.


Kabla ya hapo serikali ilikuwa haipati ushuru na kodi zinazostahili kutokana na mwanya huo uliosaidia wafanyabiashara na wachimbaji wenye tamaa ya kutajirika haraka kuficha kiasi kamili cha madini yaliyokuwa yakichimbwa hapo mgodini.

Haikuwa nia ya makala yangu hii kuanza kuandika upya historia ya madini haya hapa kwani hata mgunduzi wake Mzee Jumanne Mhero Ngoma aliyeyagundua madini hayo hapo mwaka 1967 kukosa hekima za Rais Magufuli naye chupuchupu aje afe masikini. Kwanini nasema hivyo? Nasema hivi nikitaka wewe mjasiriamali unayesoma hapa ujue fika ya kwamba, mali zaweza kuwa ni za kwako, biashara unaweza kuwa unaimiliki wewe mwenyewe lakini usipokuwa makini vya kutosha katika usimamiaji wa mapato yake hakika utashanga wajanja wengine kabisa wakinufaika na jasho lako pasipo wewe kujua mpaka pale utakapokuja kujikuta ukifa fukara.


Si kama namlaumu mzee Ngoma wala serikali zilizopita hapana, bali nataka tu kuonyesha umuhimu wa hatua hii iliyochukuliwa na serikali. Nimesoma vizuri historia ya Mzee Ngoma, alikuwa na fursa nzuri sana ya kuwa bilionea lakini alizidiwa kete na wajanja waliotumia nafasi na hata jina lake kujinufaisha wengine mfano kama Wale wahindi waliomtapeli lile jiwe kubwa la kwanza kabisa la Tanzanite alilookota akichunga mbuzi, mpaka hata kesho vitukuu vyao wataishi maisha ya peponi wangali hapa duniani.

Na sisi Kama Taifa kwa upande mwingine tulikuwa na fursa nzuri kabisa ya kunufaika na utajiri huu mkubwa toka ugunduliwe na Mzee Ngoma miaka hiyo ya 60 lakini wajanja wachache kama makampuni kutoka nchini Kenya, India na nchi nyinginezo ndio waliofaidi zaidi matunda hayo.

Yote hii ilitokana na kulegeza kamba katika udhibiti au usimamizi wa rasilimali, unapolegeza kamba usipokuwa shupavu vya kutosha wanaokukodolea ‘mimacho’ wakitamani kile ulichokuwa nacho watakichukua na kukifanya kuwa mali yao. Hivyo nilitaka tu kukukumbusha wewe kama mjasiriamali katika sekta hii ya usimamizi wa mali zako wewe upoje?


Ni lazima uwe king’ang’anizi wazungu husema aggressive , kuwa ng’ang’ari kwa maana nyingine, simaanishi unyang’anye mali za watu wengine la hasha, bali namaanisha uhakikishe unalinda vilivyo mali zako kwa gharama yeyote ile hata ikiwa ni kwa kujenga ukuta kama huu wa Tanzanite Mererani. Wenzetu Wakenya wapo hivyo na ndiyo maana hata makampuni yao utakuta yapo juu sana.

Binafsi baada ya kucheki sana hii mbinu aliyoibuni Rais wetu Magufuli ya kujenga ukuta kuthibiti mapato ya Tanzanite, nilikumbuka wakati fulani nilipokuwa naendesha biashara ya duka la rejareja niliwahi kubuni kitu kama hiki na kwa kweli kilifanya kazi japo sikukitilia maanani sana wakati huo mpaka majuzi nilipokuja kukumbuka na kuona si vibaya nikashea na watu wengine nao wakakijua hususani wamiliki wa maduka ya rejareja. Kinaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti mapato ya biashara hizi ndogo.

Mfanyakazi katika biashara yako ndogo ya duka la rejareja kama ndiyo kwanza unaanza wakati mwingine hana tofauti sana na mchimbaji au mfanyabiashara asiyemwaminifu wa madini ya Tanzanite pale Mererani kwa Serikali. Mfanyakazi au msaidizi wa duka asiyekuwa mwaminifu atafanya kila njia ili akuibie senti zako kidogo ulizowekeza katika duka lako dogo bila kujali kama umemuweka pale ili msaidiane, yeye apate kidogo na wewe pia upate kidogo.


Watu wana njia nyingi za kudhibiti na kusimamia biashara zao hususani maduka haya madogomadogo ya rejareja wasiibiwe, lakini kuna hii njia mpya niliyokuambia niliibuni, sijawahi kuisikia mahali pengine popote pale niliianza mimi mwenyewe kama huu ukuta wa Mererani ulivyoanzishwa juzi.

Kwangu ilifanya kazi na nadhani kwa mtu mwingine inaweza pia ikafanya kazi pia. Nimeamua kuiita mbinu hiyo jina, “TWO IN ONE STORE MANAGEMENT SYSTEM” ni mfumo unaomwezesha mmiliki wa duka dogo la rejareja la mtaji kuanzia milioni 3 kushuka chini kuweza kudhibiti mapato yake na faida pasipo msaidizi au mfanyakazi kumuibia kirahisi. Mfumo huo unafanyakazi huku mmiliki akiwa anafanya shughuli zake nyingine bila wasiwasi wowote.

Kumbuka kinachoyaua maduka mengi madogo ni usimamizi mbovu unaopelekea wasaidizi ama wafanyakazi kudokoa mtaji na hatimaye duka kufa kabla halijavuka mtaji wa shilingi milioni 3. Sasa ‘DAWA’ huu(MFUMO) utakwenda kukusaidia kuondokana na stress zitokanazo na msaidizi asiyekuwa mwamnifu na kukuacha wewe ukielekeza nguvu katika shughuli zako bila kuhofia tena kama atakuibia na kuja kila siku asubuhi na jioni kukagua hesabu, mfumo utakupa muda wa kutosha hata wiki nzima ndipo uje kukagua hesabu zako na pia unakupa urahisi wa kubaini mapungufu yeyote yaliyotokea mara moja.


Mfumo huu unaweza kuupata kwa njia mbili, njia ya kwanza ni kwa kuununua wenyewe moja kwa moja kwa bei ya shilingi elfu 5 ambapo unapata pia na ofa ya kitabu cha MAFANIKIO YA BIASHARA YA DUKA LA REJAREJA bure kabisa.

Njia ya pili ni kwa kujiunga na Semina na masomo ya Michanganuo na mzunguko wa fedha ndani ya Group la MICHANGANUO ONLINE kwa shilingi elfu 10 ambapo unapata na ofa ya vitu vingine mbalimbali vipatavyo 10 vikiwemo vitabu vya Michanganuo ya biashara katika lugha ya Kiswahili na kiingereza pamoja na masomo yote yaliyokwishapita na semina katika group hilo. Group hili si lazima uwe unatumia wasap, hata ukiwa na email tu inatosha.

..................................................................

Kujiunga na group la MICHANGANUO ONLINE tuma namba yako ya watsap kwenye, 0765553030  au anuani yako ya Email pamoja na kiingilio sh. elfu 10 kupitia namba za simu 0712202244  au 0765553030 jina ni Peter Augustino Tarimo. 


Kupata Vitabu BORA KABISA kutoka Self help Books Tanzania, tazama hapa chini au pia unaweza ukafungua hapa katika ukurasa huu wa vitabu wa; SMART BOOKS TANZANIA kujionea vitabu zaidi.








0 Response to "UKUTA WA RAIS MAGUFULI MERERANI MJASIRIAMALI UMEJIFUNZA KITU GANI HAPO?"

Post a Comment