KANUNI KUU YA MAFANIKIO DUNIANI ILIYO KUBWA KUSHINDA ZOTE | JIFUNZE UJASIRIAMALI

KANUNI KUU YA MAFANIKIO DUNIANI ILIYO KUBWA KUSHINDA ZOTE

JIFUNZE KUTOKA KWA WALE WALIOFANIKIWA

Watu wote Duniani waliowahi kufanya tafiti mbalimbali kuhusiana na suala la mafanikio ya watu, katika majibu yao yote inashangaza sana kukuta kwamba majibu hayo yanaweza yakafupishwa katika muhtasari wa sentensi moja tu, tena yenye maneno machache sana tutakayokwenda kuitazama katika makala hii ya leo. Sentensi hiyo ni hii hapa chini;

JIFUNZE KUTOKA KWA WALE WALIO NA UZOEFU.

Sentensi hii unaweza ukaamua kuitamka kwa kutumia maneno tofauti lakini bado ikaendelea kubakia na maana ileile, unaweza ukasema hivi; JIFUNZE KUTOKA KWA WALIOFANIKIWA, JIFUNZE KUTOKA KWA WALIOKUTANGULIA, JIFUNZE KUTOKANA NA MAKOSA YA WENGINE, JIFUNZE KUTOKA KWA MABINGWA. nk.

Utajifunza vipi kutoka kwa wale walio na uzoefu?
Ni swali watu wengi sana hujiuliza, kwa mfano hata wapo watu wengine huwa hawataki kabisa kusikia simulizi za mafanikio ya watu mashuhuri, wakiamini kwamba ili waweze kujifunza namna walivyofanikiwa watu hao ni lazima kwanza wakutane nao wenyewe ana kwa ana na hata ikiwa ni kitabu kinachowahusu basi pia ni lazima kitabu hicho awe amekiandika mwenyewe mtu huyo aliyefanikiwa. Lakini unaweza ukajiuliza, ni watu wangapi waliofanikiwa huandika vitabu juu ya maisha yao wenyewe na njia walizopitia kufanikiwa kimaisha? Jibu ni kwamba, ni wachache sana. Kwa hiyo penda tusipende ni lazima tu tusome vitabu, majarida au taarifa zinazowahusu watu hao ikiwa tutataka kujifunza mambo yao jinsi walivyofanikiwa, bila kujali kama taarifa hizo wameandika wao wenyewe au la.

SOMA: Ni kitabu gani hautakisahau maishani?

Kazi ya waandishi wa habari, waandishi wa vitabu au hata waandishi wa kwenye mitandao ya kijamii ni kuandika na kutafiti na wala siyo kile wanachokiandika basi ukute kinawahusu wao moja kwa moja . Mtu mwingine anaweza kuona umeandika kuhusiana na mafanikio, yeye moja kwa moja anakimbilia kuuliza, “ ‘Mwandishi hebu tueleze wewe umefanikiwa kiasi gani?’ au ‘nataka kujua mafanikio yako yakoje’

Si vibaya kuyajua lakini yafaa mtu kama huyo akumbuke kwamba kazi kubwa zaidi ya wandishi au watafiti ni ile kazi ya uandishi au utafiti wanaoufanya na mafanikio yao  ni kuandika au kufanya utafiti mzuri wenye faida kwa yule atakayeusoma au kuutumia. Nikiandika jambo likikusaidia basi ujue huko ndiko kufanikiwa kwangu. Kwa hiyo bila kuwepo kwa watafiti na waandishi ingelikuwa vigumu sana watu kujifunza kutoka kwa watu waliofanikiwa. Tunajifunza kupitia kazi zao, ungewezaje kuzijua habari za kina Bill Gates, Mzee Mengi, Mo, Mark Zuckerberg na wengineo, wakati hata kuonana nao ana kwa ana hujawahi?

SOMA: Kijana wa umri mdogo anaweza kuanzisha biashara na ikafanikiwa?

Kwanini inapendekezwa watu kujifunza kutoka kwa walio na uzoefu?

Nilitoka kwenye mada kidogo lakini hebu turudi tena. Sababu kubwa kwanini ujifunze kutoka kwa wale walio na uzoefu kama ule unaotamani na wewe kuwa nao, kanuni kuu kuliko kanuni zote za mafanikio nitazieleza katika mfano huu; Kwa mfano watu wote waliofanikiwa wana tabia zinazofanana, hata ikiwa siyo kwa asilimia mia moja lakini angalao zinafanana. Na hivyohivyo ndivyo ilivyokuwa kwa watu walioshindwa pia nao huwa wana tabia fulani zinazofanana. Kupitia maandishi mbalimbali, hotuba zao, historia zao, na taarifa zote kuwahusu imegundulika tabia za watu waliofanikiwa kuwa ni hizi zifuatazo;

1.  Walitumia muda wao kwa uangalifu mkubwa sana na kuweza kukamilisha mambo mengi ndani ya muda mfupi ukilinganisha na watu wengine wa kawaida.

2.  Hutenda kwa ufamisi mkubwa kazi zao, kwa usahihi na katika njia ifaayo huku muda wote wakitafuta njia  za kuboresha kile wanachokifanya kwa ajili ya kupata matokeo bora zaidi. Kutokana na ubora huo wa kazi na matokeo mazuri watu hawa hulipwa mishahara mizuri au kupata faida nyingi kutokana na biashara zao.   

Hata wewe na mimi tunaweza kutumia njia za wale waliofanikiwa kuboresha maisha yetu kwa kupitia kanuni hii ya kujifunza kutoka kwa wale waliofanikiwa au wenye uzoefu kutuzidi katika zile fani tunazotamani na sisi kuja kufanya vizuri siku moja. Ili kurahisisha kazi hii, ukiona huwezi kuonana moja kwa moja na mtu mwenye uzoefu na fani husika, basi tafua machapisho kama vile vitabu nk. kuhusiana na mtu huyo au fani unayotamani kufanya vizuri.

SOMA: Siri za matajiri na waliofanikiwa maishani.

Nitatoa mfano hapa, tuseme labda wewe unatamani kufanikiwa katika biashara ya ufugaji wa kuku, wanaweza kuwa ni wa nyama, kuku wa mayai, kuku chotara au hata kuku wa kienyeji, mtafute mtu anayefanya biashara hiyo moja kwa moja ujenge naye ukaribu, au ikishindikana basi, jitahidi upate machapisho mbalimbali yanayohusu biashara ya ufugaji wa kuku wa aina zote, michanganuo ya ufugaji wa kuku wa aina mbalimbali  na hata vitabu vyenye habari za kuku vilivyoandikwa na watu tofauti tofauti.

Kwa njia hiyo utafahamu kila kitu walichofanya wale waliowahi kufuga kuku na wewe bila ya kupoteza muda mwingi ukifanya “trial and error” au ukijaribu kufahamu ni kipi kinachofanya kazi na ni kipi kisichofanya kazi, utajikuta umepitia njia fupi ya mkato kabisa katika kuyafikia mafanikio kwenye ufugaji wa kuku iwe ni wa mayai, nyama, wa kienyeji au hata kwa ajili ya kutotolesha vifaranga.

Hatua inayofuata, amua sasa ni ufugaji wa kuku wa aina gani unaotaka kufanya, kuku wa nyama, kuku wa kienyeji, au kuku wa mayai? Baada ya hapo tekeleza mpango wako sasa ukiwa na taarifa zote muhimu kuanzia mchanganuo wote wa gharama na faida ya mradi mzima.

……………………………………………………

Ndugu msomaji wa makala hii, nimekuandalia kifurushi cha michanganuo kamili mitatu ya biashara za ufugaji wa kuku, kuku wa nyama, kuku wa kienyeji wa mayai na kuku wa kisasa wa mayai kiitwacho(MKOMBOZI CHICKS PLAN 3PACKS). Michanganuo hii ni kamili(full) ina kila kitu kuanzia wazo lenyewe la ufugaji, utekelezaji wote, mpaka mchanganuo wote wa hesabu za gharama mbalimbali na mapato yanayotokana na biashara hii.

Michanganuo hii inajibu maswali mengi wafugaji wapya wa kuku na hata wale wazoefu wanayojiuliza mara kwa mara kama vile, nahitaji kiasi gani cha mtaji kuanza kufuga kuku 100, 200, 500 nk., gharama zote za mradi ni kiasi gani tangu kuanza mpaka mwisho, ni mbinu gani za kutumia ili kupunguza gharama za ufugaji wa kuku, ni vyakula gani vinavyotakiwa kulisha kuku wa aina mbalimbali? Kati ya kuku wa kisasa na wa kienyeji, ni yupi aliye na faida zaidi, kati ya kuku wa nyama na wa mayai ni yupi anayelipa zaidi nk.

Bei ya kifurushi hiki ni shilingi elfu 10, na ukishalipa unapata na offa ya kuingia katika GROUP la WHATSAPP la MICHANGANUO ONLINE ambalo ndani yake kunapatikana watu wenye uzoefu wa biashara mbalimbali ikiwemo ufugaji wa kuku wa aina zote. Unapewa pia na offa ya vitabu na vitu vingine mbalimbali yakiwemo masomo yote yaliyopita. Ofa hizi ni za muda maalumu tu, muda ukiisha kila kitu kitaendelea kuuzwa peke yake kama kilivyo, hivyo wahi usije kuchelewa. Ikiwa hutumii whatsapp hamna shida kwani tunatumia njia 3, email pamoja na Blog ya private.

SIMU:              0712202244  AU  0765553030
WHATSAPP:   0765553030
JINA:               Peter Augustino Tarimo  

Kwa vitabu vya biashara, ujasiriamali na maendeleo binafsi tembelea SMART BOOKS TANZANIA.

0 Response to "KANUNI KUU YA MAFANIKIO DUNIANI ILIYO KUBWA KUSHINDA ZOTE"

Post a Comment