MWANAUME KUPUNGUA NGUVU ZA KIUME PESA NA MAISHA MAGUMU YANAVYOCHANGIA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

MWANAUME KUPUNGUA NGUVU ZA KIUME PESA NA MAISHA MAGUMU YANAVYOCHANGIA


TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa wanaume huwezi ukasema lina chanzo kimoja tu. Zipo sababu nyingi zikanazoweza zikasababisha hali hiyo kumtokea mwanaume yeyote yule katika umri wowote ingawa inawakumba zaidi wanaume waliopita umri wa miaka 40.

Kufanya tendo la ndoa na mwanamke au kitendo cha kufanya mapenzi kati ya mume na mke kunahitajika wote wawili kuwa na utulivu wa akili achilia mbali afya ya kawaida ya kimwili, mtu anaweza akafanya mapenzi wakati akiwa na malaria lakini siyo akiwa na msongo wa kimawazo. Hamu ya kufanya tendo la ndoa hutegemea sana vichocheo vilivyoko mwilini ambavyo utendaji kazi wake nao hutegemea amri zinazotolewa moja kwa moja katika ubongo wa mtu.

Kuna mahusiano makubwa kati ya tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na tatizo jingine la pesa. Na wanaume ndiyo wahanga wakubwa sana wa matatizo haya mawili kuliko hata vile ilivyokuwa kwa wenzao wanawake. Uchumi wa familia kwa mfano unapotetereka mtu wa kwanza kuangaliwa ni mwanamme.

Imejengeka akilini mwa watu wengi kuwa mama na watoto wanatakiwa kumtegemea baba. Hivyo hali ya pesa inapokuwa ngumu baba huathirika sana kisaikolojia. Mama atajitahidi kumpa maneno matamu ya mahaba usiku wawapo kitandani sambamba na staili za mapenzi za kila aina lakini katu mwanaume akili yake muda wote inakuwa ikiwaza pesa, ni namna gani  atakavyoweza kukabiliana na maisha ambayo familia inamtegemea yeye. Hata siku ya Valentine unaweza kuwakuta wapenzi beach wakifurahia mithili ya picha unayoiona mwishoni mwa makala hii lakini ajabu ni kwamba ungeweza kuwachungulia usiku wawapo chumbani picha utakayoishuhudia ni kama ile unayoiona mwanzoni kabisa mwa makala hii.

Hufika hatua kwa wanawake wengine wasioelewa tatizo hili kwenda kwa waganga wa kienyeji kutafuta dawa ya mapenzi wakihisi ndoa zao kukumbwa na jinni mahaba au hata uwezekano wa mume kuwa na nyumba ndogo au vimada nje ya ndoa, lakini kumbe hawajui ndio wanazidisha mambo kuwa mabaya zaidi kwa kuchukua pesa kidogo kwa ajili ya matumizi ya familia na kwenda kuwapelekea waganga matapeli.

Kwa mwanamke asiyekuwa mvumilivu wala kujua chanzo cha tatizo la mwanamume kupungukiwa nguvu za kiume  anaweza akachanganyikiwa sana kiasi cha kuamua kutoka nje ya ndoa yake na kwenda kulala na wanaume wengine kumbe ilikuwa ampe tu ushirikiano waweze kuondokana na hali ngumu ya kiuchumi na mambo kurudi kama zamani.

Vichocheo vinavyosababisha ashiki ya mapenzi kwa mwanaume kama testosteron huathiriwa kwa kiasi kikubwa na msongo wa mawazo. Wanaume wengi wanapokuwa na hali kama hiyo, huzidisha mashaka na kutojiamini huku akihisi kama vile tayari ameshageuka hanithi, ikishafikia hatua kama hii mwanaume inakuwa vigumu hata kumfikisha mkewe kileleni wakati wa tendo la ndoa huku na yeye akiwahi kufika kileleni isivyokawaida wakati wa tendo hilo.

Uwezo wa mwanaume kumpa mwanamke mimba unaweza usiathirike sana lakini hata hivyo wakati mwingine unaweza kupungua kutokana na ukweli kwamba ili mwanamke aweze kupata ujauzito, mbegu ya mwanaume na yai la mwanamke ni lazima viungane katika mji wa mimba lakini kwa bahati na sibu, hauwezi ukasema kwa uhakika kabisa kwamba leo hii X na Y wakijamiiana basi mimba lazima itunge japo tunaweza tu kubashiri.

Kwa hiyo mimba ili itunge wanandoa au wapenzi hawana budi kujamiiana mara nyingi zaidi siku wanazobashiri kutafuta ujauzito. Sasa utaona kwamba baba kama anakuwa na tatizo hili la msongo wa mawazo kutokana na matatizo ya kifedha basi hataweza kushiriki kitendo hicho mara nyingi kama inavyotakiwa na moja kwa moja kupelekea pia tatizo la mwanamke kushika mimba kuweza kutokea.

Wanaume wengi wanaopatwa na tatizo hili badala ya kusaka suluhisho la kudum , hujidanganya kwa utatuzi wa muda mfupi kwa mfano kutumia dawa za kutibu upungufu wa nguvu za kiume kama Viagra, dawa za kienyeji mfano mkuyati na mitishamba ya kila aina, dawa za kichina zinazotibu upungufu wa nguvu za kiume, pamoja na vilevi mbalimbali mfano pombe zenye spiriti kama vile viroba serikali ilivyopiga marufuku na hata pombe nyinginezo za chupa zinazotumika mpaka sasa.

Hutumia pia kwa wingi sana vyakula kama vile, mihogo mibichi, nazi, karanga mbichi, mlenda, mayai, vyakula vya baharini kama pweza, ngisi, supu au mchuzi wa pweza, samaki nk. Vyakula hivi na madawa kweli vina uwezo wa kumpa mtu nyege au ashki ya muda mfupi lakini haviwezi kuwa na uwezo wa kumuondolea tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume moja kwa moja kama chanzo chake ni msongo wa kimawazo.


Ikiwa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa mwanaume linatokana na sababu za msongo wa mawazo unaosababishwa na matatizo ya pesa au shida za kiuchumi inafaa zaidi mwanamume na hasa ikiwa kama ameoa, yeye na mke wake wakae chini na kuanza kulitafakari tatizo lililokuwa mbele yao  na kubuni njia za kuweza kulitatua. Wanandoa wanaweza wakaazimia kubuni miradi midogomidogo kama ile iliyoelezwa katika kitabu hiki cha MIFEREJI 7 YA PESA, ili kuongeza zaidi kipato cha familia badala ya kutegemea tu shughuli zao za kawaida za msingi walizozoea.

Kwa njia ya majadiliano kati ya mwanaume na mwanamke, tatizo la upungufu wa nguvu za kiume linaweza hata likatoweka lenyewe bila ya matibabu au hata kabla ya kuanza kuchukua hatua za kusaka utatuzi wenyewe wa kiuchumi kwani matatizo ya nguvu za kiume mara nyingi huchangiwa zaidi na sababu za kisaikolojia kuliko hata sababu nyingine zote kwa pamoja. Mwanamume inawezekana wakati mwingine hata ni sababu za hofu tu ya kuona labda mkewe atamfikiriaje pindi anapokuwa na dalili za tatizo hili, ndiko kunakosababisha tatizo lizidi kuwa kubwa.

……………………………………….
Mpenzi msomaji, Nakukaribisha katika Group letu la masomo ya kila siku ambapo tunajadili, jinsi ya kuboresha mizunguko ya pesa kwenye biashara zetu pamoja na kuchambua michanganuo ya biashara bunifu zilizo na fursa kubwa ya kutengeneza faida. Tunapata pia wasaa wa kushirikishana wenyewe fursa mbalimbali za kimasoko kwa biashara zetu.

Mbali na masomo hayo ya kila siku pia mara ujiungapo tu hivi tunakutumia offa ya vitu vifuatavyo bila malipo ya ziada;
1.  Kitabu cha MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI katika lugha ya kiswahili.

2.  Kitabu maarufu zaidi cha michanganuo" HOW TO WRITE A BUSINESS PLAN kwa kiingereza.Kinatumiwa na karibu vyuo vikubwa vyote duniani.

3.  Templates/Vielezo kwa ajili ya kurahisisha kazi ya kuandika mpango wako wa biashara, unajaza tu taarifa kuhusu biashara yako basi umemaliza.

4.  Kifurushi chenye michanganuo kamili 3, kuku wa mayai wa kisasa, kuku wa mayai wa kienyeji na kuku wa nyama wa kisasa,(ofa yake ni ya muda mfupi sana kitaondolewa karibuni)

5.  Masomo yote ya semina zilizopita.

Ada ni shilingi elfu 10, namba za malipo ni 0712202244 au 0765553030 jina Peter Augustino Tarimo

Whatsapp: 0765553030, tuma ujumbe NIUNGANISHE GROUP LA MICHANGANUO ONLINE Baada ya kulipia. Usisahau na anuani ya GMAIL kwa ajili ya kukuunganisha na blogu ya private.

Ikiwa hutumii whatsapp hamna shida kwani masomo haya pia yanatumwa kwa njia za email na katika blogu ya private kea ajili ya wanagroup.   

0 Response to "MWANAUME KUPUNGUA NGUVU ZA KIUME PESA NA MAISHA MAGUMU YANAVYOCHANGIA"

Post a Comment