UZURI WA MAFUNZO YA MAPISHI YA VITAFUNWA, CHAKULA LAMBALAMBA, WHATSAP MTANDAONI | JIFUNZE UJASIRIAMALI

UZURI WA MAFUNZO YA MAPISHI YA VITAFUNWA, CHAKULA LAMBALAMBA, WHATSAP MTANDAONI

Mapishi ya sambusa chapati na mikate
Kabla mitandao ya kijamii haijashika kasi, miaka ya nyuma kidogo, mtu ilikuwa kujifunza ujuzi mbalimbali kama vile jinsi ya kupika vyakula vya aina mbalimbali vikiwemo vitafunio vya chai, ice cream, koni, lambalamba, na hata pilau na biriani ni lazima kwanza utafute chuo kilichotoa mafunzo ya upishi au wakati mwingine umtafute mtaalamu aliyekwishapitia mafunzo hayo akufundishe. Kulikuwa na vitabu pia, japo upatikanaji wake ulikuwa mgumu kidogo. 

Mambo yamebadilika sana siku hizi, binafsi siku moja katika pitapita yangu mitandaoni nikakutana na tangazo la kozi za utengenezaji vyakula mbalimbali kwa njia ya whatsapp, nikawa najiuliza watu hawa wanafundishaje mtu akaelewa? au labda wanatumia njia ya video? Japo sikuwa na interest ya kujifunza mimi binafsi lakini nikasema kama ni mafunzo ya kweli basi nitampa ‘wife’ ayafuatilie.


Mapishi ya chapati kwa mfano ni kitu cha kawaida sana katika kaya nyingi Tanzania lakini chagamoto kama vile chapati kuwa kavu na ngumu ni moja ya suluhisho wakufunzi hawa wa kwenye whatsapp intaneti hutoa kirahisi mno! Sikuwa nalijua hilo kabla nikidhani ni wajanja wajanja tu wanaotaka kula hela za watu kumbe wanamaanisha kile wanachokisema. Siyo kila watoa mafunzo mtandaoni ni matapeli.


Baada ya kujiunga wasap na kuingizwa katika group la masomo, wakufunzi wake walianza kunitumia maelezo mbalimbali na picha na namna ya kupika vitu mbalimbali kuanzia, bagia za dengu, mkate mwupe, mkate wa brown, sambusa, maandazi, mkate wa kumimina, chapati za maziwa, half cake, kababu za nyama na mayai, maandazi ya kuoka, donuts, visheti, vitumbua, kachori, kalimati,  skonzi, chapati, nk. Wana masomo mengine pia ya vyakula na vitu vinavyouzwa katika biashara nyingi ndogondogo kama vile pipi, biskuti, koni, lambalamba, zulia, sabuni, barafu, kashata, na mapishi ya vyakula mbalimbali vikiwemo pilau, biriani nk.


Maelekezo yale yalikuwa mafupi na yanayoeleweka vizuri kiasi kwamba shakashaka niliyokuwa nayo juu ya mafunzo haya ziliisha kabisa. Wanakupa mahitaji yote, Maelezo na mwisho jinsi ya kuandaa. Nilimfuata wife na kumjulisha juu ya mafunzo yale akafurahi sana. Hakuamini macho yake kwani vitu vingi ambavyo alikuwa akiviona tu vikiuzwa mabarabarani sasa aliweza kuvipika mwenyewe bila wasiwasi wowote. Na ukiwa na dukuduku lolote au labda kitu fulani tuseme hamira huelewi utatumia ya aina gani, ya chenga au ya unga, basi unauliza na mkufunzi anakupa maelekezo ya kutosha.

Mafunzo kama haya ni fursa kubwa sana kwa mjasiriamali mdogomdogo anayehangaika kupata mtaji. Kwa kuwa anao mtaji kidogo sana, hawezi akaanzisha biashara kubwa itakayohitaji vitu vingi vya kuanzia lakini pia hata ikiwa anataka kuanzisha biashara ndogondogo ya chakula inayohusisha aina hizo za vyakula au vitafunwa, masomo haya ya gharama nafuu na yasiyohitaji muda maalumu bali hitaji lake tu ni mtu kuwa na simu yenye intaneti hasa smartphone, yanaweza kuwa msaada mkubwa sana kumtoa pale alipo na kumfikisha mahali pengine juu zaidi.

Kitu cha msingi nilichoona mtu anaweza akafanya ikiwa anataka kuyatumia mafunzo hayo kuanzisha biashara ndogo ni kujifunza kitu ambacho anajua ataweza kupata soko lake kwa urahisi. Kila mtu hukaa mazingira tofauti na mwenzake, inawezekana eneo unaloishi wewe ukiuza mandazi yanatoka sana lakini skonzi haziwezi kutoka kabisa, halikadhalika na mwingine yawezekana eneo analokaa vitu kama sambusa na chapatti vina soko la uhakika ushinda vitu vingine kwa hiyo hapo ni suala la kufanya utafiti wa soko kwanza hata kabla ya kuanza mafunzo yenyewe kusudi uwe na uhakika unakwenda kujifunza nini kukepa gharama ya muda na pesa ya kujifunza kila kitu hata kile ambacho huendi ‘kudili’ nacho.

Siyo vibaya pia ukafanya mchanganuo wa biashara yako ndogo kwa kuainisha mahitaji yote na bei zake, kisha ukaorodhesha mbinu utakazotumia kufanikisha uuzaji wa chakula au vitafunwa vyako kama vile, “nitatembeza kwa chombo safi mtaani huku nikitangaza, vitafunwa, vitafunwa”, “Nitaweka chombo safi barazani wateja wafuate wenyewe watakapoviona” au “Nitatembeza katika maduka ya rejareja kuomba wanipe oda ya kuwapelekea kwa jumla” Usisahau pia kukisia hesabu zako ikiwa utapata faid kiasi gani kwa siku, wiki na mwezi, ukiona hautaweza kupata faida kulingana na mahitaji yote utakayotakiwa kuwa nayo basi ni bora ukafikiria tena upya ikiwa utabadilisha aina ya chakula au vitafunwa hivyo au kutafuta biashara nyingine kabisa.


Utengenezaji wa vitu hivi sijaona mahali ambapo wanasema ni lazima utumie mashine au vyombo vya gharama kubwa tofauti na maneno ya watu wengi mitaani kwamba kuoka kitu kama mkate au skonzi ni lazima uwe na ma oven makubwa makubwa, wanapendekeza mashine na vifaa mbadala kabisa kuanzisha kiwanda chako kidogo cha utengenezaji wa vyakula.


Nimetaja kiwanda makusudi kwani huwa Napata maswali mengi sana toka kwa wajasiriamali wadogo wanaotaka kuanzisha viwanda vidogovidogo lakini wanakuulizia habari za ni wapi watapata mashine kubwakubwa ambazo najiuliza, watamudu vipi kuzinunua hata ikiwa watajua ziliko? Siyo vibaya kujua zinapatikana wapi, lakini ninachomaanisha hapa ni kuwa mfanya biashara mdogo fikiria makubwa lakini “just start small”, anza kwa kiwango kidogo kwanza ili usijeukakata tamaa njiani mambo yakionekana kuwa magumu kidogo kwani safari ya ujasiriamali ina kupanda na kushuka kabla hujafika kileleni.

……………………………………………………


Ndugu msomaji wa makala hii, unaweza kupata mafunzo yetu kwa kina kupitia vitabu mbalimbali vifuatavyo. Softcopy kwa njia ya email ni sh. elfu 10 hicho cha kwanza, elfu 5 cha pili na elfu 3 cha tatu. 

Hardcopy ni sh. elfu 20, elfu 10 na elfu 5. Ulkiletewa ulipo Dar utaongeza sh. elfu 2. Mikoani agiza mtu anayefika Dar au tunaweza kukutumia kwa basi.

SIMU:        0712202244
WASAP:   0765553030


 1. 



Kwa maelezo na vitabu zaidi tembelea ukurasa huu ufuatao, 

0 Response to "UZURI WA MAFUNZO YA MAPISHI YA VITAFUNWA, CHAKULA LAMBALAMBA, WHATSAP MTANDAONI"

Post a Comment