Kuna makosa ambayo wenye maduka wengi au biashara zingine ndogondogo huyafanya
pasipo kufahamu kuwa yanawafanya wateja waondoke huku wakiwa hawajaridhika, makosa
hayo yanakimbiza wateja pasipo wewe kujua, mteja aliyekasirika siyo tu atahama duka na kwenda kununua kwingineko, bali pia atakwenda kuwatangazia
na watu wengine wengi juu ya ubaya wako na kufanya nao wakose moyo wa kuja kununua dukani kwako.
Kwa kuyafahamu
makosa hayo, unaweza ukayakwepa na kuelekezea nguvu zako zaidi kwa yale matendo
tu yanayoleta wateja katika biashara yako.
1. Bei
isiyofaa; kushindwa kuweka bei
muafaka inayoendana na soko, wateja watakimbilia kwingine.
2. Kutoa
huduma mbaya kwa wateja, mfano
ni kauli na lugha kama hizi hapa chini;
“Mkopo amesafiri subiri mpaka atakaporudi”
“ Njoo na bibi yako mzaa babu ndipo
nikukopeshe”
“Hili siyo shirika la kukopesha jaribu kwingine tafadhali……”
“ Sina chenji
katafute kwanza chenji ndipo uje
nikuuzie”
“ tunatoa huduma za uuzaji wa vocha peke yake hapa, kuingiza ni juu yako
mwenyewe”
“Kakuambia nani hapa tunauza sigara; hili siyo
duka la walevi hebu ondoka hapa upesi”
“ Hatuna
vifungashio vya bure vipo vya
kununua tu”
Tafuta lugha nzuri kumfanya mteja atambue
kwamba sera ya duka lako hairuhusu kukopesha na siyo kutoa lugha itakayomfanya
mteja kamwe asiwe na hamu tena ya kurudi siku nyingine dukani kwako.
Sikatai kwamba imani yako au hata kiafya
hupendi kuuza vileo na sigara, lakini kwani walevi na wavutaji sigara huwa
hawana mahitaji mengine? Na ukimjulisha kwa lugha ya upole kuwa huuzi vitu
hivyo kwani hatakuelewa mpaka umuwekee mabango ya kumdhihaki?
3. Mandhari
mbaya ya duka: mpangilio wa
vitu usiovutia pamoja na uchafu kama vumbi kwenye bidhaa, sakafuni na katika mazingira
yote ya duka kwa ujumla.
4. Kukopesha
bila tahadhari; unaweza
kudhania labda kuwakopesha wateja, bila ya kuchukua tahadhari ndiyo itasaidia
wasikukimbie, kumbe ndiyo umewapa tiketi ya kubadili hata njia wanayopita kila
siku na kwenda kununua wasikodaiwa.
5. Kutokuwafahamu
washindani wako vizuri, udhaifu
na uwezo waliokuwa nao.
6. Kutokuwa
na uelewa wa bidhaa unazouza:
inatakiwa kila bidhaa angalao ufahamu
sifa zake, ubora, tarehe ya mwisho kutumika, pamoja maelezo yake jinsi ya
kuitumia ili uweze kumtoa mteja wasiwasi anapotaka kununua.
7. Uwongo:
kuwadanganya na kuwaongopea
wateja juu ya sifa na ubora wa
bidhaa.
8. Kutokufuata
sheria za nchi na mamlaka husika:
Utafuatwafutwa jambo litakalokufanya pia kila mara uwe unafunga funga duka lako ovyo na hatimae wateja
kukukimbia.
9. Uaminifu; mteja kwa bahati mbaya amesahau labda chenji
yake, simu au hata mwavuli aliokuja nao pale dukani, baada ya dakika kadhaa
anarudi huku akihema wewe unamwambia hukuviona wakati ukweli ni kwamba
umeshavificha. Hiyo siyo tabia nzuri kabisa, na mteja kama huyo umempoteza
daima.
10. Kubandika
matangazo ya ajabu ajabu kama
vile yanayokashifu imani na dini za watu wengine, ushabiki wa michezo n.k.
usipende kuanika ovyo msimamo wako upo upande gani kwani wewe unawahitaji
wateja kutoka pande zote. Kutangaza hadharani upande uliko kutasababisha wale
wateja wenye mlengo au imani tofauti na
wewe wawe wazito kuja kukuungisha. Hata kama wewe ni mkereketwa wa itikadi au
madhehebu fulani, kuweka miziki au kanda za mawaidha ya imani yako huku
ukifungulia sauti ya juu sana, siyo jambo zuri labda tu duka lenyewe liwe ni duka maalumu la kuuza CD na
kanda za imani hiyo.
11. Kuweka
msaidizi asiyefaa: Msaidizi au
mfanyakazi asiyetambua wajibu wake ni kikwazo kikubwa katika biashara za aina
zote, mpe mafunzo au maelekezo ya mara kwa mara juu ya huduma bora kwa mteja
ukiona haelekei ni bora ukamuondoa kabla hajakufukuzia wateja wako.
12. Jina
lisilofaa: mfamo utakuta mtu
kaandika bango la duka lake jina linaloelezea ama kuwa na nembo za kutisha kama vile,
MAFIA, ALQAEDA, PANYAROAD, nk. Jina linawakilisha picha ya biashara yako
nzima hivyo ni lazima liwe zuri na lenye maana inayokubalika na kila mtu.
............................................................................
Ndugu msomaji wa makala hii, kitabu cha “MAFANIKIO YA BIASHARA
YA DUKA LA REJEREJA” kipo katika mifumo yote, softcopy na hardcopy. Kitabu hiki
kimebeba uzoefu halisi wa mwandishi kwenye biashara hii kwa miaka 12, siyo
simulizi za kutunga wala utafiti wa kwenye vitabu, (it’s a real experience) Maswali yote yanayopasua watu wengi vichwa
na kushindwa kumudu kuifanya biashara ya duka au biashara nyingine zozote za
rejareja kwa ufanisi unaotakikana yamejibiwa kwa ufasaha.
HARDCOPY ni
sh. Elfu 16 na utaletewa popote pale ulipo Dar es salaam. Mikoani tunatuma kwa
njia ya basi lakini gharama za usafiri zitaongezeka, Mikoa mingi tunatuma kwa sh. 26,000/= jumla vyote kitabu na usafiri ndani yake.
SOFTCOPY ni
shilingi elfu 6 tu popote pale ulipo, ukishalipia, unatuma email yako na meseji
uliyotuma pesa kisha tunakutumia kitabu unadownload na kusoma katika simu yako
au kompyuta.
Usisahau pia semina kwenye WHATSAPP bado
zinaendelea kila saa 3 - 4 usiku, karibu sana ujiunge leo.
SIMU:
0712202244
WHATSAPP: 0765553030
JINA: Peter Augustino Tarimo
0 Response to "MAKOSA 12 YATAKAYOFUKUZA WATEJA DUKANI KWAKO NA KUDHANI UMELOGWA. "
Post a Comment